Inaonyesha machapisho yaliopangwa kwa tarehe ya hoja neema. Panga kwa uhusiano Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliopangwa kwa tarehe ya hoja neema. Panga kwa uhusiano Onyesha machapisho yote

12.29.2019

Watu Wote wa Mungu Wamsifu Kikamilifu

 

Latest Swahili Praise and Worship Song | "Watu Wote wa Mungu Wamsifu Kikamilifu" | Tenzi ya Rohoni


Tumenyakuliwa mbele ya Mungu.
Tunajiunga na karamu ya wingi, tuna furaha sana.
Tunafurahia maneno ya Mungu na tunaelewa ukweli,
roho zetu zimeokolewa na tunahisi huru.
Mioyo yetu imejaa shukrani na sifa.
Hatuna budi ila kuimba.
Furaha iliyo mioyoni mwetu haiwezi kuelezeka.
Sifu na uruke kwa furaha.
Mungu anastahili heshima na utukufu.
Mapenzi ya Mungu yanafanyika hapa duniani.
Watu wote wa Mungu wamsifu kikamilifu.

12.14.2019

Matendo maovu ni yapi? Maonyesho ya matendo maovu ni yapi?

Maneno Husika ya Mungu:


Ni kiwango kipi ambacho kulingana nacho matendo ya mtu yanatathminiwa kuwa mema au mabaya? Inategemea na iwapo katika fikira, maonyesho, na matendo yako, una ushuhuda wa kutia ukweli katika vitendo na wa kuishi kwa kudhihirisha uhalisi wa ukweli au la. Ikiwa huna uhalisi huu au huishi kwa kudhihirisha hili, basi bila shaka wewe ni mtenda maovu.

11.30.2019

Kuna tofauti zipi kati ya mabadiliko ya tabia na tabia nzuri?

Maneno Husika ya Mungu:

Mabadiliko katika tabia hasa huhusu mabadiliko katika asili ya watu. Mambo ya asili ya mtu hayawezi kuonekana kutoka kwa mienendo ya nje; yanahusisha moja kwa moja thamani na umuhimu wa kuwepo kwao. Yanahusisha moja kwa moja maadili ya mtu katika maisha, mambo yaliyo ndani kabisa ya nafsi yake, na kiini chake.

11.22.2019

Ni watu wangapi wa dini watakaorudi kwa Mungu katika maafa?

Maneno Husika ya Mungu:

Ninapougeuza uso Wangu kwa ulimwengu kuzungumza, binadamu wote wanasikia sauti Yangu, na hapo kuona kazi yote ambayo Nimefanya katika ulimwengu. Wale wanaoenda kinyume na mapenzi Yangu, hivyo ni kusema, wanaonipinga kwa matendo ya mwanadamu, watapitia kuadibu Kwangu.

11.13.2019

Ni thawabu ipi inayopewa wanawali wenye hekima? Wanawali wapumbavu wataanguka katika maafa?

Ni thawabu ipi inayopewa wanawali wenye hekima? Wanawali wapumbavu wataanguka katika maafa?
  Maneno Husika ya Mungu:
“Kuifuata kazi ya Roho Mtakatifu” kuna maana ya kufahamu mapenzi ya Mungu leo, kuweza kutenda kwa mujibu wa masharti ya sasa ya Mungu, kuweza kutii na kumfuata Mungu wa leo, na kuingia kwa mujibu wa matamshi mapya zaidi ya Mungu. Huyu pekee ndiye mtu ambaye hufuata kazi ya Roho Mtakatifu na yuko ndani ya mkondo wa Roho Mtakatifu. Watu hao hawawezi tu kupokea sifa za Mungu na kumwona Mungu, lakini wanaweza pia kujua tabia ya Mungu kutoka kwa kazi ya karibuni zaidi ya Mungu, na wanaweza kujua dhana na ukaidi wa mwanadamu, na asili na kiini cha mwanadamu, kutoka kwa kazi Yake ya karibuni zaidi; pia, wanaweza kutimiza polepole mabadiliko katika tabia yao wakati wa huduma yao.

10.28.2019

Wanawali wenye hekima ni nini? Wanawali wapumbavu ni nini?

 
    Maneno Husika ya Mungu:
    Zamani, watu wengine wamefanya utabiri kuhusu “mabikira watano wenye busara, mabikira watano wapumbavu”; ingawa utabiri huo si sahihi, si wenye makosa kabisa, kwa hiyo Naweza kuwapa ninyi maelezo fulani. Mabikira watano wenye busara na mabikira watano wapumbavu hakika hawawakilishi idadi ya watu, wala hawawakilishi watu wa aina moja mtawalia.

10.23.2019

Mtu anawezaje kupata kazi ya Roho Mtakatifu?

Maneno Husika ya Mungu:
Kazi ya Roho Mtakatifu inabadilika kutoka siku hadi siku, ikipanda juu kwa kila hatua; ufunuo wa kesho unakuwa hata juu kuliko wa leo, hatua kwa hatua ukikwea hata juu zaidi. Hii ndiyo kazi anayotumia Mungu kumkamilisha mwanadamu. Iwapo mwanadamu hawezi kwenda sambamba, basi anaweza kuachwa nyuma wakati wowote. Kama mwanadamu hana moyo wa kutii, basi hawezi kufuata hadi mwisho. Enzi ya kale imepita; hii ni enzi mpya. Na katika enzi mpya, kazi mpya lazima ifanywe.

10.21.2019

Kuna tofauti ipi kati ya mtumishi mwema na mtumishi muovu?

Maneno Husika ya Mungu:
Kazi ya mtenda kazi mwenye sifa inaweza kuwaleta watu katika njia sahihi na kuwaruhusu kuzama kwa kina katika ukweli. Kazi anayofanya inaweza kuwaleta watu mbele ya Mungu. Aidha, kazi anayofanya inaweza kutofautiana kutoka kwa mtu hadi mtu mwingine na wala haifungwi na kanuni, inawapa watu uhuru. Aidha, wanaweza kukua katika uzima kwa taratibu, wakiendelea kukua na kuzama ndani kabisa katika ukweli. Kazi ya mtenda kazi asiyehitimu haifikii kiwango hiki; kazi yake ni ya kipumbavu.

10.18.2019

Kumfuata Mungu ni nini?

Maneno Husika ya Mungu:

      Kilicho na umuhimu mkuu katika kumfuata Mungu ni kwamba kila kitu kinapaswa kuwa kwa kadri ya maneno halisi ya Mungu: Kama unafuatilia kuingia katika uzima au kutimiza mapenzi ya Mungu, kila kitu kinapaswa kulenga maneno halisi ya Mungu. Kama kile ambacho unawasiliana kwa karibu na kufuatilia hakilengi maneno halisi ya Mungu, basi wewe ni mgeni kwa maneno ya Mungu, na umeondolewa kabisa katika kazi ya Roho Mtakatifu.

10.16.2019

Unafiki ni nini?







Maneno Husika ya Mungu:
Ufafanuzi wa neno “Mfarisayo” ni upi? Ni mtu ambaye ni mnafiki, ambaye ni bandia na anajifanya katika kila kitu anachofanya, akijifanya kuwa mwema, mwenye fadhila, na mzuri. Je, hivyo ndivyo alivyo kwa kweli? Yeye ni mnafiki, na hivyo kila kitu kinachodhihirika na kufichuliwa ndani yake ni cha uongo, yote ni kujifanya—sio hali yake ya kweli. Hali yake ya kweli imefichwa ndani ya moyo wake; haionekani. Watu wasipofuatilia ukweli, kama hawaelewi ukweli, basi maarifa yao ya kidini na nadharia ambazo wamepata zinakuwa nini? Je, zinakuwa maneno ya mafundisho ambayo watu huzungumzia mara nyingi? Watu hutumia haya yanayodaiwa kuwa mafundisho sahihi kujifanya na kujionyesha kuwa wazuri.

10.15.2019

Kiongozi wa uongo au mchungaji wa uongo ni nini? Je, kiongozi wa uongo au mchungaji wa uwongo anaweza kutambuliwaje?



Maneno Husika ya Mungu:
Wale ambao wanaweza kufuata kazi ya sasa ya Roho Mtakatifu, na ambao wanaweza kuzifuata nyayo za Mungu, kiasi kwamba wamfuate Mungu popote Awaongozapo—hawa ni watu ambao wamebarikiwa na Mungu. Wale wasiofuata kazi ya sasa ya Roho Mtakatifu hawajaingia katika kazi ya maneno ya Mungu, na haijalishi wanafanya kazi kiasi gani, au mateso yao ni makubwa vipi, au wanakimbia hapa na pale kiasi gani, hakuna linalomaanisha chochote kwa Mungu kati ya hayo, na Yeye hatawasifu.

10.12.2019

Kwa nini makanisa yanaweza kupotoka na kuwa dini?

Maneno Husika ya Mungu:

Kwa nini inasemekana kwamba vitendo vya walio katika makanisa ya kidini vimepitwa na wakati? Ni kwa kuwa wanayoyaweka katika vitendo ni tofauti na kazi ya leo. Katika Enzi ya Neema, walichotenda kilikuwa sahihi, ila kwa kuwa enzi yenyewe imepita na kazi ya Mungu kubadilika, vitendo vyao hatua kwa hatua vimepitwa na wakati. Vimeachwa nyuma na kazi mpya na mwangaza mpya. Ikiwa imesimama juu ya msingi wake asili, kazi ya Roho Mtakatifu imepiga hatua kadhaa kwa kina.

10.11.2019

Kujihusisha katika sherehe ya kidini ni nini?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Kanisa





Maneno Husika ya Mungu:
Maisha ya kawaida ya kiroho hayakomi tukwa ombi, wimbo, maisha ya kanisa, kula na kunywa maneno ya Mungu, na matendo mengine kama haya, bali yana maana ya kuishi maisha ya kiroho yaliyo mapya na ya kusisimua. Siyo kuhusu mbinu, lakini matokeo. Watu wengi sana wanafikiri kwamba ili kuwa na maisha ya kawaida ya kiroho lazima mtu asali, aombe, ale na anywe maneno ya Mungu, au kujaribu kuelewa maneno ya Mungu. Bila kujali kama kuna matokeo yoyote, au kama kuna kuelewa kwa kweli, watu hawa hulenga tu kufanya mambo yasiyo ya dhati kwa nje, na hawalengi matokeo ni watu wanaoishi ndani ya mila za dini, na si watu wanaoishi ndani ya kanisa, na hata zaidi wao si watu wa ufalme.

10.09.2019

Ni nini maana ya “acha kila kitu nyuma na kumfuata Mungu”?

Ni nini maana ya “acha kila kitu nyuma na kumfuata Mungu”?

Maneno Husika ya Mungu:
Unaweza kuutoa moyo wako na mwili na upendo wako wote wa kweli kwa Mungu, uyaweke mbele Zake, kuwa mtiifu kabisa Kwake, na kufikiria kabisa mapenzi Yake. Si kwa ajili ya mwili, si kwa ajili ya familia, wala si kwa ajili ya matamanio yako mwenyewe, bali ni kwa ajili ya maslahi ya nyumba ya Mungu. Katika kila kitu unaweza kuchukua neno la Mungu kama kanuni, kama msingi. Hivyo, malengo yako na mtazamo wako yote yatakuwa mahali sahihi, na utakuwa mtu ambaye anapata sifa za Mungu mbele Zake.

10.05.2019

Kuna tofauti ipi kati ya mtu mwaminifu na mtu mdanganyifu?

Maneno Husika ya Mungu:

Nawathamini sana wale wasio na shaka kuhusu wengine na pia nawapenda sana wale wanaokubali ukweli kwa urahisi; kwa aina hizi mbili za wanadamu Ninaonyesha utunzaji mkubwa, kwani machoni Pangu wao ni waaminifu. Kama una udanganyifu mwingi, basi utakuwa na moyo wenye hadhari na mawazo ya shaka juu ya mambo yote na wanadamu wote. Kwa sababu hii, imani yako Kwangu inajengwa kwa msingi wa shaka. Imani kama hii ni moja ambayo kamwe Sitaitambua. Bila imani ya kweli, basi utakuwa mbali hata zaidi na upendo wa kweli. Na ikiwa unaweza kumshuku Mungu na kumkisia utakavyo, basi wewe bila shaka ni mdanganyifu zaidi kati ya wanadamu wengine.

9.28.2019

Hukumu ni nini?

Hukumu ni nini?

Maneno Husika ya Mungu:
Kazi ya hukumu ni kazi ya Mungu Mwenyewe, kwa hivyo lazima ifanywe na Mungu Mwenyewe kwa kawaida; haiwezi kufanywa na mwanadamu kwa niaba Yake. Kwa sababu hukumu ni kumshinda mwanadamu kupitia ukweli, hakuna shaka kuwa Mungu bado Anaonekana kama kiumbe aliyepata mwili kufanya kazi hii miongoni mwa wanadamu. Hiyo ni kumaanisha, wakati wa siku za mwisho, Kristo atautumia ukweli kuwafunza wanadamu duniani kote na kufanya ukweli wote ujulikane kwao. Hii ni kazi ya hukumu ya Mungu.

9.25.2019

Katika miaka ya hivi karibuni, makundi ya kidini na madhehebu mbalimbali katika ulimwengu wa kidini yamekosa matumaini zaidi na zaidi, watu wamepoteza imani yao ya asili na upendo na wamekuwa hasi zaidi na zaidi na dhaifu. Pia tunahisi kunyauka kwa roho na tunahisi kuwa hatuna chochote cha kuhubiri na kwamba sote tumepoteza kazi ya Roho Mtakatifu. Tafadhali tuambie, kwa nini ulimwengu wote wa kidini umekosa matumaini hivyo? Mungu kweli anauchukia na umetelekezwa na Mungu? Tunafaaje kuelewa laana ya Mungu ya ulimwengu wa kidini katika Kitabu cha Ufunuo?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Biblia

Katika miaka ya hivi karibuni, makundi ya kidini na madhehebu mbalimbali katika ulimwengu wa kidini yamekosa matumaini zaidi na zaidi, watu wamepoteza imani yao ya asili na upendo na wamekuwa hasi zaidi na zaidi na dhaifu. Pia tunahisi kunyauka kwa roho na tunahisi kuwa hatuna chochote cha kuhubiri na kwamba sote tumepoteza kazi ya Roho Mtakatifu. Tafadhali tuambie, kwa nini ulimwengu wote wa kidini umekosa matumaini hivyo? Mungu kweli anauchukia na umetelekezwa na Mungu? Tunafaaje kuelewa laana ya Mungu ya ulimwengu wa kidini katika Kitabu cha Ufunuo?

Jibu:
Sasa, dunia nzima ya dini inakumbwa na ukiwa ulioenea pote, isiyo na kazi ya Roho Mtakatifu, na imani na upendo wa watu wengi umepungua—hili tayari limekuwa ukweli unaokubalika. Nini hasa ni sababu ya msingi ya ukiwa katika jumuiya ya dini ni swali ambalo sisi wote lazima tulielewe kikamilifu. Kwanza, hebu tuangalie nyuma kwa muda kwa mbona hekalu liligeuka la ukiwa katika siku za baadaye za Enzi ya Sheria, na kisha tutaweza kuelewa kikamilifu sababu ya ukiwa wa dunia ya dini katika siku za mwisho. Katika siku za baadaye za Enzi ya Sheria, viongozi wa Kiyahudi hawakuzifuata amri za Mungu Waliitembea njia yao wenyewe na kumwasi Mungu; hii ndiyo sababu kuu ambayo ilisababisha ukiwa wa hekalu moja kwa moja.

9.24.2019

Ingawa wachungaji na wazee wa kanisa wanashikilia mamlaka katika ulimwengu wa kidini na wanaitembea njia ya Mafarisayo wanafiki, tunamwamini Bwana Yesu, sio wachungaji na wazee wa kanisa, kwa hiyo unawezaje kusema kwamba sisi pia tunaitembea njia ya Mafarisayo? Je, hatuwezi kuokolewa kwa kumwamini Mungu ndani ya dini?

Ingawa wachungaji na wazee wa kanisa wanashikilia mamlaka katika ulimwengu wa kidini na wanaitembea njia ya Mafarisayo wanafiki, tunamwamini Bwana Yesu, sio wachungaji na wazee wa kanisa, kwa hiyo unawezaje kusema kwamba sisi pia tunaitembea njia ya Mafarisayo? Je, hatuwezi kuokolewa kwa kumwamini Mungu ndani ya dini?

Jibu:
Kuna watu wengi katika dini ambao wanaamini na kuabudu bila kufikiria na kufuata Mafarisayo. Kwa hiyo kama njia wanayoenda ni njia ya Mafarisayo ni dhahiri mara tu unapofikiri juu yake. Unathubutu kusema kuwa unaabudu na kuwalinda Mafarisayo katika moyo wako lakini huna uhusiano na dhambi zao? Unathubutu kusema kuwa unawafuata Mafarisayo wanafiki, lakini wewe si kama wao, mtu anayepinga Mungu? Je, bado hatuwezi kung’amua swali rahisi kama hilo? Aina ya mtu unayefuata ni aina ya njia unayotembea. Ikiwa unawafuata Mafarisayo basi uko kwenye njia ya Mafarisayo. Ukitembea njia ya Mafarisayo basi wewe kiasili ni aina hiyo ya mtu kama Mafarisayo.

9.23.2019

Wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa hushikilia mamlaka katika ulimwengu wa kidini na watu wengi huwatii na kuwafuata—huu ni ukweli. Unasema kwamba wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa hawaukubali ukweli wa Mungu kuwa amekuwa mwili, kwamba hawaamini ukweli ulioonyeshwa na Mungu mwenye mwili na kwamba wanaitembea njia ya Mafarisayo, na tunakubaliana na jambo hili. Lakini kwa nini unasema kuwa wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa wote ni Mafarisayo wanafiki, kuwa wote ni wapinga Kristo waliofichuliwa na kazi ya Mungu katika siku za mwisho, na kwamba wataingia katika maangamizo mwishoni? Hatuwezi kukubali jambo hili kwa wakati huu. Tafadhali shiriki unachotegemeza dai hili, kwamba watu hawa hawawezi kuokolewa na kwamba ni lazima wote waingie katika maangamizo.

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Biblia

Wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa hushikilia mamlaka katika ulimwengu wa kidini na watu wengi huwatii na kuwafuata—huu ni ukweli. Unasema kwamba wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa hawaukubali ukweli wa Mungu kuwa amekuwa mwili, kwamba hawaamini ukweli ulioonyeshwa na Mungu mwenye mwili na kwamba wanaitembea njia ya Mafarisayo, na tunakubaliana na jambo hili. Lakini kwa nini unasema kuwa wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa wote ni Mafarisayo wanafiki, kuwa wote ni wapinga Kristo waliofichuliwa na kazi ya Mungu katika siku za mwisho, na kwamba wataingia katika maangamizo mwishoni? Hatuwezi kukubali jambo hili kwa wakati huu. Tafadhali shiriki unachotegemeza dai hili, kwamba watu hawa hawawezi kuokolewa na kwamba ni lazima wote waingie katika maangamizo.

Jibu:
Asili ya jinsi watu katika jamii ya kidini wanavyomkana Mungu zinaweza tu kufichuliwa na kuchanguliwa baada ya kuja kwa Kristo mwenye mwili. Hakuna wanadamu wapotovu wanaoweza kuutambua ukweli na asili ya jamii ya kidini ya kumkana Mungu, kwa sababu wanadamu wapotovu hawana ukweli. Wanaweza tu kudhibitiwa, kuchanganywa, na kuchezewa na wachungaji wa uwongo na pepo wapinga Kristo ili kujiunga nao katika kufanya uovu, na kuwa watumishi na washiriki wa Shetani katika kumkana Mungu. Hili ni jambo la kawaida. … Hebu tuone jinsi, wakati wa Enzi ya Neema, Bwana Yesu alivyoufichua ukweli na asili ya jinsi pepo wabaya wapinga Kristo katika jamii ya kidini walivyomuasi Mungu daima:

9.22.2019

Watu wengi katika ulimwengu wa kidini wanaamini kuwa wachungaji na wazee wa kanisa wamechaguliwa na kuwekwa na Bwana, na kwamba wote humtumikia Bwana katika makanisa ya kidini; tukiwafuata na kuwatii wachungaji na wazee wa kanisa, sisi kwa kweli tunamtii na kumfuata Bwana. Kwa mintarafu hasa ya maana ya kumtii mwanadamu na kumfuata mwanadamu, na kinachomaanishwa hasa maana na kumtii Mungu na kumfuata Mungu, watu wengi hawaelewi kipengele hiki cha ukweli, kwa hiyo tafadhali shiriki hili kwa ajili yetu.

Watu wengi katika ulimwengu wa kidini wanaamini kuwa wachungaji na wazee wa kanisa wamechaguliwa na kuwekwa na Bwana, na kwamba wote humtumikia Bwana katika makanisa ya kidini; tukiwafuata na kuwatii wachungaji na wazee wa kanisa, sisi kwa kweli tunamtii na kumfuata Bwana. Kwa mintarafu hasa ya maana ya kumtii mwanadamu na kumfuata mwanadamu, na kinachomaanishwa hasa maana na kumtii Mungu na kumfuata Mungu, watu wengi hawaelewi kipengele hiki cha ukweli, kwa hiyo tafadhali shiriki hili kwa ajili yetu.

Jibu:
Katika dini, watu wengine hufikiri wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa wote wamechaguliwa na kuwekwa na Bwana. Kwa hivyo, watu wanapaswa kuwatii. Je, mtazamo kama huu una msingi wowote katika Biblia? Je, umethibitishwa na neno la Bwana? Je, una ushuhuda wa Roho Mtakatifu na uthibitisho wa Roho Mtakatifu? Ikiwa majibu yote ni la, si basi imani ya walio wengi kuwa wachungaji na wazee wa kanisa wote wameteuliwa na kuwekwa imara na Bwana hutukia katika dhana na mawazo ya watu? Tufikirie hayo. Katika Enzi ya Sheria, Musa alichaguliwa na kuwekwa na Mungu. Je, hili lina maana kuwa viongozi wote Wayahudi wakati wa Enzi ya Sheria walikuwa wameteuliwa na kutayarishwa na Mungu? Katika Enzi ya Neema, Mitume 12 wa Bwana Yesu wote walichaguliwa na kupakwa mafuta na Bwana Yesu Mwenyewe.