2.24.2019

nyimbo za dini | Tabia Ya Mungu Ni Ya Juu na Tukufu

Tabia ya Mungu ni ya Juu na Tukufu


Furaha ya Mungu ni haki na mwangaza kuja katika dunia,
ni kuangamizwa kwa giza na uovu.
Furaha Yake ni kuleta mwangaza kwa binadamu, na uzuri katika maisha yao.
Furaha Yake ni haki; ni ishara ya vitu vyote vizuri,
na ishara ya heri njema, na ishara ya heri njema.
Ghadhabu ya Mungu ni kuwa vitu visivyo vya haki viko hapa kutesa binadamu,
kwamba giza na uovu vina nafsi yake,
na pia vitu vinavyofukuza ukweli,
na kwamba kuna vitu vinavyopinga mazuri.
Ghadhabu Yake ni ishara ya mwisho wa vitu vyote vibaya,
na hata zaidi ishara ya utakatifu Wake, ishara ya utakatifu Wake.

II

Anahuzunika kuwa binadamu, ambao Ana imani kwao, wako gizani,
kwamba kazi Yake kwa binadamu inakosa kufikia mapenzi Yake,
kwamba binadamu Wake wapendwa hawawezi wote kuishi katika mwangaza.
Anahisi huzuni kwa wale wasio na hatia kati ya binadamu,
kwa wale waaminifu ilhali vipofu kati yao,
kwa wale walio wazuri lakini bila imani.
Huzuni Yake ni ishara ya uzuri Wake,
ya rehema Yake, ya uzuri, na ukarimu.

III

Furaha Yake ni adui kushindwa, kuushinda moyo wa kweli wa mwanadamu,
nguvu za maadui Wake kutolewa, kuangamizwa,
na binadamu kuwa salama katika maisha mazuri na ya amani.
Furaha Yake iko mbali na furaha ya kawaida ya mwanadamu,
ni ladha ya kuvuna matunda zaidi ya furaha.
Furaha Yake ni ishara kuwa tangu sasa,
binadamu hatateseka tena, na ataingia katika dunia ya mwangaza.
Hisia za binadamu, kwa upande mwingine, zote zinainuka kwa ajili ya maslahi yake mwenyewe,
sio kwa ajili ya haki, mwanga, au kilicho cha kupendeza,
na sembuse kwa ajili ya neema iliyotolewa na Mbingu.
Hisia za binadamu ni za ubinafsi na ni za ulimwengu wa giza.
Hazipo kwa ajili ya utashi, sembuse kwa ajili ya mpango wa Mungu,
na hivyo mwanadamu na Mungu hawawezi kamwe kuzungumziwa kwa namna mmoja.

kutoka katika "Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili

       Sikiliza zaidi: nyimbo za kuabudu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni