11.22.2019

Ni watu wangapi wa dini watakaorudi kwa Mungu katika maafa?

Maneno Husika ya Mungu:

Ninapougeuza uso Wangu kwa ulimwengu kuzungumza, binadamu wote wanasikia sauti Yangu, na hapo kuona kazi yote ambayo Nimefanya katika ulimwengu. Wale wanaoenda kinyume na mapenzi Yangu, hivyo ni kusema, wanaonipinga kwa matendo ya mwanadamu, watapitia kuadibu Kwangu.
Nitachukua nyota nyingi mbinguni na kuzitengeneza upya, na kwa mujibu Wangu jua na mwezi vitafanywa upya—anga hazitakuwa tena jinsi zilivyokuwa hapo awali; vitu visivyohesabika duniani vitafanywa kuwa vipya. Yote yatakuwa kamili kupitia maneno Yangu. Mataifa mengi katika ulimwengu yatagawanishwa upya na kubadilishwa kuwa taifa Langu, ili kwamba mataifa yote yaliyomo duniani yatatoweka milele na kuwa taifa linaloniabudu Mimi; mataifa yote ya dunia yataangamizwa, na hayatakuwepo tena. Kati ya binadamu walio ulimwenguni, wale wote walio wa Shetani wataangamizwa; wale wote wanaomwabudu Shetani watalazwa chini na moto Wangu unaochoma—yaani, isipokuwa wale walio ndani ya mkondo, waliobaki watabadilishwa kuwa jivu. Nitakapoadibu watu wengi, wale walio katika dunia ya kidini, kwa kiasi tofauti, watarudi kwa ufalme Wangu, wakiwa wameshindwa na kazi Yangu, kwani watakuwa wameona kufika kwa Aliye Mtakatifu akiwa amebebwa juu ya wingu jeupe. Wanadamu wote watafuata aina yao, na watapokea kuadibu kunakotofautiana kulingana na kile walichofanya. Wale ambao wamesimama kinyume na Mimi wataangamia; na kwa wale ambao matendo yao duniani hayakunihusisha, kwa sababu ya vile wamejiweka huru wenyewe, wataendelea kuwa duniani chini ya uongozi wa wana Wangu na watu Wangu. Nitajionyesha kwa mataifa mengi yasiyohesabika, Nikipaza sauti Yangu kote duniani Nikitangaza kukamilika kwa kazi Yangu kuu ili wanadamu wote waone kwa macho yao.

kutoka katika “Sura ya 26” ya Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima katika Neno Laonekana katika Mwili

Madondoo ya Mahubiri na Ushirika kwa ajili ya Marejeo:

Watu wengine husema, “Mwishowe, ni watu wangapi ndani ya jamii za dini wataweza kumwamini Mwenyezi Mungu?” Soma zaidi kuhusu maneno ya Mwenyezi Mungu na utajua. Kwa sasa, lango la neema halijafungwa bado, na hatujafika wakati wa maafa makubwa. Hasa wakati wa maafa makubwa, kutakuwa na watu wengine ndani ya jamii ya dini wanaorudi kwa Mungu kwa viwango mbalimbali. Hii ndiyo sababu huwezi kuamua kwa sasa “Wale wote ndani ya dunia ya dini wasiomkubali Mwenyezi Mungu lazima waangamie.” Bado kuna muda kiasi. Katika wakati huu, unajua ni nani katika jamii za dini ambaye atamkubali Mungu na nani hatamkubali Mungu? Hili ni jambo ambalo hatuwezi kuona vizuri; ni Mungu pekee anayejua. Hata hivyo, tunapoeneza injili na kushuhudia kuhusu Mungu kwa watu wa dini, tunapata kwamba wanakataa hili. Wote wanampinga na kumshutumu Mwenyezi Mungu. Je, sote hatujaona hili? Na kwa hiyo, kueneza injili kwa watu wa dini ni vigumu sana. Hili linaamua kwamba wale walio ndani ya dunia za dini ambao hatimaye watarudi kwa Mwenyezi Mungu ni wachache sana kwa idadi. Hii ni kwa sababu wanazuiwa vikali na wachungaji, wazee na fikira za dini; wamedanganywa kwa kina na uenezaji wa habari hasi. Hawana mioyo ya kutafuta ukweli na kuchunguza njia ya kweli. Je, hili si kweli? Ukienda katika eneo la dini kueneza injili, utakutana na yafuatayo: Kwanza, utakataliwa na kukumbushwa makosa yako; pili, utaaibishwa; tatu, utashambuliwa kwa pamoja, au kukejeliwa na kushutumiwa. Hata kutakuwa na watu watakaokupiga picha bila idhini yako na kuionyesha kwa wengine wote ndani ya kanisa na kusema, “Mtu huyu amekuja kueneza injili ya Mwenyezi Mungu. Hakuna mtu anayepaswa kumpokea.” Hivi ndivyo jinsi dunia ya dini inamtendea yeyote anayekuja kueneza injili ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho. Hili linaonyesha nini? Dunia ya dini kwa muda mrefu imefanya kazi kama ngome imara ya wapinga Kristo na imekuwa sehemu ya nguvu ovu za Shetani. Hata hivyo, huwezi kusema kwamba hakuna mtu kutoka dunia ya dini anayeweza kuokolewa—kuna wale wanaoweza kuokolewa, ni kwamba tu ni wachache sana, sana kwa idadi.

kutoka katika Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha, Juzuu ya 132

Watu wengine wanauliza, “Kwa nini unasema kwamba hakutakuwa na watu wengi kutoka ndani ya dini wanaokubali kazi ya Mungu kabla ya maafa makubwa? Sidhani hilo ni jambo la hakika.” Kutoka ndani ya waumini wa Enzi ya Neema, ndani ya kanisa lolote, wengi wao wako hapo kufuatilia ukweli kwa kweli, au kula mkate Wake hadi washibe tu? Watu wengi wako hapo ili kula mkate Wake hadi washibe tu. Je, hakuna watu wengi ambao wamepagawa na pepo, wanaoongea kwa ndimi, kupokea ufunuo, kuona maono, kuponya magonjwa, kufukuza pepo, na kuonyesha miujiza? Wale ambao wamepagawa na pepo wanaunda sehemu, wale wanaokula mkate Wake hadi washibe tu wanaunda sehemu, na wengine ambao ni wapinga Kristo na waovu wanaochukia ukweli pia wanaunda sehemu. Na tena kuna watu waliokanganywa ambao hawana ufahamu hata kidogo wa ukweli. Punde tunapoondoa makundi haya ya watu, wale waliobakia ambao wanapenda ukweli watakuwa wengi? Je, hata watajumuisha asilimia kumi kwa jumla? La, haiwezekani! Je, hii si hali halisi ya mambo? Kwa hiyo, wale walio ndani ya jamii ya dini ambao wataweza kurudi mbele za Mungu kabla ya maafa makubwa ni idadi ndogo sana ya watu; hawatajumuisha walio wengi hata kidogo, kwa sababu watu walio ndani ya dini wanaopenda ukweli daima wamekuwa wachache sana kwa idadi. Huu ni ukweli kamili, na hausemwi bila msingi.

kutoka katika Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha, Juzuu ya 133

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni