12.29.2019

Watu Wote wa Mungu Wamsifu Kikamilifu

 

Latest Swahili Praise and Worship Song | "Watu Wote wa Mungu Wamsifu Kikamilifu" | Tenzi ya Rohoni


Tumenyakuliwa mbele ya Mungu.
Tunajiunga na karamu ya wingi, tuna furaha sana.
Tunafurahia maneno ya Mungu na tunaelewa ukweli,
roho zetu zimeokolewa na tunahisi huru.
Mioyo yetu imejaa shukrani na sifa.
Hatuna budi ila kuimba.
Furaha iliyo mioyoni mwetu haiwezi kuelezeka.
Sifu na uruke kwa furaha.
Mungu anastahili heshima na utukufu.
Mapenzi ya Mungu yanafanyika hapa duniani.
Watu wote wa Mungu wamsifu kikamilifu.


Tunafurahia maneno ya Mungu kila siku.
Tunayatenda maneno ya Mungu, tunaingia katika uhalisi.
Tunapitia hukumu na utakaso,
na tunaishi kwa kudhihirisha mfano wa binadamu wapya.
Mwenyezi Mungu ametuokoa kutoka katika upotoshaji wa Shetani.
Sasa tumebadilika kweli.
Utukufu wote uwe kwa Mwenyezi Mungu!
Sifu na uruke kwa furaha.
Mungu anastahili heshima na utukufu.
Mapenzi ya Mungu yanafanyika hapa duniani.
Watu wote wa Mungu wamsifu kikamilifu.

Mwenyezi Mungu amemshinda Shetani,
kufanya kikundi cha watu kuwa washindi,
wakikamilishwa kwa majaribu na dhiki.
Wao ndio washindi mbele ya Shetani!
Tabia ya Mungu yenye haki imefichuliwa.
Wote wanaompinga Mungu wataangamia.
Mwenyezi Mungu amemshinda Shetani!

Sifu na uruke kwa furaha.
Mungu anastahili heshima na utukufu.
Mapenzi ya Mungu yanafanyika hapa duniani.
Watu wote wa Mungu wamsifu kikamilifu.

Wale wanaofuatilia ukweli wanapata wokovu wa Mungu.
Wale walio na imani ya kweli kwa Mungu wanapokea neema Yake.
Tabia ya Mungu yenye haki tunaisifu!
Hadi mbinguni zafika nyimbo zetu za sifa!
Kazi ya Mwenyezi Mungu ni ya kimiujiza kweli.
Maneno ya Mungu yatimiza yote.
Watu wote wanamrudia Mungu,
wakiisifu kazi kubwa ya Mungu ambayo imekamilika!
Sifu na uruke kwa furaha.
Mungu anastahili heshima na utukufu.
Mapenzi ya Mungu yanafanyika hapa duniani.
Watu wote wa Mungu wamsifu kikamilifu.

Umetoholewa kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni