9.04.2019

Unashuhudia kuwa katika siku za mwisho Mungu huonyesha ukweli na kufanya kazi ya kumhukumu na kumtakasa mwanadamu, hivyo ni kwa jinsi gani hasa Mungu humhukumu, kumtakasa na kumwokoa mwanadamu?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,hukumu

Unashuhudia kuwa katika siku za mwisho Mungu huonyesha ukweli na kufanya kazi ya kumhukumu na kumtakasa mwanadamu, hivyo ni kwa jinsi gani hasa Mungu humhukumu, kumtakasa na kumwokoa mwanadamu?

Jibu:
Kila mtu ambaye sasa anatafuta na kuchunguza njia ya kweli anataka kuelewa jinsi Mwenyezi Mungu anavyofanya kazi Yake ya hukumu ya siku za mwisho. Mwenyezi Mungu ameonyesha maneno mengi kuhusu suala hili la ukweli. Hebu tusome vifungu vichache vya neno la Mwenyezi Mungu.
Mwenyezi Mungu anasema, “Mungu Anapopata mwili mara hii, kazi Yake ni kuonyesha tabia Yake, kimsingi kupitia kuadibu na hukumu. Akitumia haya kama msingi, Analeta ukweli zaidi kwa mwanadamu, kuonyesha njia zaidi za matendo, na hivyo Hufikia lengo Lake la kumshinda mwanadamu na kumwokoa mwanadamu kutokana na tabia yake potovu. Hili ndilo liko katika kazi ya Mungu katika Enzi ya Ufalme” (Dibaji ya Neno Laonekana katika Mwili).

9.03.2019

Unasema kwamba watu wanaomwamini Mungu wanapaswa kuikubali kazi ya hukumu ya Mungu katika siku za mwisho, na ni hapo tu ndipo wanapoweza kutakasiwa tabia yao potovu na wao wenyewe kuokolewa na Mungu. Lakini sisi, kwa mujibu wa mahitaji ya Bwana, hutenda unyenyekevu na uvumilivu, kuwapenda adui zetu, kuibeba misalaba yetu, kuviacha vitu vya dunia, na sisi hufanya kazi na kuhubiri kwa ajili ya Bwana na kadhalika. Hivyo si haya yote ni mabadiliko yetu? Daima tumetafuta kwa njia hii, kwa hiyo hatuwezi kupata utakaso, unyakuo na kuingia katika ufalme wa mbinguni?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Biblia

Unasema kwamba watu wanaomwamini Mungu wanapaswa kuikubali kazi ya hukumu ya Mungu katika siku za mwisho, na ni hapo tu ndipo wanapoweza kutakasiwa tabia yao potovu na wao wenyewe kuokolewa na Mungu. Lakini sisi, kwa mujibu wa mahitaji ya Bwana, hutenda unyenyekevu na uvumilivu, kuwapenda adui zetu, kuibeba misalaba yetu, kuviacha vitu vya dunia, na sisi hufanya kazi na kuhubiri kwa ajili ya Bwana na kadhalika. Hivyo si haya yote ni mabadiliko yetu? Daima tumetafuta kwa njia hii, kwa hiyo hatuwezi kupata utakaso, unyakuo na kuingia katika ufalme wa mbinguni?

Jibu:
Tunaweza kuwapenda adui zetu, kubeba msalaba, kushinda mwili wetu, na kueneza injili ya Bwana. Hizi ni tabia chanya zinazotokana na imani yetu kwa Bwana, na kuweza kutenda kwa njia hii kunaashiria kuwa imani yetu kwa Bwana ni ya kweli. Tabia hizi nzuri zinaweza kuonekana kuwa sahihi kwa wengine na kana kwamba ziko sambamba na neno la Mungu, lakini haimaanishi kwamba tunayaweka maneno ya Mungu katika vitendo na kufuata mapenzi ya Baba wa mbinguni, wala haimaanishi kwamba tumeacha asili yetu ya dhambi na kutakaswa. Tunapokuwa tunaangalia tabia nzuri za wengine hatuwezi tu kuangalia kuonekana kwao kwa nje; lazima pia tuangalie nia zao na madhumuni ya hatimaye.

9.02.2019

Sisi hufuata mfano wa Paulo na hufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya Bwana, tukieneza injili na kumshuhudia Bwana, na tukiyalisha makanisa ya Bwana, kama vile Paulo tu: “Nimepigana vita vizuri, nimeutimiza mwendo wangu, nimeihifadhi imani” (2 Timotheo 4:7). Si huku ni kufuata mapenzi ya Mungu? Kutenda kwa njia hii kunamaanisha kuwa tunastahili kunyakuliwa na kuingia katika ufalme wa mbinguni, hivyo kwa nini tunapaswa kuikubali kazi ya Mungu ya hukumu na utakaso katika siku za mwisho kabla tuweze kuletwa katika ufalme wa mbinguni?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Kanisa

Sisi hufuata mfano wa Paulo na hufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya Bwana, tukieneza injili na kumshuhudia Bwana, na tukiyalisha makanisa ya Bwana, kama vile Paulo tu: “Nimepigana vita vizuri, nimeutimiza mwendo wangu, nimeihifadhi imani” (2 Timotheo 4:7). Si huku ni kufuata mapenzi ya Mungu? Kutenda kwa njia hii kunamaanisha kuwa tunastahili kunyakuliwa na kuingia katika ufalme wa mbinguni, hivyo kwa nini tunapaswa kuikubali kazi ya Mungu ya hukumu na utakaso katika siku za mwisho kabla tuweze kuletwa katika ufalme wa mbinguni?

Jibu:
Swali ni la muhimu sana. Inahusisha ikiwa mtu anaweza kuletwa kwenye ufalme wa mbinguni kwa kuamini katika Bwana. Waumini wengi wa Bwana wanahisi kwamba kufuata mfano wa Paulo kwa kutumia na kutumia rasilmali na kufanya kazi kwa ajili ya Bwana ni sawa na kufuata njia ya Bwana na kustahili kuingia kwenye ufalme wa mbinguni wakati Bwana atakaporudi. Hii imekuwa dhana ya watu wengi. Je, dhana hii ina msingi katika neno la Bwana? Je, inafurahisha moyo wa Bwana tukifuatilia kwa njia hii? Je, kwa kweli tunafuatilia njia ya Bwana kwa kumtumikia Bwana kama Paulo? Je, tutakuwa na sifa zinazostahili ufalme wa mbinguni? Bwana Yesu alisema, “Siye kila mmoja ambaye aliniambia, Bwana, Bwana, ataingia ufalme wa mbinguni, ila yeye atendaye mapenzi ya Baba yangu ambaye yuko mbinguni.

9.01.2019

Bibilia inasema: “Kwani mwanadamu husadiki moyoni ili kupata haki; na kwa mdomo hukubali hadi apate wokovu” (Warumi 10:10). Tunaamini kwamba Bwana Yesu alitusamehe dhambi zetu na kutufanya kuwa wenye haki kupitia imani. Aidha, tunaamini kwamba mtu akiokolewa mara moja, basi ameokolewa milele, na Bwana atakaporudi tutanyakuliwa na tutaingia katika katika ufalme wa mbinguni. Hivyo kwa nini unashuhudia kuwa tunapaswa kukubali kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho kabla ya kuweza kuokolewa na kuletwa katika ufalme wa mbinguni?

Bibilia inasema: “Kwani mwanadamu husadiki moyoni ili kupata haki; na kwa mdomo hukubali hadi apate wokovu” (Warumi 10:10). Tunaamini kwamba Bwana Yesu alitusamehe dhambi zetu na kutufanya kuwa wenye haki kupitia imani. Aidha, tunaamini kwamba mtu akiokolewa mara moja, basi ameokolewa milele, na Bwana atakaporudi tutanyakuliwa na tutaingia katika katika ufalme wa mbinguni. Hivyo kwa nini unashuhudia kuwa tunapaswa kukubali kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho kabla ya kuweza kuokolewa na kuletwa katika ufalme wa mbinguni?

Jibu:
Waumini wote katika Bwana hufikiria: Bwana Yesu alitukomboa Alipokufa msalabani, hivyo tayari tumeondolewa dhambi zote. Bwana hatuoni tena kama wenye dhambi. Tumekuwa wenye haki kupitia kwa imani yetu. Mradi tuvumilie hadi mwisho, tutaokolewa. Bwana atakaporudi tutanyakuliwa moja kwa moja kuingia katika ufalme wa mbinguni. Naam, huo ndio ukweli? Je, Mungu aliwahi kamwe kutoa ushahidi katika maneno Yake wa kuunga mkono madai haya? Kama mtazamo huu hauambatani na ukweli, matokeo yatakuwa ni yapi? Sisi ambao tunamwamini Bwana tunapaswa kutumia maneno Yake mwenyewe kama msingi wa mambo yote.

8.31.2019

Watu wengi katika ulimwengu wa kidini wanaamini kuwa Bwana Yesu kusema “Imekwisha” (Yohana 19:30) msalabani ni ushahidi kwamba kazi ya Mungu ya wokovu tayari imekamilika kabisa. Na bado unashuhudia kwamba Bwana amerejea katika mwili kuonyesha ukweli na kufanya kazi ya hukumu akianza na nyumba ya Mungu ili kuwaokoa wanadamu kabisa. Kwa hiyo ni kwa njia gani hasa mtu anafaa kuelewa kazi ya Mungu ya kuwaokoa wanadamu? Hatuko dhahiri juu ya kipengele hiki cha ukweli, kwa hiyo tafadhali shiriki hili kwa ajili yetu.

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Biblia

Watu wengi katika ulimwengu wa kidini wanaamini kuwa Bwana Yesu kusema “Imekwisha” (Yohana 19:30) msalabani ni ushahidi kwamba kazi ya Mungu ya wokovu tayari imekamilika kabisa. Na bado unashuhudia kwamba Bwana amerejea katika mwili kuonyesha ukweli na kufanya kazi ya hukumu akianza na nyumba ya Mungu ili kuwaokoa wanadamu kabisa. Kwa hiyo ni kwa njia gani hasa mtu anafaa kuelewa kazi ya Mungu ya kuwaokoa wanadamu? Hatuko dhahiri juu ya kipengele hiki cha ukweli, kwa hiyo tafadhali shiriki hili kwa ajili yetu.

Jibu:
Wakati Bwana Yesu alisema msalabani “Imekwisha” (Yohana 19:30), Alikuwa anazungumzia hasa kuhusu nini? Je, Alimaanisha kwamba kazi ya ukombozi ilikuwa imekwisha, au alikuwa Akimaanisha kwamba kazi ya Mungu ya kumwokoa mwanadamu kikamilifu ilikuwa imekwisha? Je, watu wa wakati ule hakika wangejua? Inaweza kusemwa kwamba hakuna aliyejua. Kile Bwana Yesu alichosema yalikuwa ni maneno: “Imekwisha.” Hakusema kwamba kazi ya Mungu ya kumwokoa mwanadamu ilikuwa imekwisha.

8.30.2019

Ulishuhudia kuwa Bwana amerejea na hufanya kazi Yake ya hukumu akianza kwa nyumba ya Mungu katika siku za mwisho. Hili linaonekana kuwa tofauti na hukumu ya kiti cha enzi kikubwa cheupe katika Kitabu cha Ufunuo. Kile watu wengi katika dini wanachofikiria ni kwamba hukumu ya kiti cha enzi kikubwa cheupe imelenga wasioamini walio wa pepo Shetani. Bwana atakapokuja, waumini watachukuliwa kwenda mbinguni, na kisha Atatuma maafa kuwaangamiza wasioamini. Hiyo ndiyo hukumu mbele ya kiti cha enzi kikubwa cheupe. Unashuhudia mwanzo wa hukumu ya Mungu katika siku za mwisho, lakini hatujaona Mungu akileta maafa kuwaangamiza wasioamini. Basi inawezaje kuwa hukumu ya kiti cha enzi kikubwa cheupe?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,hukumu

Ulishuhudia kuwa Bwana amerejea na hufanya kazi Yake ya hukumu akianza kwa nyumba ya Mungu katika siku za mwisho. Hili linaonekana kuwa tofauti na hukumu ya kiti cha enzi kikubwa cheupe katika Kitabu cha Ufunuo. Kile watu wengi katika dini wanachofikiria ni kwamba hukumu ya kiti cha enzi kikubwa cheupe imelenga wasioamini walio wa pepo Shetani. Bwana atakapokuja, waumini watachukuliwa kwenda mbinguni, na kisha Atatuma maafa kuwaangamiza wasioamini. Hiyo ndiyo hukumu mbele ya kiti cha enzi kikubwa cheupe. Unashuhudia mwanzo wa hukumu ya Mungu katika siku za mwisho, lakini hatujaona Mungu akileta maafa kuwaangamiza wasioamini. Basi inawezaje kuwa hukumu ya kiti cha enzi kikubwa cheupe?

Jibu:
Wale wote ambao wanaelewa Biblia wanajua kuwa hukumu ya kiti kikubwa cheupe cha enzi iliyotabiriwa katika Kitabu cha Ufunuo ni maono ya hukumu ya Mungu katika siku za mwisho. Mwenyezi Mungu mwenye mwili Alikuja kuonyesha ukweli na kufanya kazi Yake katika siku za mwisho, Akianza kuwatakasa na kuwaokoa binadamu potovu. Hii inamaanisha hukumu ya kiti kikubwa cheupe cha enzi imeanza tayari. Hukumu lazima ianzie kutoka nyumba ya Mungu. Mungu kwanza Ataunda kikundi cha washindi kabla ya maafa. Kisha, Mungu ataleta chini maafa makubwa na kuanza kuyazawadia mazuri na kuadhibu maovu, hadi hii enzi ya uovu iangamizwe. Hukumu ya Mungu ya kiti kikubwa cheupe cha enzi katika siku za mwisho basi itakamilika kabisa.

8.29.2019

Wewe hushuhudia kuwa Mungu Mwenyezi huonyesha ukweli na hufanya kazi Yake ya hukumu ya siku za mwisho. Nadhani kuwa imani yetu katika Bwana Yesu na kukubali kazi ya Roho Mtakatifu inamaanisha kuwa tayari tumepitia kazi ya Mungu ya hukumu. Hapa kuna maneno ya Bwana Yesu kama ushahidi: “Nisipoenda, Mfariji hatakuja kwenu; lakini nikiondoka, nitamtuma kwenu. Na wakati atakuja, ataushutumu ulimwengu kuhusu dhambi, na kuhusu haki, na kuhusu hukumu” (Yohana 16:7-8). Tunaamini kwamba, ingawa kazi ya Bwana Yesu ilikuwa kazi ya ukombozi, baada ya kupaa mbinguni na siku ya Pentekoste, Roho Mtakatifu alishuka na kufanya kazi kwa wanadamu: “… ataushutumu ulimwengu kuhusu dhambi, na kuhusu haki, na kuhusu hukumu.” Inafaa kuwa kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho, kwa hiyo ninachopenda kukifuatilia ni, ni nini hasa tofauti kati ya kazi ya hukumu katika siku za mwisho zinazofanywa na Mwenyezi Mungu na kazi ya Bwana Yesu?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,siku za mwisho

Wewe hushuhudia kuwa Mungu Mwenyezi huonyesha ukweli na hufanya kazi Yake ya hukumu ya siku za mwisho. Nadhani kuwa imani yetu katika Bwana Yesu na kukubali kazi ya Roho Mtakatifu inamaanisha kuwa tayari tumepitia kazi ya Mungu ya hukumu. Hapa kuna maneno ya Bwana Yesu kama ushahidi: “Nisipoenda, Mfariji hatakuja kwenu; lakini nikiondoka, nitamtuma kwenu. Na wakati atakuja, ataushutumu ulimwengu kuhusu dhambi, na kuhusu haki, na kuhusu hukumu” (Yohana 16:7-8). Tunaamini kwamba, ingawa kazi ya Bwana Yesu ilikuwa kazi ya ukombozi, baada ya kupaa mbinguni na siku ya Pentekoste, Roho Mtakatifu alishuka na kufanya kazi kwa wanadamu: “… ataushutumu ulimwengu kuhusu dhambi, na kuhusu haki, na kuhusu hukumu.” Inafaa kuwa kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho, kwa hiyo ninachopenda kukifuatilia ni, ni nini hasa tofauti kati ya kazi ya hukumu katika siku za mwisho zinazofanywa na Mwenyezi Mungu na kazi ya Bwana Yesu?

Jibu:
Kwa kuwa mnatambua aliyofanya Bwana Yesu ilikuwa kazi ya ukombozi, na njia aliyoleta ni: “Tubuni: kwa kuwa ufalme wa mbinguni u karibu” (Mathayo 4:17), basi mlikuwa na msingi gani kuamua kwamba Roho Mtakatifu alikuja katika Pentekoste kufanya kazi ya hukumu katika siku za mwisho? Mlitumia tu msingi wa neno la Bwana Yesu ambalo lilisema, “Nisipoenda, Mfariji hatakuja kwenu; lakini nikiondoka, nitamtuma kwenu. Na wakati atakuja, ataushutumu ulimwengu kuhusu dhambi, na kuhusu haki, na kuhusu hukumu” (Yohana 16:7-8), mnathubutu kuwa na uhakika kwamba kazi iliyofanywa na Roho Mtakatifu ilikuwa kazi ya hukumu katika siku za mwisho, kuna msingi wowote kulingana na neno la Mungu? Je, Bwana Yesu alisema “Roho Mtakatifu amekuja.

8.28.2019

Imeandikwa wazi katika Biblia kwamba Bwana Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu, na wale wote wanaomwamini Bwana pia wanaamini kwamba Bwana Yesu ni Kristo na kwamba Yeye ni Mwana wa Mungu. Na bado unashuhudia kuwa Kristo mwenye mwili ni onyesho la Mungu, kwamba Yeye ni Mungu Mwenyewe. Utatuambia tafadhali kama Kristo mwenye mwili kweli ni Mwana wa Mungu, au ni Mungu Mwenyewe?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,ukweli

wanaomwamini Bwana pia wanaamini kwamba Bwana Yesu ni Kristo na kwamba Yeye ni Mwana wa Mungu. Na bado unashuhudia kuwa Kristo mwenye mwili ni onyesho la Mungu, kwamba Yeye ni Mungu Mwenyewe. Utatuambia tafadhali kama Kristo mwenye mwili kweli ni Mwana wa Mungu, au ni Mungu Mwenyewe?

Jibu:
Kristo aliyepata mwili ni Mungu Mwenyewe au Mwana wa Mungu? Hasa ni swali ambalo waumini wengi huwa na tatizo kulielewa. Wakati Bwana Yesu aliyepata mwili Alikuja kufanya kazi ya kuwakomboa wanadamu, Mungu aligeuka kuwa Mwana wa Adamu, Akionekana na kufanya kazi miongoni mwa wanadamu. Hakuifungua tu Enzi ya Neema, lakini alianzisha pia enzi mpya ambamo Mungu alikuja mwenyewe katika ulimwengu wa wanadamu kuishi na mwanadamu. Kwa ibada kuu, mwanadamu Alimwita Bwana Yesu kama Kristo, Mwana wa Mungu. Wakati huo, Roho Mtakatifu pia alishuhudia ukweli kwamba Bwana Yesu ni Mwana mpendwa wa Mungu, na Bwana Yesu alimwita Mungu wa mbinguni Baba. Kwa namna hii, fikira ya uhusiano huu wa Baba-Mwana uliundwa katika ulimwengu wa dini. Sasa hebu tufikirie kwa muda mfupi.

8.27.2019

Katika Enzi ya Neema, Mungu alipata mwili ili kutumika kama sadaka ya dhambi kwa wanadamu, akiwaokoa kutoka kwa dhambi. Katika siku za mwisho Mungu amepata mwili tena ili kuonyesha ukweli na kufanya kazi Yake ya hukumu ili kumtakasa na kumwokoa mwanadamu kabisa. Kwa nini Mungu anahitaji kuwa mwili mara mbili ili kufanya kazi ya kumwokoa wanadamu? Na kuna umuhimu gani wa Mungu kuwa mwili mara mbili?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mungu

Katika Enzi ya Neema, Mungu alipata mwili ili kutumika kama sadaka ya dhambi kwa wanadamu, akiwaokoa kutoka kwa dhambi. Katika siku za mwisho Mungu amepata mwili tena ili kuonyesha ukweli na kufanya kazi Yake ya hukumu ili kumtakasa na kumwokoa mwanadamu kabisa. Kwa nini Mungu anahitaji kuwa mwili mara mbili ili kufanya kazi ya kumwokoa wanadamu? Na kuna umuhimu gani wa Mungu kuwa mwili mara mbili?

Jibu:
Ni kwa nini lazima Mungu apate mwili mara mbili kufanya kazi ya kuwaokoa wanadamu? Tunapaswa kuelewa vizuri kwanza: Kuhusu wokovu wa wanadamu, kupata mwili kwa Mungu mara mbili kuna maana ya kina na kubwa. Kwa sababu kazi ya wokovu, haijalishi kama tunazungumza kuhusu ukombozi au hukumu na utakaso katika siku za mwisho, haiwezi kutekelezwa na mwanadamu. Inahitaji Mungu kupata mwili na kutekeleza kazi hiyo Mwenyewe. Katika Enzi ya Neema, Mungu alipata mwili kama Bwana Yesu, yaani, Roho wa Mungu alijivika mwili mtakatifu na usio na dhambi, na alipigiliwa misumari msalabani kutumika kama dhabihu ya dhambi, Akamkomboa mwanadamu kutoka kwa dhambi yake. Ndiyo. Sote tunalifahamu hili. Lakini kuhusu kurudi kwa Bwana Yesu katika siku za mwisho, kwa nini Anapata mwili kama Mwana wa Adamu kuonekana na kufanya kazi? Wengi wana wakati mgumu kulielewa hili.

8.26.2019

Mungu alimtumia Musa kufanya kazi ya Enzi ya Sheria, hivyo kwa nini Mungu hawatumii watu kufanya kazi Yake ya hukumu katika siku za mwisho, lakini badala yake Analazimika kupata mwili ili kuifanya Mwenyewe?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,upendo wa Mungu

Mungu alimtumia Musa kufanya kazi ya Enzi ya Sheria, hivyo kwa nini Mungu hawatumii watu kufanya kazi Yake ya hukumu katika siku za mwisho, lakini badala yake Analazimika kupata mwili ili kuifanya Mwenyewe?

Jibu:
Ni kwa nini lazima Mungu apate mwili ili kufanya kazi Yake ya hukumu katika siku za mwisho? ni swali ambalo wengi walio na kiu ya ukweli na wanatafuta kuonekana kwa Mungu wanalijali sana. Pia ni swali linalohusiana na kama tunaweza kunyakuliwa kwenda katika ufalme wa mbinguni. Kwa hiyo, ni muhimu sana kuelewa kipengele hiki cha ukweli. Ni kwa nini lazima Mungu ajipatie mwili ili kufanya kazi Yake ya hukumu katika siku za mwisho badala ya kumtumia mwanadamu kuifanya kazi Yake? Hili linaamuliwa na hali ya kazi ya hukumu. Kwa sababu kazi ya hukumu ni onyesho la Mungu la ukweli na onyesho la tabia Yake yenye haki ili kuwashinda, kuwatakasa, na kuwaokoa wanadamu. Hebu tusome vifungu vichache kutoka kwa neno la Mwenyezi Mungu.

8.25.2019

Bwana Yesu alikuwa Mungu mwenye mwili na hakuna yeyote anaweza kukanusha hili. Sasa unashuhudia kwamba Mwenyezi Mungu ni Bwana Yesu aliyerudi katika mwili, lakini wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa wanasema kuwa kile unachoamini ni mtu tu, wanasema kuwa umedanganywa, na hatuwezi kulielewa jambo hili. Wakati huo Bwana Yesu alipokuwa mwili na kuja kufanya kazi ya ukombozi, Mafarisayo Wayahudi pia walisema kuwa Bwana Yesu alikuwa mtu tu, wakisema kwamba mtu yeyote aliyemwamini Yeye alikuwa akidanganywa. Kwa hiyo, tungependa kufuatilia kipengele hiki cha ukweli kuhusu kupata mwili. Kupata mwili ni nini hasa? Na ni nini asili ya kupata mwili? Tafadhali shiriki hili kwa ajili yetu.

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,siku za mwisho

Bwana Yesu alikuwa Mungu mwenye mwili na hakuna yeyote anaweza kukanusha hili. Sasa unashuhudia kwamba Mwenyezi Mungu ni Bwana Yesu aliyerudi katika mwili, lakini wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa wanasema kuwa kile unachoamini ni mtu tu, wanasema kuwa umedanganywa, na hatuwezi kulielewa jambo hili. Wakati huo Bwana Yesu alipokuwa mwili na kuja kufanya kazi ya ukombozi, Mafarisayo Wayahudi pia walisema kuwa Bwana Yesu alikuwa mtu tu, wakisema kwamba mtu yeyote aliyemwamini Yeye alikuwa akidanganywa. Kwa hiyo, tungependa kufuatilia kipengele hiki cha ukweli kuhusu kupata mwili. Kupata mwili ni nini hasa? Na ni nini asili ya kupata mwili? Tafadhali shiriki hili kwa ajili yetu.

Jibu:
Imani yenu katika Bwana Yesu kama kupata mwili kwa Mungu si uwongo. Lakini mbona mnamwamini Bwana Yesu? Je, kweli mnamfikiria Bwana Yesu kuwa ni Mungu? Mnamwamini Bwana Yesu kwa sababu ya kile kilichorekodiwa katika Biblia na kwa sababu ya kazi ya Roho Mtakatifu. Lakini haijalishi mnachosema, ikiwa hamjamwona Bwana Yesu uso kwa uso, je, mwaweza kuthubutu kusema kwamba mnamjua Bwana Yesu? Katika imani yenu kwa Bwana, mnarudia tu maneno ya Petro, aliyesema kwamba Bwana Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu aishiye, lakini je, mnaamini kwamba Bwana Yesu ni dhihirisho la Mungu, ni Mungu Mwenyewe? Mnathubutu kusema kwamba mnatambua kiini kitakatifu cha Bwana Yesu? Mnathubutu kuahidi kwamba kama Bwana Yesu angekuja tena akionyesha ukweli, mngetambua sauti Yake? Imani yenu kwa Bwana Yesu si chochote ila imani katika maneno haya mawili “Bwana Yesu.”

8.24.2019

Wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa mara nyingi huwahubiria waumini kwamba mahubiri yoyote yanayosema kwamba Bwana amekuja katika mwili ni uongo. Wao hutegemeza hili aya za Biblia: “Basi iwapo mtu yeyote atawaambia, Tazameni, Kristo yuko huku, au yuko pale; msiamini hili. Kwa kuwa wataibuka Makristo wasio wa kweli, na manabii wasio wa kweli, nao wataonyesha ishara kubwa na vioja; ili kwamba, ikiwezekana, watawadanganya walio wateule zaidi” (Mathayo 24: 23-24). Sasa hatuna habari tunavyofaa kumtambua Kristo wa kweli kutoka kwa wale wa uongo, hivyo tafadhali jibu swali hili.

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Kanisa

Wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa mara nyingi huwahubiria waumini kwamba mahubiri yoyote yanayosema kwamba Bwana amekuja katika mwili ni uongo. Wao hutegemeza hili aya za Biblia: “Basi iwapo mtu yeyote atawaambia, Tazameni, Kristo yuko huku, au yuko pale; msiamini hili. Kwa kuwa wataibuka Makristo wasio wa kweli, na manabii wasio wa kweli, nao wataonyesha ishara kubwa na vioja; ili kwamba, ikiwezekana, watawadanganya walio wateule zaidi” (Mathayo 24: 23-24). Sasa hatuna habari tunavyofaa kumtambua Kristo wa kweli kutoka kwa wale wa uongo, hivyo tafadhali jibu swali hili.

Jibu:
Bwana Yesu kweli alitabiri kwamba kungekuwa na Kristo wa uongo na manabii wa uongo katika siku za mwisho. Huu ni ukweli. Lakini Bwana Yesu pia alitabiri wazi mara nyingi kwamba Atarudi. Hakika tunaamini hivyo? Wakati wa kuchunguza unabii wa Bwana Yesu kurudi, watu wengi huupa kipaumbele wasiwasi wao wa Kristo wa uongo na manabii wa uongo. na kutotilia maanani jinsi ya kukaribisha kuwasili kwa bwana harusi, na jinsi ya kusikia sauti ya bwana harusi. Suala ni lipi hapa? Je, si hili ni jambo la kula kwa hofu ya kusongwa, ya kuwa mwenye busara katika umaskini na kuwa mjinga utajirini?