XVI. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kama Mungu Kweli ni Mungu wa Utatu au ni Mungu Mmoja wa Kweli
Kumuainisha Mungu mmoja wa kweli kama “Mungu wa utatu” ni kumkana na kumkufuru Mungu
Hebu Niwaambie hilo, kwa hakika, Utatu Mtakatifu haupo popote katika dunia hii. Mungu hana Baba wala Mwana, vivyo hivyo hakuna dhana ya chombo kitumiwacho kwa pamoja na Baba na Mwana: Roho Mtakatifu. Huu wote ni uongo mkubwa zaidi na haupo kabisa katika dunia hii! Hata hivyo uongo huu una asili yake na haukosi msingi kabisa, kwani akili zenu si punguani, na mawazo yenu hayakosi mantiki. Badala yake, ziko sawa na yenye ubunifu kwa kiasi kikubwa, kwamba haziwezi kuzuiwa hata na Shetani yeyote.