12.30.2018

Watu Wanamjua Mungu Bora Kupitia Kazi ya Maneno

Umeme wa Mashariki,siku za mwisho,ukweli

Watu Wanamjua Mungu Bora Kupitia Kazi ya Maneno

I
Mungu wa siku za mwisho hasa anatumia neno kumkamilisha mwanadamu,
si ishara na miujiza ya kumdhulumu au kumshawishi,
kwa kuwa hivi haviwezi kueleza nguvu za Mungu.
Ikiwa Mungu angeonyesha tu ishara na miujiza,
haingewezekana kudhihirisha ukweli wa Mungu,
na hivyo haingewezekana kumkamilisha mwanadamu. 
Mungu hamkamilishi mwanadamu kwa ishara na miujiza,
isipokuwa anamnyunyizia maji na kumchunga na maneno,
ili kufanikisha utiifu wa mwanadamu, ujuzi wa Mungu.
Hili ndilo lengo la kazi Yake na maneno Yake.
Mungu hatumii ishara na miujiza kumkamilisha mwanadamu.
Anatumia maneno na aina nyingi za kazi badala yake,
kama vile usafishaji, ushughulikiaji, upogoaji au utoaji wa maneno.
Mungu ananena kutoka kwa mitazamo tofauti ili kumkamilisha mwanadamu,
na kumpa mwanadamu ujuzi mwingi wa kazi,
hekima na ajabu ya Mungu.
II
Kazi ya Mungu inayofanyika leo ni kazi halisi,
bila ishara au miujiza sasa,
kwani vingetapanya kazi Yake halisi,
na Hangeweza kufanya kazi yoyote zaidi.
Ingeweza kuonyesha kama imani ya mwanadamu kwa Mungu ni kweli
kama Angesema Atatumia neno kumkamilisha mwanadamu
lakini pia akamwonyesha mwanadamu ishara na miujiza?
Kwa hiyo, Mungu hafanyi mambo kama hayo.
Mungu hatumii ishara na miujiza kumkamilisha mwanadamu.
Anatumia maneno na aina nyingi za kazi badala yake,
kama vile usafishaji, ushughulikiaji, upogoaji au utoaji wa maneno.
Mungu ananena kutoka kwa mitazamo tofauti ili kumkamilisha mwanadamu,
na kumpa mwanadamu ujuzi mwingi wa kazi,
hekima na ajabu ya Mungu.
III
Kuna udini mwingi sana katika mwanadamu.
Mungu amekuja wakati wa siku za mwisho
kutoa mawazo mwanadamu ya dini, mambo yasiyo ya kweli
na kumfanya mwanadamu aujue uhalisi wa Mungu.
Amekuja kuondoa sura ya Mungu
ambaye ni wa dhahania, mbunifu na asiyekuwepo.
Kwa hiyo sasa jambo pekee la thamani kwako
ni kuwa na ujuzi ya uhalisi.
Kutafuta ukweli katika imani ya mwanadamu kwa Mungu
na kufuatilia maisha badala ya ishara na miujiza,
hili inapaswa kuwa lengo la wote wanaomwamini Mungu.
Mungu hatumii ishara na miujiza kumkamilisha mwanadamu.
Anatumia maneno na aina nyingi za kazi badala yake,
kama vile usafishaji, ushughulikiaji, upogoaji au utoaji wa maneno.
Mungu ananena kutoka kwa mitazamo tofauti ili kumkamilisha mwanadamu,
na kumpa mwanadamu ujuzi mwingi wa kazi,
hekima na ajabu ya Mungu.
kutoka katika "Yote Yanafanikishwa Kupitia kwa Neno la Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili

kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

       Tazama zaidi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni