7.20.2019

Biblia ni kumbukumbu tu ya hatua mbili za kazi za Mungu katika Enzi ya Sheria na Enzi ya Neema; siyo kumbukumbu ya ukamilifu wa kazi ya Mungu

XI. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kipengele cha Ukweli Kuhusu Uhusiano kati ya Mungu na Biblia

Biblia ni kumbukumbu tu ya hatua mbili za kazi za Mungu katika Enzi ya Sheria na Enzi ya Neema; siyo kumbukumbu ya ukamilifu wa kazi ya Mungu


Aya za Biblia za Kurejelea:
Bado ningali nayo mengi ya kuwaambieni, lakini hivi sasa hamwezi kuyavumilia. Hata hivyo, wakati yeye, Roho wa ukweli, atakapokuja, atawaongoza hadi kwenye ukweli wote: kwa maana hatazungumza juu yake mwenyewe; bali chochote atakachosikia, atakinena: na atawaonyesha mambo yajayo” (Yohana 16:12-13).

7.19.2019

Ni vipi Mungu huutawala na kuusimamia ulimwengu mzima?

X. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kipengele cha Ukweli Kuhusu Jinsi ya Kumjua Mungu

Ni vipi Mungu huutawala na kuusimamia ulimwengu mzima?


Maneno Husika ya Mungu:
Ni viumbe wangapi wanaoishi na kuzaana katika ulimwengu mpana, wakifuata sheria ya maisha tena na tena, wakifuata sheria isiyobadilika. Wanaokufa huenda na hadithi za walio hai, na walio hai hurudia historia hii yenye huzuni ya wale waliokufa. Na kwa hivyo wanadamu hawawezi kujizuia ila kujiuliza wenyewe; Kwa nini tunaishi? Na kwa nini inatulazimu kufa? Nani anayeitawala dunia hii? Na ni nani muumbaji wa mwanadamu?

7.18.2019

Ni vipi Mungu amewaongoza na kuwaruzuku wanadamu hadi leo?

X. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kipengele cha Ukweli Kuhusu Jinsi ya Kumjua Mungu

Ni vipi Mungu amewaongoza na kuwaruzuku wanadamu hadi leo?


Maneno Husika ya Mungu:
Kazi ya usimamizi wa Mungu ilianza Alipoumba ulimwengu, na mwanadamu ni kiini cha kazi Yake. Uumbaji wa Mungu wa kila kitu, unaweza kusemwa, ni kwa ajili ya mwanadamu. Kwa sababu Kazi ya usimamizi Wake imesambaa katika maelfu ya miaka, na haijatekelezwa katika dakika na sekunde tu, ama kufumba na kufumbua, ama katika mwaka mmoja au miwili, ilimbidi Aumbe vitu vingine zaidi kwa ajili ya maisha ya mwanadamu, kama vile jua, mwezi, na aina zote za viumbe walio hai, na chakula na mazingira kwa ajili ya wanadamu. Huu ndio ulikuwa mwanzo wa usimamizi wa Mungu.

7.17.2019

Ni katika vipengele vipi ambapo uweza na hekima ya Mwenyezi Mungu hufichuliwa hasa?

X. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kipengele cha Ukweli Kuhusu Jinsi ya Kumjua Mungu

Ni katika vipengele vipi ambapo uweza na hekima ya Mwenyezi Mungu hufichuliwa hasa?


Maneno Husika ya Mungu:
Matamshi ya Mungu ni mamlaka, Maneno ya Mungu ni hoja za kweli, na kabla hajatamka maneno kutoka kinywani Mwake, hivi ni kusema, wakati Anapofanya uamuzi wa kufanya kitu, tayari kitu hicho kimefanyika.
kutoka katika “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee I” katika Neno Laonekana katika Mwili

7.16.2019

Mtu anawezaje kujua asili na tabia ya Mungu?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Neno la Mungu

X. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kipengele cha Ukweli Kuhusu Jinsi ya Kumjua Mungu

Mtu anawezaje kujua asili na tabia ya Mungu?


Maneno Husika ya Mungu:
Watu mara nyingi husema kwamba si jambo rahisi kumjua Mungu. Mimi, hata hivyo, nasema kwamba kumjua Mungu si jambo gumu kamwe, kwani Mungu mara kwa mara huruhusu binadamu kushuhudia matendo Yake. Mungu hajawahi kusitisha mazungumzo Yake na mwanadamu; Yeye hajawahi kujificha kutoka kwa binadamu, wala Yeye hajajificha. Fikira Zake, mawazo Yake, maneno Yake na matendo Yake vyote vimefichuliwa kwa mwanadamu.

7.15.2019

Kumjua Mungu ni nini hasa? Kuwa kwa ufahamu wa Biblia na nadharia ya teolojia unaweza kuchukuliwa kama kumjua Mungu?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,ukweli

X. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kipengele cha Ukweli Kuhusu Jinsi ya Kumjua Mungu

Kumjua Mungu ni nini hasa? Kuwa kwa ufahamu wa Biblia na nadharia ya teolojia unaweza kuchukuliwa kama kumjua Mungu?


Maneno Husika ya Mungu:
Kumjua Mungu kunamaanisha nini? Kunamaanisha kwamba mwanadamu anajua shangwe, hasira, huzuni na furaha ya Mungu; huku ndiko kumjua Mungu. Unasema kwamba umemwona Mungu, ilhali huelewi shangwe, hasira, huzuni, na furaha ya Mungu, huelewi tabia Yake, wala huelewi haki Yake. Huna ufahamu wa rehema Zake, na hujui Anachokipenda ama Anachokichukia. Huu si ufahamu wa Mungu. Ikiwa unamjua, unamwelewa, na unaweza kuelewa mapenzi Yake kiasi, basi unaweza kumwamini kwa kweli, kumtii kwa kweli, kumpenda kwa kweli, na kumwabudu Yeye kwa kweli. Ikiwa huelewi mambo haya, basi unafuata tu, mtu fulani anayefuata tu na kufuata umati.

7.14.2019

Sura ya tatizo la mwanadamu kutokubali ukweli ulioonyeshwa na Kristo ni ipi? Matokeo ya mtu kutomchukua Kristo kama Mungu ni yapi?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,ukweli

IX. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kwamba Kristo ni Onyesho la Mungu Mwenyewe

Sura ya tatizo la mwanadamu kutokubali ukweli ulioonyeshwa na Kristo ni ipi? Matokeo ya mtu kutomchukua Kristo kama Mungu ni yapi?

Aya za Biblia za Kurejelea:
“Yesu akawaambia, … Ninyi ni wa baba yenu ibilisi, na mtatimiliza tamaa za baba yenu. Alikuwa mwuaji tangu mwanzo, na hakudumu katika ukweli, kwa sababu ukweli haupo ndani yake. Anaponena uwongo, anazungumza yaliyo yake mwenyewe: kwani yeye ni mwongo, na baba wa uwongo. Na kwa kuwa nawaambieni ukweli, hamniamini. … Yule ambaye ni wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu: nyinyi kwa hivyo hamyasikii, kwa kuwa nyinyi si wa Mungu” (Yohana 8:42-45, 47).

7.13.2019

Kristo ni Mwana wa Mungu au ni Mungu Mwenyewe?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Biblia

IX. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kwamba Kristo ni Onyesho la Mungu Mwenyewe

Kristo ni Mwana wa Mungu au ni Mungu Mwenyewe?

Aya za Biblia za Kurejelea:
“Filipo akamwambia, Bwana, tuonyeshe Baba, na hiyo itatutosha. Yesu akasema kwake, nimekuwa nanyi kwa muda mrefu, na bado hujanijua, Filipo? Yeye ambaye ameniona amemwona Baba; na unasemaje basi, Tuonyeshe Baba? Huamini kwamba mimi niko ndani ya Baba, na Baba yuko ndani ya mimi? Maneno ninenayo kwenu sineni juu yangu, ila Baba aishiye ndani yangu, anazifanya kazi hizo. Niamini kwamba niko ndani ya Baba, na Baba yuko ndani ya mimi, la sivyo niamini kwa ajili ya kazi hizo” (Yohana 14:8-11).

7.12.2019

Mtu anawezaje kujua asili ya utukufu wa Kristo?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Biblia

IX. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kwamba Kristo ni Onyesho la Mungu Mwenyewe

Mtu anawezaje kujua asili ya utukufu wa Kristo?

Aya za Biblia za Kurejelea:
“Yesu akanena kwake, Mimi ndiye njia, ukweli na uhai….” “Maneno ninenayo kwenu sineni juu yangu, ila Baba aishiye ndani yangu, anazifanya kazi hizo. Niamini kwamba niko ndani ya Baba, na Baba yuko ndani ya mimi, la sivyo niamini kwa ajili ya kazi hizo” (Yohana 14:6, 10-11).
Maneno Husika ya Mungu:

7.11.2019

Mtu anayemwamini Mungu ni lazima aweze kutambua wachungaji wa uwongo na wapinga Kristo kuiacha dini na kurudi kwa Mungu

VIII. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kipengele cha Ukweli Kuhusu Tofauti Kati ya Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu

Mtu anayemwamini Mungu ni lazima aweze kutambua wachungaji wa uwongo na wapinga Kristo kuiacha dini na kurudi kwa Mungu

Aya za Biblia za Kurejelea:
“Bwana Yehova alisema hivi kwa wachungaji; Ole wao wachungaji wa Israeli wajilishao! Wachungaji hawapaswi kuwalisha kondoo? Mnawala kondoo walio wanono, na kuvalia sufu zao, mnawaua wale ambao wamenona: lakini hamwalishi kondoo. Hamjawapa nguvu wagonjwa, wala hamjawaponya waliougua, wala hamjawafunga waliovunjika, wala hamjawarudisha wale waliofukuzwa, wala hamjawatafuta wale waliopotea; lakini mmewatawala kwa nguvu na ukatili” (Ezekieli 34:2-4).

7.10.2019

Mtu lazima atambue tofauti kati ya Kristo mwenye mwili na Makristo wa uongo na manabii wa uongo

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli

VIII. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kipengele cha Ukweli Kuhusu Tofauti Kati ya Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu

Mtu lazima atambue tofauti kati ya Kristo mwenye mwili na Makristo wa uongo na manabii wa uongo

Aya za Biblia za Kurejelea:
Mimi ndiye njia, ukweli na uhai” (Yohana 14:6).
Huamini kwamba mimi niko ndani ya Baba, na Baba yuko ndani ya mimi? Maneno ninenayo kwenu sineni juu yangu, ila Baba aishiye ndani yangu, anazifanya kazi hizo” (Yohana 14:10).
Mimi na yeye Baba yangu tu mmoja” (Yohana 10:30).
Kwa kuwa wataibuka makristo wasio wa kweli, na manabii wasio wa kweli, nao wataonyesha ishara kubwa na vioja; ili kwamba, ikiwezekana, watawadanganya walio wateule zaidi” (Mathayo 24:24).

7.09.2019

Kuna tofauti ipi kati ya kazi ya wale wanaotumiwa na Mungu na kazi ya viongozi wa kidini?

VIII. Ni Lazima Mtu Ashiriki kwa Dhahiri Kipengele cha Ukweli Kuhusu Tofauti Kati ya Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu

Kuna tofauti ipi kati ya kazi ya wale wanaotumiwa na Mungu na kazi ya viongozi wa kidini?

Aya za Biblia za Kurejelea:
“Naye akasema … Mtumishi wangu Musa hayuko hivyo, ambaye ni mwaminifu nyumbani mwangu mwote” (Hesabu 12:6-7).
“Na Yesu akajibu na kumwambia, … Na pia nakuambia, Kwamba wewe ni Petro, na nitalijenga kanisa langu juu ya mwamba huu; na milango ya jahanamu haitashinda dhidi ya kanisa hilo. Na nitakupa funguo za ufalme wa mbinguni: na chochote utakachofunga duniani kitafungwa mbinguni: na chochote utakachoweka huru duniani kitawekwa huru mbinguni” (Mathayo 16:17-19).