Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo wokovu,ukweli. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo wokovu,ukweli. Onyesha machapisho yote

6.19.2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Tamko la Thelathini na Saba

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Tamko la Thelathini na Saba


Kotekote katika enzi, kazi yote Niliyoifanya—kila hatua ya kazi hiyo—imekuwa na mbinu Zangu zinazofaa za kazi. Ni kwa sababu ya hili ndio watu Wangu wapendwa wamekuwa watakatifu zaidi na zaidi, na wa kufaa zaidi na zaidi kwa matumizi Yangu. Kwa sababu hiyo hiyo, hata hivyo, jambo la kusikitisha ni kwamba kadri mbinu Zangu za kazi zinavyoongezeka, idadi ya watu inapungua, ambalo husababisha watu kuzama katika kutafakari. Bila shaka, Kazi Yangu leo sio tofauti na watu wengi wamejikuta tena katika kutafakari, kwa hiyo kwa sababu ya mabadiliko ya mbinu Zangu, kuna sehemu ya watu ambao watajiondoa.