Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Yesu-Kristo. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Yesu-Kristo. Onyesha machapisho yote

1.17.2018

3. Asili na Maendeleo ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

3. Asili na Maendeleo ya Kanisa la Mwenyezi Mungu
Katika Enzi ya Neema, Bwana Yesu aliwaahidi wafuasi wake, “Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi muwepo.” (Yohana 14:3) Kadhalika Alitabiri, “Kwa maana kama umeme utokavyo mashariki, na kumulika hata magharibi; hivyo ndivyo ujio wake Mwana wa Adamu utakavyokuwa.” (Mathayo 24:27) Katika siku za mwisho, kama ilivyoahidiwa na kutabiriwa na Yeye, Mungu tena Amekuwa mwili na kushukia Mashariki ya dunia—China—kufanya kazi ya kuhukumu, kuadibu, ushindi, na wokovu Akitumia neno, kwa msingi wa kazi ya ukombozi ya Bwana Yesu.