Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Neno-Lonekana-katika-Mwili. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Neno-Lonekana-katika-Mwili. Onyesha machapisho yote

3.20.2019

Matamshi ya Mungu | Sura ya 22 na 23

Leo, wote wako tayari kuelewa mapenzi ya Mungu na kujua tabia ya Mungu, lakini hakuna anayejua kwa nini hawezi kufuata matamanio yake, hajui kwa nini moyo wake daima humsaliti, na kwa nini hawezi kutimiza kile anachotaka. Kwa hiyo, yeye anakabiliwa tena na hali mbaya ya kukata tamaa, lakini pia anaogopa. Asiweze kuonyesha hisia hizi zinazopingana, anaweza tu kuonyesha huzuni na kuendelea kujiuliza: Je, inaweza kuwa Mungu hajanipa nuru? Inaweza kuwa Mungu ameniacha kwa siri? Pengine wengine wote wako sawa, na Mungu amewapa wote nuru isipokuwa mimi.