11.28.2019

Mabadiliko ya tabia hudhihirishwaje?

Maneno Husika ya Mungu:

Ikiwa tabia yako inaweza kubadilika au la inategemea na ikiwa unaweza kuendelea na maneno halisi ya Roho Mtakatifu au la na una ufahamu wa kweli. Hili ni tofauti na kile mlichoelewa awali. Kile ulichoelewa kuhusu mabadiliko katika tabia awali kilikuwa kwamba wewe, ambaye ni rahisi kuhukumu, kupitia kwa kufundishwa nidhamu na Mungu huzungumzi ovyo ovyo tena. Lakini hii ni hali moja tu ya mabadiliko, na hivi sasa suala muhimu zaidi ni kufuata uongozi wa Roho Mtakatifu.
Unafuata chochote asemacho Mungu; unatii chochote asemacho Yeye. Watu hawawezi kubadilisha tabia yao wenyewe; lazima wapitie hukumu na kuadibu, mateso na usafishaji wa maneno ya Mungu, au kushughulikiwa, kufunzwa nidhamu, na kupogolewa na maneno Yake. Ni baada ya hapo tu ndipo wanaweza kutimiza utiifu na ibada kwa Mungu, na sio kujaribu kumdanganya Yeye na kumshughulikia kwa uzembe. Ni kupitia kwa usafishaji wa maneno ya Mungu ndio watu hupata mabadiliko katika tabia. Ni wale tu wanaopitia mfichuo, hukumu, kufundishwa nidhamu, na kushughulikiwa kwa maneno Yake ambao hawatathubutu tena kufanya mambo kwa kutojali, na watakuwa watulivu na makini. Jambo muhimu sana ni kwamba wanaweza kutii neno la sasa la Mungu na kutii kazi ya Mungu, na hata kama hayalingani na fikira za binadamu, wanaweza kuweka kando fikira hizi na kutii kwa hiari. Mabadiliko katika tabia yalipozungumziwa hapo awali, imekuwa hasa kuhusu kujinyima mwenyewe, kuruhusu mwili kuteseka, kufunza nidhamu mwili wa mtu, na kujiondolea mapendeleo ya mwili—hii ni aina moja ya mabadiliko katika tabia. Watu sasa wanajua kwamba maonyesho halisi ya mabadiliko katika tabia ni kutii maneno halisi ya Mungu na vilevile kuweza kuwa na ufahamu halisi wa kazi Yake mpya. Kwa njia hii watu wataweza kuondoa ufahamu wao wa awali wa Mungu, ambao ulipotoshwa na fikira zao wenyewe, na kutimiza ufahamu wa kweli wa na utiifu Kwake. Hii tu ndio maonyesho halisi ya mabadiliko katika tabia.

kutoka katika “Wale Ambao Tabia Yao Imebadilika ni Wale Ambao Wameingia Katika Uhalisi wa Neno la Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Watu wanaweza kuwa na tabia nzuri, lakini hiyo haimaanishi kuwa wako na ukweli. Bidii ya watu inaweza tu kuwafanya wazingatie mafundisho na kufuata kanuni; watu wasio na ukweli hawana namna ya kutatua shida halisi, na mafundisho hayawezi kushikilia nafasi ya ukweli. Wale ambao wamepitia mabadiliko katika tabia zao ni tofauti. Wana ukweli ndani yao, wanatambua masuala yote, wanajua jinsi ya kutenda kulingana na mapenzi ya Mungu, jinsi ya kutenda kulingana na kanuni za ukweli, jinsi ya kutenda ili kumridhisha Mungu, nao wanaelewa asili ya upotovu wanaoufichua. Mawazo na dhana zao wenyewe vinapofichuliwa, wanaweza kutambua na kuunyima mwili. Hivi ndivyo mabadiliko katika tabia yanavyoonyeshwa. Kitu cha muhimu kuhusu mabadiliko katika tabia ni kwamba yana ukweli na uwazi, na unapotekeleza mambo, yanauweka ukweli katika matendo kwa usahihi wa karibu na upotovu wao hauonekani mara nyingi. Kwa jumla, mtu ambaye tabia yake imebadilika huonekana kuwa na busara na mwenye utambuzi, na kutokana na kuelewa kwake kwa ukweli, kujidai na kiburi havifichuliwi sana. Anaweza kuona kila kitu kwa uwazi, basi hawi mwenye kiburi baada ya kupata uwazi huu. Anaweza kuwa na ufahamu wa taratibu kuhusu ni ipi nafasi ya mwanadamu, jinsi ya kutenda kwa busara, jinsi ya kuwa mtiifu, nini anachofaa kusema na nini asichofaa kusema, na nini cha kusema na nini cha kutenda kwa watu gani. Hii ndiyo sababu inasemwa kuwa watu wa aina hii ni wenye busara kiasi. Wale ambao wana mabadiliko katika tabia zao wanaishi kwa kudhihirisha sura ya binadamu kwa kweli, nao wana0 ukweli; hawategemei ushawishi wa wengine. Wale ambao wamekuwa na mabadiliko katika tabia wako imara zaidi, hawasitisiti, na haijalishi wako katika hali gani, wanajua jinsi ya kutimiza wajibu wao sawasawa na jinsi ya kufanya mambo ili kumridhisha Mungu. Wale ambao tabia zao zimebadilika hawalengi nini cha kufanya ili kujifanya waonekane wazuri katika kiwango cha juujuu—wanao uwazi wa ndani kuhusu kile cha kufanya ili kumridhisha Mungu. Kwa hivyo, kutoka nje wanaweza kukosa kuonekana wenye shauku sana ama kama wamefanya jambo lolote kubwa, lakini kila kitu wanachofanya kina maana, kina thamani, na kina matokeo ya kiutendaji. Wale ambao tabia zao zimebadilika wana uhakika kuwa na ukweli mwingi—hii inaweza kuthibitishawa kwa mitazamo yao kuhusu mambo na kanuni zao katika vitendo vyao. Wale wasio na ukweli hawajakuwa na mabadiliko katika tabia hata kidogo. Hiyo si kusema kwamba mtu aliyekomaa katika ubinadamu wake lazima atakuwa na mabadiliko katika tabia; labda hufanyika wakati baadhi ya sumu za kishetani katika asili ya mtu zinabadilika kwa sababu ya maarifa yao kuhusu Mungu na ufahamu wao wa ukweli. Hiyo ni kusema, sumu hizo zinatakaswa na ukweli unaoonyeshwa na Mungu unaanza kustawi ndani ya mtu huyo, unakuwa maisha yake, nao unakuwa msingi wa kuwepo kwake. Hapo tu ndipo anakuwa mtu mpya, na hivyo tabia yake inabadilika. Hivi si kusema kwamba tabia yake ya nje ni ya upole kuliko hapo awali, kuwa alikuwa na kiburi lakini sasa maneno yake ni ya busara, kwamba hakuwa anamsikiza mtu yeyote lakini sasa anaweza kuwasikiza wengine—mabadiliko haya ya nje hayawezi kusemwa kuwa ni mabadiliko katika tabia. Bila shaka mabadiliko katika tabia yanajumuisha hali hizi, lakini jambo lililo muhimu zaidi ni kuwa maisha yake ya ndani yamebadilika. Ukweli unaoonyeshwa na Mungu unakuwa maisha yake hasa, baadhi ya sumu za kishetani zilizo ndani zimetolewa, mtazamo wa mtu huyo umebadilika kabisa, na hakuna chochote kati ya hali hizo kinachokubaliana yale ya dunia. Anaona waziwazi njama na sumu za joka kubwa jekundu; amefahamu kiini cha kweli cha maisha. Kwa hivyo maadili ya maisha yake yamebadilika—hili ndilo badiliko la muhimu zaidi na kiini cha mabadiliko katika tabia.

kutoka katika “Tofauti Kati ya Mabadiliko ya Nje na Mabadiliko katika Tabia” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Kuna sifa bainifu ya mabadiliko katika tabia: Ni kuweza kukubali ukweli na kutii mambo yaliyo sahihi na yanayolingana na ukweli. Haijalishi ni nani anayekupa mapendekezo—wawe ni vijana au wazee, iwe mnashirikiana vizuri, iwe kuna visasi kati yenu, alimradi anasema kitu kilicho sahihi, kinacholingana na ukweli, na chenye manufaa kwa kazi ya nyumba ya Mungu, unaweza kukichukua na kukikubali. Huathiriwi na mambo mengine yoyote. Hiki ni kipengele kimoja cha udhihirisho huo. Kipengele kingine ni kwamba unapokumbana na suala unaweza kutafuta ukweli. Kwa mfano, unakumbana na jambo usilolifahamu ambalo hakuna mtu anayelielewa kikamilifu. Wewe unaweza kutafuta ukweli, kuona ni kitendo cha aina gani kinacholingana na kanuni za ukweli, na kinatosheleza mahitaji ya Mungu. Ilhali kipengele kingine ni uwezo wa kufikiria mapenzi ya Mungu. Jinsi unaweza kufikiria mapenzi Yake inategemea ni wajibu upi unatimiza na ni mahitaji yapi ambayo Mungu anayo kwako katika wajibu huu. Kuweza kuutekeleza kulingana na kile ambacho Mungu anahitaji, kutenda kwa jitihada ya kumridhisha Mungu, na kutenda kwa kuwajibika na uaminifu—yote haya ni kufikiria mapenzi ya Mungu. Kama hujui jinsi ya kufikiria mapenzi ya Mungu katika suala hilo, lazima ufanye utafutaji fulani ili kukamilisha hilo, na kumridhisha Yeye.

kutoka katika “Ni kwa Kuweka Ukweli Katika Vitendo Tu Ndipo Unaweza Kutupa Minyororo ya Tabia Potovu” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Madondoo ya Mahubiri na Ushirika kwa ajili ya Marejeo:

Kipengele cha kwanza cha udhihirisho wa kupitia mabadiliko katika tabia ni, angalau, uchaji wa Mungu. … Wale wanaomcha Mungu wana nafasi ya Mungu mioyoni mwao. Kwa hakika watatilia maanani mapenzi ya Mungu katika kila kitu, na katika masuala makuu hasa hawatathubutu kufanya maamuzi yasiyo na subira. Wao daima humwomba Mungu na kujaribu kutafuta nia Yake. Kwa mfano, hawathubutu kupuuza au kuacha kwa urahisi mambo yanayohusiana na njia yao katika maisha au masuala yanayohusiana na kanuni za ukweli. Wanapokabiliwa na uchaguzi kuhusu masuala makuu ya mema au maovu, wanaweza kuyaacha mapenzi yao na kuacha mwili wao wenyewe ili kumtii na kumridhisha Mungu. Hii ni ishara ya kuwa mcha Mungu. Wale ambao ni wacha Mungu hakika ni wa kusema kweli zaidi na waaminifu zaidi kuliko mtu wa wastani. Wanashughulikia mambo yao kwa njia ya kisirisiri, wala si kwa ujeuri kama vile walivyofanya awali. Wanafanya mambo kwa utulivu na kwa busara zaidi, si kiholela na bila uangalifu. Inaweza kusemwa kwamba watu kuwa na uchaji wa Mungu ndani yao ni hatua ya kwanza, kwamba ni mwanzo wa mabadiliko katika tabia zao za maisha….

Kipengele cha pili cha udhihirisho wa kupitia mabadiliko katika tabia ni kuweza kutii mipango na mipangilio ya Mungu. Haijalishi anachofanya Mungu, jinsi Mungu anavyowatendea au jinsi vitendo vya Mungu visivyo jinsi wanavyotamani, hawana mawazo na hawalalamiki, lakini wanaweza kutii; wanaweza kufikia hili. Ingawa wana uzoefu na mafunzo mengi ya kushindwa, wanafahamu kweli kwamba mipangilio na mipango ya Mungu ni bora kabisa na ya maana zaidi, na kwamba bila kujali anachofanya Mungu, daima ni cha manufaa kwa watu. Hasa katika masuala ambapo watu wengi huwa na uwezekano wa kukuza fikira kumhusu Mungu, wanaweza kuona kwamba kile afanyacho Mungu ni cha maana zaidi na ni cha kufaa zaidi kukumbuka na kushiriki. Hawana tena uchaguzi wao binafsi katika kile ambacho Mungu hufanya kwa sababu wametambua kwamba Yeye hufanya mambo kwa njia bora zaidi, na kadiri yasivyoweza kufanikishwa zaidi kwa watu, ndivyo yalivyo na umuhimu wa kina zaidi. Ni wakati tu uzoefu wa watu umefikia hatua hii ndipo wanapokuwa na utii wa kweli kwa Mungu. … Wale ambao wamepitia mabadiliko ya tabia wana utii zaidi na mahitaji machache ya kibinafsi. Kutoka nje, hawaonekani kuwa na ufahamu mkubwa au mjibizo kwa matendo ya Mungu; kwa kweli, wanajua vizuri sana mioyoni mwao na ndani yao ni watiifu na wenye shukrani. Huu ndio udhihirisho wa pili wa wale ambao wamebadilika katika tabia.

Kipengele cha tatu cha udhihirisho wa mabadiliko katika tabia ni kuweza kwa uaminifu na kwa hakika kufanya wajibu wa kiumbe aliyeumbwa. Kwa sababu wale ambao tabia zao zimebadilika hupata ufahamu wa wazi wa maana ya kufanya wajibu wa mtu kama kiumbe, hakuna uzembe au udanganyifu katika wajibu wao. Hawalalamiki wakikabiliwa na matatizo au vikwazo, na watahisi huzuni na majuto makubwa kama kazi ya nyumba ya Mungu itakabiliwa na hasara kwa sababu kitu hakijafanyika vizuri. Wao waweka jitihada zote katika kutafuta suluhisho. Watu ambao tabia yao imebadilika huona kufanya wajibu wao kama wito wao, kama wajibu wao wa haki na sahihi. Ikiwa hawajafanya wajibu wao vizuri wanahisi hii ndiyo aibu yao kubwa zaidi na vile vile kushindwa kwao kukuu zaidi kama binadamu. Wanaamini kwamba wale wanaofanya wajibu wao vibaya hawapaswi kuitwa binadamu au kuishi mbele ya Mungu, na kwamba ni kwa kufanya wajibu wa mtu vizuri tu ndipo unaweza kweli kulipa upendo wa Mungu, kustahili kuitwa binadamu, na kuishi duniani. Wale ambao tabia zao zimebadilika huona kufanya wajibu wao vizuri kumridhisha Mungu kama raha na furaha yao wenyewe. Ndiyo sababu pia ni mojawapo ya maonyesho ya msingi ya mabadiliko katika tabia. …

Kipengele cha nne cha udhihirisho wa mabadiliko katika tabia ni kuweza kumpenda Mungu kweli. Katika kupitia kazi ya Mungu, mabadiliko ya tabia yatatokea tu kwa wale wanaopata ukweli kwa hakika. Baada ya tabia ya maisha ya mtu kubadilika, hana tena tabia potovu ya kishetani ya majivuno, kujisifu, kujionyesha, na kujidai. Kwa sababu ana ukweli fulani ndani yake na pia maarifa ya kweli ya Mungu, mafundisho hayo ya kidini, fikira na mawazo hubadilishwa; Kristo ni hazina yake, kwa hiyo anapata njaa zaidi ya maneno ya Mungu. Kadiri anavyoelewa ukweli zaidi, ndivyo anavyoweza kuhisi uzuri wa Mungu zaidi. Anapogundua uzuri wa Mungu zaidi upendo wa Mungu ndani yake unakuwa halisi zaidi na zaidi, na upendo wake wa Mungu unakua kadiri anavyopata ukweli zaidi kutoka Kwake. Mara anapopata ufahamu wa kweli wa Mungu upendo wake kwa Mungu unakuwa wa kweli zaidi. Watu wanaompenda Mungu kweli huchukua moyo wa Kristo kama wao wenyewe, wakifanya kila kitu kulingana na nia ya Kristo. Kama Kristo hajaridhika, bila kujali jinsi wanavyohisi kwamba wamefanya mambo vizuri hawapati furaha kutoka kwayo. Huu ndio wakati wanapoweza kutii mapenzi ya Kristo kikamilifu na kutotenda kulingana na mapenzi yao. Utii wa kweli unatoka kwa ufahamu wa kweli wa Mungu na upendo wa kweli wa Mungu. Utii wa kweli upo tu ndani ya upendo; hakuna upinzani au vikwazo katika upendo. Ni wale tu wanaompenda Mungu kweli ndio wanaoweza kuyazingatia mapenzi Yake katika mambo yote na kuziacha hisia zao wenyewe. Wale ambao tabia zao zimebadilika hakika wanampenda Mungu kweli—bila upendo wa kweli wa Mungu ndani ya mioyo yao, inaweza kusemwa bila shaka kuwa bado hakujakuwa na badiliko katika tabia yao ya maisha. Hili ni bila shaka.

Kipengele cha tano cha udhihirisho wa mabadiliko katika tabia ni kuwa na mahusiano sahihi kati ya watu wawili, yaani, kuwapenda wengine kama unavyojipenda mwenyewe. Mabadiliko ya tabia ni matokeo ya watu kuwa na ukweli fulani ndani yao. Ukweli huu huwa maisha yao kwa viwango tofauti na kubadili hali zao potovu za zamani; hawajishi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya mwili tena, lakini wanaweza kuishi kwa ajili ya Mungu na kuishi kufanya mapenzi ya Mungu. Kwa sababu watu ambao tabia zao zimebadilika wana upendo na utii wa kweli kwa Mungu, wao pia bila shaka wanadhihirisha maonyesho mengi ya upendo kwa wengine, kama vile wasiwasi, upendo, msaada, uvumilivu na ustahimilivu; pia wanaweza kuishi kwa upatanifu na watu. Hawatalazimisha chuki zao wenyewe kwa wengine au kuwa watu wenye kutafuta makosa, kutuhumu, na wenye chuki wanapoona dosari kwa wengine. Wao ni waaminifu kwa wengine na wanaweza kuwatendea watu kulingana na maneno ya Mungu. Jinsi Mungu anavyowasamehe, kuwapenda, na kuwatendea watu hugeuka kuwa kanuni zao za kutenda. Watu wenye mabadiliko ya tabia wanaweza kuuchukulia moyo wa Mungu kama moyo wao wenyewe—wao hawana tu upendo kwa Mungu, bali pia kwa watu wengine, na wanaweza kuishi kwa upatanifu na wale wote walio katika nyumba ya Mungu. Huu ndio mfano wa binadamu wa kufaa ambaye Mungu amezungumzia. Watu ambao tabia zao zimebadilika wanaweza kupenda kile ambacho Mungu hupenda na kuchukia kile ambacho Mungu huchukia, na wana ukweli, kanuni na hekima katika kuwatendea watu. Huu ni udhihirisho wa kipengele cha tano cha mabadiliko katika tabia.
kutoka katika “Maonyesho Matano ya Msingi ya Mabadiliko ya Tabia” katika Mkusanyiko wa Mahubiri—Ruzuku ya Maisha
Yaliyopendekezwa: Umeme wa Mashariki

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni