12.20.2018

nyimbo za dini | Mamlaka ya Mungu ni ya Pekee


I

Mamlaka ya Mungu ni ya pekee; ni maneno Yake maalum na kiini,
ambayo hakuna viumbe wengine walio nayo, walioumbwa au wasioumbwa.
Muumba peke Yake ndiye aliye na mamlaka kama hayo, Mungu wa Pekee ana kiini hiki.
Mungu aliumba kila kitu, Yeye ana mamlaka juu ya vyote. 
Yeye hadhibiti sayari fulani tu, si sehemu ya uumbaji au wanadamu tu.
Lakini Yeye anashikilia yote katika mikono Yake yenye uweza, makubwa au madogo, yanayoonekana au la,
kutoka kwa nyota hadi chembe ndogo ya uhai, na viumbe wote waliopo katika maumbo mengine.
Hii ndiyo maana hasa ya "kila kitu" ambacho Mungu hudhibiti.

II

Mamlaka ya Mungu yanaonekana kuwa magumu kuelewa, lakini sio ya dhahania hata kidogo.
Yako pamoja na mwanadamu kila dakika na kila siku,
mwanadamu anaweza kuona na kuhisi jinsi yalivyo kweli.
Ukweli huu halisi unaonyesha kwamba nguvu za Mungu zipo;
hufanya mwanadamu kufahamu kwamba Mungu tu ndiye ana nguvu kama hiyo.
Mungu aliumba kila kitu, Yeye ana mamlaka juu ya vyote.
Yeye hadhibiti sayari fulani tu, si sehemu ya uumbaji au wanadamu tu.
Lakini Yeye anashikilia yote katika mikono Yake yenye uweza, makubwa au madogo, yanayoonekana au la,
kutoka kwa nyota hadi chembe ndogo ya uhai, na viumbe wote waliopo katika maumbo mengine.
Hii ndiyo maana hasa ya "kila kitu" ambacho Mungu hudhibiti.
Huu ni ulimwengu ambapo Mungu anashika madaraka Yake,
mawanda ya ukuu Wake na utawala.

kutoka katika "Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III" katika Neno Laonekana katika Mwili

kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

       Soma zaidi: Kujua Kanisa la Mwenyezi Mungu


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni