9.14.2018

Papa hapa, Hivi Sasa, Tuungane Pamoja





  • Papa hapa, Hivi Sasa, Tuungane Pamoja
  •  
  • I
  • Kwa kupendana, sisi ni familia. Ah … ah …
  • Papa hapa, hivi sasa, tunaungana;
  • kusanyiko la watu wampendao Mungu.
  • Bila upendeleo, tukishikizwa kwa karibu,
  • furaha na utamu vikijaza nyoyo zetu.
  • Jana tuliacha majuto na hatia; leo tunaelewana,
  • tunaishi katika upendo wa Mungu.
  • Pamoja, tuna furaha zaidi, huru kutoka kwa mwili.
  • Ndugu zangu, pendaneni; sisi ni familia moja.
  • Bila upendeleo, tukishikizwa kwa karibu, Ah … ah …
  • II
  • Papa hapa, hivi sasa, tunaungana;
  • kusanyiko la watu kote ulimwenguni.
  • Mwanzo tukiwa tumepotoshwa lakini tumeokolewa na Mungu.
  • Tuna lugha moja na moyo mmoja, nia moja.
  • Tukishiriki hisia za tulipokuwa tumetengana;
  • na uzoefu na maarifa tuliyonayo.
  • Sasa tumeshika mwendo adhimu wa maisha,
  • mbele yetu, maisha anisi ya baadaye yaliyojaa tumaini na mng'aro.
  • Wakati anisi ujao, uliojaa mng'aro. Ah … ah …
  • III
  • Papa hapa, hivi sasa, tunaungana;
  • lakini hivi punde tutakuwa tumetengana.
  • Hali tumetwishwa mizigo ya kazi na mapenzi ya Mungu,
  • tutatengana kwa ajili ya kazi ya Mungu.
  • Tunapokusanyika, sisi hucheka na kuongea kwa furaha;
  • tunapoondoka, tunatumainishana.
  • Upendo wa Mungu, chanzo chetu cha kuwa watiifu hadi mwisho.
  • Kwa maisha mazuri ya baadaye, tutafanya lolote tutakaloweza.
  • Kwa maisha mazuri ya baadaye, tutafanya lolote tutakaloweza.
  •  
  • kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

             Soma zaidi: Kujua Kanisa la Mwenyezi Mungu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni