9.17.2018

Kuukaribisha Uso Wako Unaotabasamu Unapoonekana Mbele Yangu

Umeme wa Mashariki, hukumu, Nyimbo, Mungu

Kuukaribisha Uso Wako Unaotabasamu Unapoonekana Mbele Yangu

Uliniinua kutoka kwa vumbi hadi ndani ya kumbatio Lako.
Uliamsha moyo wangu kutoka kwa usingizi wa usiku mrefu wa giza.
Nikitazama ndani ya ukungu wangu, naona uso Wako unaotabasamu.
Inauita moyo wangu na upendo wangu.
Sikufikiria kamwe ningeuona uso Wako.
Baraka iliyoje imenipata bila kutarajia.
Baraka iliyoje nilipoona sura Yako.
Kwani natoka mavumbini na sina dhamani yoyote.
Ilhali Mwenyezi Mungu mwenye utukufu Amekuja kwangu uso kwa uso.
Kimya mbele Yako, nasikiliza Unapozungumza.
Maneno Yako yana joto, maneno Yako yana nguvu.
Hukumu na kuadibu vinauamsha moyo wangu.
Upendo wa kweli na mzuri ambao nitashikilia kwa karibu kila wakati.
Uzuri wako unazidi maneno. Ni wa ajabu!
Kuuchukua moyo wangu, kuamsha upendo wangu pia.
Nimekariri kila moja ya sifa Zako nzuri.
Ni matamanio yangu makubwa kukupa Wewe upendo wangu wote.
Kutoa upendo wangu wote Kwako, Kwako.
Uko wapi, mpendwa Mungu wangu? Siwezi kusahau, upendo Wako ni mkubwa sana.
Mbona uniokoe tu kisha ukae mbali?
Hakuna amani hadi upendo Wako ulipwe.
Kwa uchungu moyo wangu unaita, ukikutazamia kwa hamu.
Maneno Yako yakiniongoza, ni kama Uko hapa mbele ya uso wangu.
Pamoja na maneno Yako moyoni mwangu, ni kama Uko na mimi katika upande wangu.
Neno Lako ni maisha yangu, likiuzidi moyo wangu wote.
Kuishi kulingana na neno Lako hunipa amani na furaha.
Nataka kuishi neno Lako, kukutukuza na kukushuhudia Wewe!
Kimya mbele Yako, nasikiliza Unapozungumza.
Maneno Yako yana joto, maneno Yako yana nguvu.
Hukumu na kuadibu vinauamsha moyo wangu.
Upendo wa kweli na mzuri ambao nitashikilia kwa karibu kila wakati.
Uzuri wako unazidi maneno. Ni wa ajabu!
Kuuchukua moyo wangu, kuamsha upendo wangu pia.
Nimekariri kila moja ya sifa Zako nzuri.
Ni matamanio yangu makubwa kukupa Wewe upendo wangu wote.
Kutoa upendo wangu wote Kwako, Kwako.
Nitatimiza wajibu wangu kulipiza upendo Wako na kukamilisha mapenzi Yako.
Naukaribisha uso Wako unaotabasamu unaoonekana mbele yangu.
Ni tamanio langu kuu kukupa Wewe upendo wangu wote.
Nitatimiza wajibu wangu kulipiza upendo Wako na kukamilisha mapenzi Yako.
Naukaribisha uso Wako unaotabasamu unaoonekana mbele yangu.
Ni tamanio langu kuu kukupa Wewe upendo wangu wote.

kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

           Kujua zaidi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni