8.24.2018

Furaha katika Nchi Nzuri ya Kanaani

Mwenyezi Mungu, Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mungu

Furaha katika Nchi Nzuri ya Kanaani

Nimerejea katika familia ya Mungu, nikiwa mwenye msisimko na furaha.
Nina bahati ya kukujua Wewe Mwenyezi Mungu, nimekupa moyo wangu.
Ingawa nimepitia katika Dunia ya Mateso, nimeona jinsi Mungu anavyopendeza.
Upendo wangu kwa Mungu unakuwa siku baada ya siku, Mungu ndiye chanzo cha furaha yangu.
Nimeduwazwa na uzuri wa Mungu, moyo wangu umempenda Yeye.
Siwezi kutosheleza kumpenda Mungu, nyimbo za sifa zinajaa moyoni mwangu.
Nimeduwazwa na uzuri wa Mungu, moyo wangu umempenda Yeye.
Siwezi kamwe kutosheleza kumpenda Mungu, nyimbo za sifa zinajaa moyoni mwangu.
Katika nchi hii iliyobarikiwa ya Kanaani, kila kitu ni kipya, kila kitu kina uhai.
Mwenyezi Mungu anatamka sauti Yake, akituongoza katika Enzi ya Ufalme.
Katika maneno Yake tunapata njia ya kutembea, tukijua njia ambayo mwanadamu anapaswa kuchukua.
Ndoto ya mbinguni sasa inatimia, si tena ya kutafuta, kusaka, kutamani sana.
Kukutana na Mungu uso kwa uso, furaha kweli, kuelewa mapenzi ya Mungu katika neno Lake.
Najua kwamba Mungu ni mwaminifu na mwenye haki, tabia ya Mungu, ya kupendeza isiyoelezeka.
Jinsi gani Anavyopendeza mpendwa wangu! Uzuri Wake unaushika moyo wangu.
Manukato ya mpendwa wangu yananifanya nione ugumu kumwacha.
Nyota zinanitabasamu kwangu angani, jua linaniamkia kutoka juu.
Pamoja na mwanga wa jua, pamoja na jua na umande, matunda ya uzima yanakua kwa uthabiti na kuiva.
Maneno ya Mungu, yaliyojaa na yenye utajiri, yanatuletea karamu tamu kwetu.
Utoaji wa Mungu wenye ukarimu na uliojaa unatufanya tushibe.
Nchi ya Kanaani, nchi ya maneno ya Mungu; upendo Wake unatuletea furaha isiyokoma.
Nchi ya Kanaani, nchi ya maneno ya Mungu; upendo Wake unatuletea furaha isiyokoma.
Harufu nzuri ya matunda imejaa hewani.
Ukiishi hapa kwa siku chache, utaipenda zaidi ya kitu kingine.
Hutataka kamwe kuondoka.
Mwezi wa shaba unaangaza mwanga wake. Mazuri na yenye furaha, yalivyo maisha yangu.
Mpendwa Aliye moyoni mwangu, uzuri Wako unazidi maneno yote.
Moyo wangu una upendo mtamu Kwako, sina budi ila kuruka kwa furaha.
Daima uko moyoni mwangu, nitakuwa na Wewe maisha yangu yote.
Moyo wangu unakutamani sana kila wakati; kukupenda Wewe kunaufurahisha moyo wangu kila siku.
Ee mpendwa uliye moyoni mwangu! Nimekupa upendo wangu wote.
Moyo wangu unakutamani sana kila wakati; kukupenda Wewe kunaufurahisha moyo wangu kila siku.
Ee mpendwa uliye moyoni mwangu! Nimekupa upendo wangu wote.


kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

      Soma zaidi: Kujua Kanisa la Mwenyezi Mungu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni