Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Yehova ni Bwana wa viumbe vyote. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Yehova ni Bwana wa viumbe vyote. Onyesha machapisho yote

10.26.2017

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Kazi Katika Enzi ya Sheria

Yehova , Injili, Umeme wa Mashariki

Kazi katika Enzi ya Sheria

  Mwenyezi Mungu alisema, “Kazi ambayo Yehova alifanya kwa Waisraeli ilianzisha mahali pa Mungu pa asili miongoni mwa binadamu, ambapo pia palikuwa pahali patakatifu ambapo Alikuwapo. Aliwekea kazi Yake mipaka kwa watu wa Israeli. Mwanzoni, Hakufanya kazi nje ya Israeli; badala yake, Aliwachagua watu Aliowaona kuwa wa kufaa ili kuzuia eneo la kazi Yake. Israeli ni mahali ambapo Mungu aliwaumba Adamu na Hawa, na kutoka katika mavumbi ya mahali hapo Yehova alimuumba mwanadamu; mahali hapa pakawa kituo cha kazi Yake duniani. Waisraeli, ambao walikuwa wa ukoo wa Nuhu na pia wa ukoo wa Adamu, walikuwa msingi wa kibinadamu wa kazi ya Yehova duniani.”