7.08.2018

Uchaguzi Kutoka katika Mafungu Kumi ya Neno la Mungu juu ya “Kazi na Kuingia”

Uchaguzi Kutoka katika Mafungu Kumi ya Neno la Mungu juu ya “Kazi na Kuingia”

1. Tangu watu waanze kukanyaga njia sahihi ya maisha, kumekuwa na mambo mengi ambayo bado hayajaeleweka vizuri. Bado wapo kwenye mkanganyiko kabisa kuhusu kazi ya Mungu, na kuhusu kiasi gani cha kazi wanapaswa kufanya. Hii, kwa upande mmoja, ni kwa sababu ya kuwa na uelekeo tofauti wa uzoefu wao na mipaka katika uwezo wao wa kupokea; kwa upande mwingine, ni kwa sababu kazi ya Mungu bado haijawaleta watu katika hatua hii. Kwa hiyo, kila mtu anapata utata kuhusu masuala mengi ya kiroho. Sio tu kwamba hamna uhakika kuhusu kile ambacho mnapaswa kuingia kwacho; bali pia ni wajinga kuhusu kazi ya Mungu. Hili ni zaidi ya suala la hasara kwenu. Ni dosari kubwa iliyopo kwa wale walio katika ulimwengu wa dini. Hii ndiyo sababu kuu ya watu kutomjua Mungu, na hivyo dosari hii ni kasoro ya kawaida miongoni mwa wale wote wanaomtafuta. Hakuna mtu hata mmoja aliyewahi kumjua Mungu, au amekwishawahi kuuona uso Wake halisi. Ni kwa sababu hii ndipo kazi ya Mungu inakuwa ngumu kama kazi ya kuhamisha mlima au kukausha bahari. Ni watu wangapi ambao wamejitoa sadaka maisha yao kwa ajili ya kazi ya Mungu; ni wangapi wametengwa kwa sababu ya kazi Yake; ni wangapi wameteswa hadi kufa kwa ajili ya kazi Yake; ni wangapi wamelia kwa ajili ya upendo wao kwa Mungu, wamekufa pasipo haki; ni wangapi wamekutana na mateso katili na ya kinyama...? Kwamba majanga haya yatapita–hii sio kwa sababu ya watu kutokuwa na maarifa juu ya Mungu? Inawezekanaje mtu ambaye hamjui Mungu awe na ujasiri wa kusimama mbele Yake? Inawezekanaje mtu anayemwamini Mungu na bado anamtesa awe na ujasiri wa kusimama mbele Yake? Haya si makosa kwa wale waliopo katika ulimwengu wa kidini pekee, bali ni makosa ya kawaida kwenu na kwao. Watu wanamwamini Mungu bila kumfahamu, ni kwa sababu hii watu hawamheshimu Mungu kutoka mioyoni mwao, na hawamchi Yeye mioyoni mwao. Hata kuna wale ambao, kwa majivuno makuu na hali, wanafanya kazi ambayo wanafikiria kichwani wenyewe katika mkondo huu, na wanaifanya kazi ya Mungu kulingana na matakwa yao wenyewe na tamaa zao za kibadhirifu. Watu wengi wanafanya ovyoovyo, hawamtukuzi Mungu bali wanafuata mapenzi yao wenyewe. Je, hii si mifano mizuri ya mioyo ya watu yenye ubinafsi? Je, haya hayaonyeshi dalili nyingi zaidi za udanganyifu walionao watu?
kutoka "Kazi na Kuingia (1)" katika Neno Laonekana katika Mwili
2. Watu wanaweza kuwa wenye akili sana, lakini inawezekanaje karama zao zichukue nafasi ya kazi ya Mungu? Watu wanaweza kujali mzigo wa Mungu, lakini hawawezi kufanya mambo kwa ubinafsi sana. Je, matendo ya watu ni ya kiungu kweli? Je, mtu yeyote anaweza kuhakikishwa kwa namna chanya? Kutoa ushuhuda kuhusu Mungu kurithi utukufu Wake—huyu ni Mungu Anayewatenga na kuwainua watu; kwa nafsi yao hawawezi kustahili. Kazi ya Mungu ndio kwanza imeanza, maneno Yake ndio kwanza yameanza kuzungumzwa. Katika hatua hii, watu wanajisikia vizuri kwa nafsi yao wenyewe; hii haiwezi kuwa ni kujitafutia fedheha? Wanaelewa kidogo sana. Hata mwanafalsafa mwenye karama ya juu sana, mzungumzaji mzuri kabisa, hawezi kuelezea yote kuhusu uteule wa Mungu—sembuse nyinyi? Ni vyema msijione wakubwa kabisa kupita viwango vya mbinguni, badala yake jioneni kuwa watu wa chini kabisa kuliko watu razini wengine wanaotafuta kumpenda Mungu. Hii ndiyo njia ambayo kwayo mnapaswa kuingia: kujiona wadogo kuliko wengine wote. Kwa nini mjiweke katika viwango vya juu? Kwa nini mjiweke katika heshima hiyo ya juu? Katika safari ndefu ya maisha, mmepiga hatua chache tu za kwanza. Mnachokiona ni mkono wa Mungu tu, si mwili mzima wa Mungu. Ni wajibu wenu kuiona kazi ya Mungu zaidi, kugundua zaidi juu ya kile mnachopaswa kuingia kwacho, kwa sababu mmebadilika kidogo sana.
kutoka "Kazi na Kuingia (1)" katika Neno Laonekana katika Mwili
3. Kwa kweli, kati ya vitu vingi katika uumbaji wa Mungu, mwanadamu ni wa kiwango cha chini sana. Ingawa ni mtawala wa vitu vyote, mwanadamu ni kiumbe pekee ambaye yupo chini ya hila za Shetani, ni kiumbe pekee ambaye anashikwa kwa namna nyingi katika uharibifu wake. Mwanadamu hajawahi kuwa na ukuu juu yake mwenyewe. Watu wengi wanaishi katika uovu wa Shetani, na kuumizwa na dhihaka zake; anawaudhi kwa njia hii hata hapo watakapokuwa wamelemewa kabisa, wakistahimili kila badiliko, kila ugumu katika ulimwengu wa kibinadamu. Baada ya kuwachezea, Shetani anaweka mwisho wa hatima yao. Na hivyo watu wanapita katika maisha yao yote wakiwa na mkanganyiko, wala hawajawahi kufurahia hata siku moja vitu vizuri ambavyo Mungu Amewaandalia, badala yake wanajeruhiwa na Shetani na kuachwa wakiwa wameharibika kabisa. Leo wamekuwa wadhoofu na walegevu sana kiasi kwamba hawana mwelekeo wa kuzingatia kazi ya Mungu. Ikiwa watu hawana mwelekeo wa kuzingatia kazi ya Mungu, uzoefu wao utabakia kuwa vipandevipande na kutokamilika milele, na kuingia kwao kutabakia sehemu tupu milele.
kutoka "Kazi na Kuingia(1)" katika Neno Laonekana katika Mwili
4. Katika Miaka elfu kadhaa tangu Mungu Alipokuja duniani, idadi yoyote ya watu wenye mawazo ya kiburi wamekuwa wakitumiwa na Mungu kufanya kazi Yake kwa miaka mingi; lakini wale wanaoijua kazi Yake ni wachache sana takribani hawapo kabisa. Kwa sababu hii, idadi kubwa ya watu ambao hawajatajwa wanachukua jukumu la kumpinga Mungu na wakati huo huo wanafanya kazi Yake, kwa sababu, badala ya kufanya kazi Yake, kimsingi wanafanya kazi ya mwanadamu katika nafasi waliyopewa na Mungu. Je, hii inaweza kuitwa kazi? Wanawezaje kuingia? Mwanadamu amechukua neema ya Mungu na kuizika. Kwa sababu hii, kwa karne nyingi zilizopita wale wanaofanya kazi Yake wana kuingia kwa kiwango kidogo. Hawazungumzi juu ya kuijua kazi ya Mungu kwa sababu wana uelewa mdogo wa hekima ya Mungu. Inaweza kusemwa kwamba, ingawa kuna watu wengi wanaomtumikia Mungu, wameshindwa kuona jinsi Alivyoinuliwa, na hii ndiyo sababu watu wamejifanya wao ndio Mungu wa kuabudiwa na watu.
kutoka "Kazi na Kuingia (1)" katika Neno Laonekana katika Mwili
5. Kwa miaka mingi sana Mungu Amebakia sirini katika uumbaji; Ameangalia katika misimu yote ya machipuko na kipupwe nyuma ya umande ufunikao; Ametazama chini kutoka katika mbingu ya tatu kwa siku nyingi sana; Ametembea miongoni mwa wanadamu kwa miezi na miaka mingi sana. Amekaa juu ya wanadamu wote Akisubiri kwa utulivu katika vipindi vingi vya baridi. Hajawahi kujionyesha wazi kwa mtu yeyote yule, wala kutoa sauti hata kidogo, Anaondoka bila ishara na kurudi kimyakimya. Nani anaweza kuujua uso wake halisi? Hajawahi kuzungumza na mwanadamu hata mara moja, Hajawahi kuonekana kwa mwanadamu hata mara moja. Ni rahisi kiasi gani kwa watu kufanya kazi ya Mungu? Wanatambua kidogo tu kwamba kumjua Yeye ni kitu kigumu sana kuliko vitu vyote. Leo Mungu Amezungumza na mwanadamu, lakini mwanadamu hajawahi kumfahamu, kwa sababu kuingia kwake katika maisha ni finyu sana na hakuna kina. Kwa mtazamo Wake, watu hawastahili kabisa kuonekana mbele za Mungu. Wana uelewa mdogo sana juu ya Mungu na wametanga mbali Naye sana. Aidha, mioyo inayomwamini Mungu ni tatanishi sana, na hawana taswira ya Mungu ndani ya mioyo yao. Na matokeo yake, juhudi za Mungu zenye kubeba maumivu, na kazi Yake, kama vipande vya dhahabu vilivyofunikwa mchangani, haviwezi kutoa mwanga. Kwa Mungu, tabia, nia, na mitazamo ya watu hawa ni machukizo sana. Ni dhaifu katika uwezo wao wa kupokea, hawana hisia kiasi cha kufa ganzi, wamejishusha thamani na kuharibika, wametumikishwa kupita kiasi, dhaifu wasiokuwa na dhamiri, ni lazima waongozwe kama ng'ombe na farasi wanavyoongozwa. Kama ilivyo kuingia kwao katika roho, au kuingia katika kazi ya Mungu, hawachukui tahadhari yoyote, hawajizatiti hata kidogo kuteseka kwa ajili ya ukweli. Kwa mtu kama huyu Mungu kumfanya awe mkamilifu haitakuwa rahisi. Hivyo ni muhimu kwamba mnapanga kuingia kwenu katika pembe hii - kwamba kupitia kazi yenu na kuingia kwenu ndipo mnakaribia kuijua kazi ya Mungu.
kutoka "Kazi na Kuingia (1)" katika Neno Laonekana katika Mwili
6. Kazi inapozungumziwa, mwanadamu anaamini kwamba kazi ni kusafiri kwenda huku na huko kwa ajili ya Mungu, akihubiri kila sehemu, na kugharimia rasilmali kwa ajili ya Mungu. Ingawa imani hii ni sahihi, ni ya upande mmoja sana; kile ambacho Mungu Anamwomba mwanadamu si kusafiri kwenda huku na huko kwa ajili ya Mungu; ni huduma zaidi na kujitoa ndani ya roho. Kaka na dada wengi hawajawahi kufikiria juu ya kumfanyia Mungu kazi hata baada ya miaka mingi sana ya uzoefu, maana kazi kama mwanadamu anavyoielewa haipatani na ile ambayo Mungu Anaitaka. Kwa hiyo, mwanadamu havutiwi kwa namna yoyote ile na kazi ya Mungu, na hii ndiyo sababu ya kuingia kwa mwanadamu kuwa kwa upande mmoja. Nyinyi nyote mnapaswa kuingia kwa kumfanyia Mungu kazi, ili kwamba muweze kupata uzoefu wa vipengele vyake vyote. Hiki ndicho mnapaswa kuingia kwacho. Kazi haimaanishi kutembea huku na huko kwa ajili ya Mungu; maana yake ni iwapo maisha ya mwanadamu na kile ambacho mwanadamu anaishi kwa kudhihirisha ni kwa ajili ya Mungu kufurahia. Kazi inamaanisha mwanadamu kutumia uaminifu walionao kwa Mungu na maarifa waliyonayo juu ya Mungu ili kumshuhudia Mungu na kumhudumia mwanadamu. Huu ndio wajibu wa mwanadamu, na kitu ambacho wanadamu wote wanapaswa kutambua. Kwa maneno mengine, kuingia kwenu ni kazi yenu; mnatafuta kuingia wakati wa kazi yenu kwa ajili ya Mungu. Kupata uzoefu wa Mungu sio tu kuweza kula na kunywa neno Lake; na muhimu zaidi, mnapaswa kuwa na uwezo wa kumshuhudia Mungu, kumtumikia Mungu, na kumhudumia mwanadamu. Hii ndiyo kazi, na pia kuingia kwenu; hiki ndicho ambacho kila mwanadamu anapaswa kukitimiza.
kutoka "Kazi na Kuingia (1)" katika Neno Laonekana katika Mwili
7. Kuna watu wengi ambao wanajikita tu katika kusafiri huku na huko kwa ajili ya Mungu, na kuhubiri kila sehemu, halafu hawazingatii uzoefu wao binafsi na kupuuzia kuingia kwao katika maisha ya kiroho. Hiki ndicho kinasababisha wale wanaomtumikia Mungu kuwa watu wanaompinga Mungu. Kwa miaka mingi sana, wale wanaomtumikia Mungu na kumhudumia mwanadamu anaona kufanya kazi na kuhubiri kuwa ndio kuingia, na hakuna anayechukulia uzoefu wake binafsi wa kiroho kuwa kuingia muhimu. Badala yake, wanatumia nuru ya kazi ya Roho Mtakatifu kuwafundisha wengine. Wanapohubiri, wanakuwa na mzigo mkubwa sana na wanapokea kazi ya Roho Mtakatifu, na kupitia hili wanatoa sauti ya Roho Mtakatifu. Wakati huo, wale wanaofanya kazi wanahisi kuridhika kana kwamba kazi ya Roho Mtakatifu ni uzoefu wao binafsi wa kiroho; wanahisi kwamba maneno yote wanayoyazungumza wakati huo ni ya kwao wenyewe.... Baada ya kuwa umehubiri kwa namna hiyo, unahisi kwamba kimo chako halisi sio mdogo kama ulivyoamini. Baada ya Roho Mtakatifu kufanya kazi ndani yako kwa namna ile ile mara kadhaa, basi unaamini kwamba tayari una kimo na unaamini kimakosa kwamba kazi ya Roho Mtakatifu ni kuingia kwako na asili yako binafsi. Unapopitia uzoefu huu kwa mfululizo, unakuwa mzembe kuhusu kuingia kwako. Halafu unakuwa mvivu bila kujua, na kutozingatia kabisa kuingia kwako mwenyewe. Kwa hiyo, unapowahudumia wengine, unapaswa kutofautisha waziwazi kati ya kimo chako na kazi ya Roho Mtakatifu. Hii itasaidia zaidi kuingia kwako na kuunufaisha zaidi uzoefu wako. Mwanadamu kudhani kazi ya Roho Mtakatifu ni uzoefu wake binafsi ndio mwanzo wa upotovu. Hivyo, kazi yoyote mnayoifanya, mnapaswa kuzingatia kuingia kwenu kama somo muhimu.
kutoka "Kazi na Kuingia (1)" katika Neno Laonekana katika Mwili
8. Mtu anafanya kazi ili kutimiza mapenzi ya Mungu, kuwaleta wale wote wanaoutafuta moyo wa Mungu mbele Yake, kumleta mwanadamu kwa Mungu, na kuitambulisha kazi ya Roho Mtakatifu na uongozi wa Mungu kwa mwanadamu, kwa kufanya hivyo atakuwa anayakamilisha matunda ya kazi ya Mungu. Kwa sababu hii, ni muhimu kuelewa kiini cha kufanya kazi. Kama mtu anayetumiwa na Mungu, watu wote wanafaa kumfanyia kazi Mungu, yaani, wote wana fursa ya kutumiwa na Roho Mtakatifu. Hata hivyo kuna hoja moja mnayopaswa kuielewa: Mwanadamu anapofanya kazi ya Mungu, mwanadamu anakuwa na fursa ya kutumiwa na Mungu, lakini kile kinachosemwa na kujulikana na mwanadamu sio kimo cha mwanadamu kabisa. Mnaweza tu kujua vizuri kasoro zako katika kazi yenu, na kupokea nuru kubwa kutoka kwa Roho Mtakatifu, kwa kufanya hivyo mtakuwa mnaweza kupata kuingia kuzuri katika kazi yenu. Kama mwanadamu anachukulia uongozi wa Mungu kuwa ni kuingia kwake mwenyewe na kile kilichomo ndani ya mwanadamu, hakuna uwezekano wa mwanadamu kuongezeka kimo. Roho Mtakatifu humpatia mwanadamu nuru anapokuwa katika hali ya kawaida; katika nyakati kama hizo, mara nyingi mwanadamu anadhani nuru anayopokea ni kimo chake mwenyewe katika uhalisia, maana Roho Mtakatifu Huangazia katika njia ya kawaida: kwa kutumia kile ambacho ni cha asili kwa mwanadamu. Mwanadamu anapofanya kazi na kuzungumza, au wakati mwanadamu anapofanya maombi katika shughuli zake za kiroho, ndipo ukweli utawekwa wazi kwao. Hata hivyo, katika uhalisia, kile ambacho mwanadamu anakiona ni nuru tu iliyoangaziwa na Roho Mtakatifu (kwa asili, hii inahusiana na ushirikiano kutoka kwa mwanadamu) na sio kimo halisi cha mwanadamu. Baada ya kipindi cha kupitia uzoefu ambao mwanadamu anakabiliana na shida nyingi, kimo halisi cha mwanadamu unadhihirika katika mazingira kama hayo. Ni katika muda huo ndipo mwanadamu anagundua kwamba kimo cha mwanadamu sio mkubwa hivyo, na ubinafsi, kujitumainia nafsi, na tamaa za mwanadamu vyote vinaibuka. Ni baada tu ya mizunguko kadhaa ya uzoefu kama huo ndipo wengi wa jinsi hiyo ambao wameamshwa ndani ya roho zao watatambua kwamba haukuwa uhalisia wao hapo nyuma, bali ni nuru ya muda tu kutoka kwa Roho Mtakatifu, na mwanadamu alipokea mwangaza tu. Roho Mtakatifu Anapomwangazia mwanadamu ili kuuelewa ukweli, mara nyingi inakuwa katika namna ya wazi na tofauti, bila muktadha. Yaani, Hayajumuishi matatizo haya ya mwanadamu katika ufunuo huu, na badala yake Anatoa ufunuo moja kwa moja. Mwanadamu anapokabiliana na matatizo katika kuingia, basi mwanadamu anaijumuisha nuru ya Roho Mtakatifu, na huu unakuwa uzoefu halisi wa mwanadamu....Kwa hiyo, mnapoipokea kazi ya Roho Mtakatifu, mnapaswa kujikita zaidi katika kuingia kwenu, na wakati huo huo, kuona kipi ni kazi ya Roho Mtakatifu na kipi ni kuingia kwenu, vilevile kujumuisha kazi ya Roho Mtakatifu katika kuingia kwenu, ili kwamba muweze kukalishwa Naye vizuri na kuruhusu hulka ya kazi ya Roho Mtakatifu kuletwa pamoja ndani yenu. Wakati mnapitia uzoefu wenu wa kazi ya Roho Mtakatifu, mnamjua Roho Mtakatifu, vilevile nyinyi wenyewe, na katikati ya mateso makali, mnajenga uhusianao wa kawaida pamoja na Mungu, na uhusiano baina yenu na Mungu unakuwa wa karibu siku kwa siku. Baada ya michakato mingi ya kupogolewa na kusafishwa, mnakuza upendo wa kweli kwa Mungu. Hii ndiyo sababu mnapaswa kutambua kwamba mateso, mapigo, na dhiki havitishi; kinachoogopesha ni kuwa na kazi ya Roho Mtakatifu tu lakini sio kuingia kwenu. Siku inapofika kwamba kazi ya Mungu imemalizika, mtakuwa mmefanya kazi bure; ingawa mmepitia uzoefu wa kazi ya Mungu, hamtakuwa mmemjua Roho Mtakatifu au kuwa na kuingia kwenu wenyewe. Nuru anayopewa mwanadamu na Roho Mtakatifu si ya kudumisha hisia za mwanadamu; ni kufungua njia kwa ajili ya kuingia kwa mwanadamu, vilevile kumruhusu mwanadamu kumjua Roho Mtakatifu, na kuanzia hapo anakuza moyo wa heshima na ibada kwa Mungu.
kutoka "Kazi na Kuingia (1)" katika Neno Laonekana katika Mwili
9. Mungu Amemwaminia mwanadamu vitu vingi sana na Amezungumza bila kikomo juu ya kuingia kwa mwanadamu. Lakini kwa sababu tabia ya watu ni duni, maneno mengi juu ya Mungu ni shida sana kufuatwa. Kuna sababu mbalimbali za tabia yao duni, kama vile uharibifu wa itikadi na maadili ya binadamu, kutokuwa na malezi mazuri; imani za usihiri zilizojaa moyoni mwa mwanadamu; mtindo wa maisha uliopotoka unaopelekea maradhi mengi katika sehemu ya ndani kabisa ya moyo wa mwanadamu; maarifa ya juujuu ya utamaduni, na takribani asilimia tisini ya watu ambao hawana elimu ya utamaduni na, aidha, watu wachache sana wanapata viwango vya juu vya elimu ya utamaduni, hivyo, kimsingi watu hawajui Roho ni nini na Mungu ni nini, bali wana taswira hafifu ya Mungu na isiyoeleweka vizuri kama wanavyooneshwa na usihiri; mivuto yenye madhara iliyozama ndani kabisa ya moyo wa mwanadamu iliyokuja baada ya maelfu ya miaka ya roho ya utaifa na fikra za utaifa vimewaacha watu wakiwa wamefungwa na kutiwa minyororo, bila uhuru wowote, na kusababisha watu kutokuwa na hamasa, hawana ustahimilivu, hawana shauku ya kusonga mbele lakini badala yake wanakuwa baridi na kurudi nyuma, wakiwa na akili ya utumwa ambayo ina nguvu sana. Na kadhalika na kadhalika. Sababu hizi zimetengeneza taswira mbaya za itikadi, mawazo, maadili na tabia ya kibinadamu. Inaonekana wanadamu wanaishi katika dunia ya giza la kutisha, na hakuna anayetafuta kusonga mbele, hakuna anayefikiria kwenda katika ulimwengu ulio bora. Badala yake, wanakubali tu uchaguzi wao katika maisha na kutumia siku zao kukuza na kuwalea watoto, wakikazana, wakitoka jasho, wakifanya kazi, wakiwa na njozi ya kuwa na familia nzuri na yenye furaha, hisia za tendo la ndoa, adabu kwa mzazi kwa upande wa watoto, kuwa na maisha yenye furaha na kuishi kwa amani. ...Kwa miongo mingi, maelfu, makumi elfu ya miaka hadi leo, watu wamekuwa wakipoteza muda wao, hakuna anayetengeneza maisha makamilifu, wanapigana tu wenyewe kwa wenyewe katika ulimwengu wa giza, wakipambana kupata umaarufu na utajiri, na kufanyiana njama wao kwa wao. Nani aliyekuwa anatafuta mapenzi ya Mungu? Kulikuwa na mtu yeyote aliyekuwa anaitikia kazi ya Mungu? Sehemu hizi zote za ndani ya wanadamu zilizochukuliwa na ushawishi wa giza zimekuwa asili ya mwanadamu toka zamani, hivyo ni vigumu sana kufanya kazi ya Mungu na hata agizo la Mungu halipewi uzito mkubwa leo. Ninaamini kwamba watu hawatanizingatia Ninapotamka maneno haya maana kile Ninachokisema ni historia ya maelfu ya miaka. Kuzungumza juu ya Historia kuna maana ya ukweli, aidha, ni kashfa zinazojulikana kwa wote, sasa kuna maana gani kuzungumza kitu ambacho ni kinyume na ukweli?
kutoka "Kazi na Kuingia (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili
10. Shughuli za kishirikina ambazo watu wanashughulika nazo, Mungu Anazichukia sana. Hata sasa, watu wengi bado hawawezi kuachana nazo na wanafikiri kwamba shughuli hizi za kishirikina zimeamriwa na Mungu, na bado wanazo hadi leo hii, bado hawajaondokana nazo kabisa. Mambo kama sherehe za arusi au mahari, zawadi ya pesa na dhifa na maneno mengine na virai vinavyohusiana na matukio ya sherehe, maneno ya zamani yamerithishwa, na shughuli zote za kishirikina zisizokuwa na maana zinazofanywa kwa niaba ya wafu na taratibu za mazishi, yote haya yanachukiwa sana na Mungu; hata Jumapili (Sabato, kama ilivyoadhimishwa na Wayahudi) pia inachukiwa na Mungu, mahusiano ya kibinadamu na mawasiliano ya kidunia pia yanachukiwa sana na kukataliwa na Mungu. Hata Sikukuu ya Machipuko na Siku ya Krismasi ambazo zinajulikana kwa kila mtu hazikuamriwa na Mungu, sembuse wanasesere na mapambo (keki ya Mwaka Mpya, mafataki, kandili, zawadi za Krismasi, sherehe za Krismasi na Ushirika Matakatifu) maana sikukuu hizi, je, sio sanamu katika mioyo ya watu? Kumega mkate siku ya Sabato, mvinyo na kitani nyembamba navyo ni sanamu. Siku mbalimbali za sherehe za kijadi ambazo ni maarufu sana nchini China, kama vile Siku ya kuinua Vichwa vya Joka, Sikukuu ya Mashua ya Joka, Sikukuu ya Majira ya Kati ya Kupukutika, Sikukuu ya Laba na Siku ya Mwaka Mpya, na sikukuu zisizokuwa na maana kabisa katika ulimwengu wa kidini kama vile Pasaka, Siku ya Ubatizo, na Siku ya Krismasi, zote hizi zimepangwa na kurithishwa kwa watu wengi tangu zama za kale hadi leo, zote hazina ulinganifu na binadamu aliyeumbwa na Mungu. Ni uwezo mkubwa wa fikra za watu na "dhana bunifu" ambazo zimewaruhusu kurithishwa hadi leo. Zinaonekana kuwa hazina kasoro, lakini yote hayo ni ukweli kwamba Shetani alifanya hila zake kwa wanadamu. Kadri Shetani anavyoishi katika eneo fulani ndivyo eneo hilo linarudi nyuma kimaendeleo na kutofaa, ndivyo desturi za kishirikina zinakuwa nyingi zaidi. Vitu hivi vinawafunga watu kwa nguvu, bila kutoa nafasi kwa ajili ya maendeleo. Sikukuu nyingi katika ulimwengu wa kidini zinaonekana kuonyesha uhalisia mkubwa na zinaonekana kujenga daraja katika kazi ya Mungu, lakini ni vifungo visivyoshikika vya Shetani vikifungafunga maarifa ya watu juu ya Mungu, ni hila za Shetani. Kimsingi, hatua ya kazi ya Mungu ilipomalizika, Alikuwa Amekwishaharibu zana zake na mtindo wa wakati huo bila kuacha alama yoyote. Hata hivyo, "waumini wasalihina" bado wanaabudu vitu hivyo vya kushikika na kuacha kile Alicho nacho Mungu bila hata kukichunguza, wanaonekana wanampenda Mungu sana lakini uhalisia ni kwamba wamemtoa ndani ya nyumba zamani sana na kumweka Shetani mezani kwa ajili ya kumwabudu. Sanamu ya Yesu, Msalaba, Maria, Ubatizo wa Yesu na Meza ya Bwana ya Mwisho, vyote hivi, watu wanavichukulia kama Mungu na wanaviabudu wakati wakilia kwa sauti kwa kurudiarudia "Mungu Baba." Je, huu sio utani? Hadi leo, misemo mingi ya kimapokeo kama hiyo iliyorithishwa kwa wanadamu, Mungu anaichukia, na inazuia kabisa njia ya kuelekea kwa Mungu na, aidha, inasababisha hasara kubwa katika kuingia kwa mwanadamu. Mbali na kiwango ambacho Shetani amemharibu mwanadamu, sheria ya Witness Lee, uzoefu wa Lawrence, uchunguzi wa Watchman Nee, na kazi ya Paulo, haya yote yameuteka moyo wa mwanadamu. Mungu hana namna ya kufanya kazi kwa wanadamu kwa sababu ndani yao kuna ubinafsi mwingi, sheria, kanuni, taratibu na mifumo, na vitu hivi, ukiongezea vitendo vya watu vya imani za kishirikina, vimewakamata na kuwaharibu wanadamu. Ni kana kwamba mawazo ya watu yanazunguka, filamu ya kisasili katika rangi, ikiwa na watu wa ajabu wakiendesha mawingu, ya kubuni sana kiasi cha kusisimua na kustaajabisha.
kutoka "Kazi na Kuingia (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili
11. Njia nzuri ya kubadilisha tabia ya mwanadamu ni kuondoa vitu hivi vyenye sumu kubwa katika mioyo ya wanadamu, kuwaacha watu kuanza kubadilisha itikadi na maadili yao. Kwanza kabisa, watu wanatakiwa kuona waziwazi kaida zote hizi za kidini, shughuli za kidini, tarehe, sikukuu, zote Mungu Anazichukia. Wanatakiwa kuwa huru kutoka katika vifungo hivi vya itikadi za kishirikina na kuondoa rangi za kishirikina zilizozama kabisa ndani. Haya yote ni sehemu ya kuingia kwa mwanadamu. Mnatakiwa kuelewa kwa nini Mungu Anawatoa watu kutoka katika ulimwengu usiokuwa na dini, kuwatoa katika kanuni. Hili ndilo lango la kuingia kwenu, ingawa halina uhusiano na uzoefu wenu wa kiroho, haya ni mambo makubwa yanayowazuia kuingia, yanayowazuia kumjua Mungu. Yanatengeza "mtego" unaowakamata watu. Watu wengi wanasoma Biblia sana na wanaweza kukariri mafungu mengi kutoka katika Biblia. Katika kuingia kwao leo, watu bila kujua wanaitumia Biblia kupima kazi ya Mungu kana kwamba msingi wa kazi ya Mungu ni Biblia, na chanzo chake ni Biblia. Kazi ya Mungu inapokuwa sambamba na Biblia, watu wanaunga mkono kazi ya Mungu kwa nguvu zote na kumwangalia Mungu kwa macho mapya; kazi ya Mungu inapokuwa haifanani na Biblia, watu wanakuwa na dukuduku sana kiasi cha kuhangaika na kutafuta msingi wa kazi ya Mungu; kama kazi ya Mungu haikutajwa katika Biblia, watu watampuuza Mungu. Inaweza kusemwa kwamba watu wengi wanakubali kwa hadhari sana, wanatii kwa kusita na wanatambua kwa kawaida uwepo wa kazi ya Mungu, na kuhusu mambo yaliyopita, wanashikilia nusu na kuacha nusu. Je, huku kunaweza kuitwa kuingia? Kushikilia vitabu vya wengine kama hazina, na kuvichukulia kama ufunguo wa dhahabu wa kufungua lango la ufalme, watu hawaonyeshi kuvutiwa na matakwa ya Mungu ya leo. Aidha, "wataalamu wengi wenye akili" katika mkono wao wa kushoto wanashikilia maneno ya Mungu, huku katika mkono wa kulia wanashikilia "kazi kuu" za wengine, kana kwamba wanataka kutafuta msingi wa maneno ya Mungu kutoka katika kazi kuu hizi ili kuthibitisha kabisa kwamba maneno ya Mungu ni sahihi, na hata wanatoa ufafanuzi kwa wengine kwa kuunganisha na kazi kuu, kana kwamba walikuwa wanafanya kazi. Kusema kweli, "watafiti wa kisayansi" wengi miongoni mwa wanadamu hawajawahi kufikiria juu ya mafanikio makubwa ya kisayansi leo, mafanikio ya kisayansi ambayo hayajawahi kufikiriwa (yaani, kazi ya Mungu, maneno ya Mungu na njia ya kuingia uzimani), hivyo watu "wanajitegemea," wakihubiri" wakitegemea sana ndimi zao, wakiringia "jina zuri la Mungu." Hata hivyo, kuingia kwao kupo hatarini na umbali wa matakwa ya Mungu unaonekana kuwa mbali sana kama kuanzia uumbaji hadi wakati huu. Ni rahisi kiasi gani kufanya kazi ya Mungu?
kutoka "Kazi na Kuingia (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili
12. Inaonekana watu wamekwishaamua kuacha nusu yao kwa mambo ya zamani na kuleta nusu yao kwa wakati wa leo, nusu kwa Shetani na nusu kwa Mungu, kana kwamba hii ndiyo njia ya kuwa na dhamiri iliyotulia na kuweza kuwa na hisia ya utulivu fulani. Mioyo ya watu inadhuru sana kwa siri, wanaogopa sio tu kupoteza kesho bali pia wanahofia kupoteza jana, wanaogopa sana kumkosea Shetani na kumkosea Mungu wa leo Anayeonekana kuwa ndiye na kuwa siye. Kwa sababu itikadi na maadili ya watu ni duni sana, uwezo wao wa kutambua vitu kwa kweli ni mbaya, na kimsingi hawajui kama kazi ya leo ni ile kazi ya Mungu au siyo. Pengine ni kwa sababu fikra za kishirikina za watu zimekita sana mizizi kiasi kwamba ushirikina na ukweli, Mungu na sanamu, vinawekwa katika kundi moja; wala hawajali kuweka tofauti baina ya vitu hivi. Inaonekana kama wametesa bongo zao lakini bado mambo hayo hayajawa wazi. Na hiyo ndio maana wanadamu wanasimama katika njia zao na hawawezi tena kusonga mbele. Haya yote yanatokea kwa sababu watu hawana elimu ya itikadi ambayo ni sahihi, kitu ambacho kinawafanya iwe vigumu katika kuingia kwao. Na matokeo yake, watu wanapoteza mvuto kabisa katika kazi ya Mungu wa kweli, bali wanaendelea kung'ang'ania katika kazi ya mwanadamu (kama vile watu wanaotazamwa kuwa ni watu wakubwa) kana kwamba imepigwa muhuri. Je, haya si masomo mapya kabisa kwa ajili ya kuingia kwa mwanadamu?
kutoka "Kazi na Kuingia (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili
13. Ikiwa mwanadamu anaweza kuingia kabisa kulingana na kazi ya Roho Mtakatifu, maisha yake yatachipuka haraka kama mmea wa mwanzi baada ya mvua ya majira ya kuchipua. Kwa kuangalia kimo cha sasa wa watu wengi, hakuna mtu hata mmoja anayetilia mkazo umuhimu wa uzima. Badala yake, watu wanaweka umuhimu katika baadhi ya mambo ya juujuu yasiyokuwa na umuhimu. Au wanakimbia huku na kule na kufanya kazi bila malengo na ovyoovyo bila mwelekeo, hawajui waende njia gani na zaidi kwa ajili ya nani. "Wanajificha wenyewe katika unyenyekevu." Ukweli ni kwamba, ni wachache miongoni mwenu mnaojua makusudi ya Mungu kuhusu siku za mwisho. Ni wachache sana miongoni mwenu wanaojua nyayo za Mungu, na wachache zaidi wanajua utimilifu wa mwisho wa Mungu utakavyokuwa. Halafu kila mtu, kwa utashi tupu, anakubali kufundishwa nidhamu na kushughulikiwa na wengine, kama vile anarekebisha na kusubiri siku ambayo hatimaye wamekwishaifanya na wanaweza kustarehe. Sitatoa maoni yoyote juu ya "maajabu" haya miongoni mwa watu, lakini kuna hoja moja ambayo wote mnapaswa kuielewa. Kwa sasa watu wengi wanaelekea katika hali isiyo ya kawaida, hatua zao za kuingia tayari zinaelekea katika mwisho wa mauti. Pengine watu wengi wanafikiri kwamba mwanadamu anatamani "Shangri-La" ('bonde la utulivu'), wakiamini kuwa ni "sehemu ya uhuru." Kimsingi, sivyo ilivyo. Mtu anaweza kusema kwamba watu wamekwishapotoka tayari.
kutoka "Kazi na Kuingia (4)" katika Neno Laonekana katika Mwili
14. Mungu Amekuwa mwili katika nchi ya China, ambayo wenyeji wa Hong Kong na Taiwan wanaiita bara. Mungu Alipokuja kutoka juu na kuja duniani, hakuna mtu mbinguni wala duniani aliyejua, maana hii ndiyo maana ya kweli ya Mungu kurudi kwa namna ya siri. Amekuwa katika mwili Akifanya kazi na kuishi kwa muda mrefu, bado hakuna mtu yeyote aliyejua. Hata leo hii, hakuna mtu anayetambua. Pengine hiki kitabakia kuwa kitendawili cha milele. Mungu kuja katika mwili wakati huu sio kitu ambacho mtu yeyote anaweza kujua. Haijalishi ni kwa kiwango kikubwa kiasi gani Roho Mtakatifu Anafanya kazi, siku zote Mungu yupo katika hali ya utulivu, kamwe Hajiachilii mbali. Mtu anaweza kusema kwamba inaonekana kama hatua hii ya kazi Yake inafanyika mbinguni. Ingawa ipo wazi kabisa kwa kila mtu, hakuna anayeitambua. Mungu Atakapomaliza hatua hii ya kazi Yake, kila mtu atazinduka kutoka katika ndoto yake na kugeuza mitazamo yao ya zamani. Nakumbuka Mungu Alishawahi kusema, "Kuja katika mwili wakati huu ni sawa na kuanguka katika tundu la duma.” Hii ina maana kwamba kwa sababu awamu hii ya kazi ya Mungu imemfanya Mungu kuja katika Mwili na kuzaliwa katika makazi ya joka kuu jekundu, kuja Kwake duniani wakati huu kumeambatana na hatari nyingi zaidi. Anachokabiliana nacho ni visu na bunduki na kumbi za starehe; Anavyokabiliana navyo ni vishawishi; Anaokutana nao ni umati wa watu wenye sura za wauaji. Ana hatari ya kuuawa wakati wowote. Mungu Alikuja na ghadhabu. Hata hivyo, Alikuja ili Aweze kufanya kazi ya utakasaji, ikiwa na maana kwamba kufanya sehemu ya pili ya kazi Yake inayoendelea baada ya kazi ya wokovu. Kwa ajili ya hatua hii ya kazi Yake, Mungu Amejitolea mawazo na uangalizi wa hali ya juu kabisa na Anatumia njia yoyote inayoweza kufikiriwa ili kuepuka mashambulio ya majaribu, Anajificha katika unyenyekevu Wake na kamwe haringii utambulisho Wake. Katika kumwokoa mwanadamu msalabani, Yesu Alikuwa Anakamilisha tu kazi ya wokovu; Alikuwa hafanyi kazi ya utakasaji. Hivyo ni nusu tu ya kazi ya Mungu ndiyo ilikuwa inafanywa, na kukamilisha kazi ya ukombozi ilikuwa ni nusu ya mpango Wake mzima. Kwa kuwa enzi mpya ilikuwa inakaribia kuanza na ile ya zamani kukaribia kutoweka, Mungu Baba Alianza kukusudia sehemu ya pili ya kazi Yake na Akaanza kujiandaa kwa ajili yake. Wakati uliopita, kupata mwili huku katika siku za mwisho huenda hakukutolewa unabii, na hivyo kuweka msingi wa usiri mkubwa unaozunguka ujio wa Mungu katika mwili kipindi hiki. Wakati wa mapambazuko, bila kujulikana kwa mtu yeyote, Mungu Alikuja duniani na Akaanza maisha Yake katika mwili. Watu hawakujua kipindi hiki. Pengine wote walikuwa wamelala, pengine wengi waliokuwa wanakesha walikuwa wanasubiri, na pengine wengi walikuwa wanamwomba Mungu wa mbinguni kimyakimya. Lakini miongoni mwa watu hawa wote, hakuna hata mmoja aliyejua kuwa Mungu tayari Amekwishawasili duniani. Mungu Alifanya hivi ili Aifanye kazi Yake kwa urahisi na kupata matokeo bora zaidi, na pia ilikuwa ni kwa sababu ya kuepuka majaribu zaidi. Mwanadamu anapoamka kutoka usingizini, kazi ya Mungu itakuwa imekwishakamilika zamani sana na Ataondoka, na kufunga maisha Yake ya kutembeatembea na kusafiri duniani. Kwa kuwa kazi ya Mungu inamtaka Mungu kutenda na kuzungumza Yeye binafsi, na kwa kuwa hakuna namna ambayo mwanadamu anaweza kusaidia, Mungu Ameyavumilia maumivu makali ya kuja duniani kufanya kazi Yeye Mwenyewe. Mwanadamu hawezi kushikilia nafasi ya kazi ya Mungu. Kwa hiyo Mungu Alijihatarisha mara elfu kadhaa kuliko ilivyokuwa katika wakati wa Enzi ya Neema na kuja chini mahali ambapo joka kuu jekundu linaishi ili kufanya kazi Yake, kuweka mawazo Yake yote na uangalizi katika kuokoa kundi hili la watu maskini, kulikomboa kundi hili la watu lililogeuka na kuwa rundo la samadi. Ingawa hakuna anayejua uwepo wa Mungu, Mungu Hahangaiki kwa sababu ni faida kubwa kwa kazi ya Mungu. Kila mtu ni mwovu sana, sasa inawezekanaje kila mtu avumilie uwepo wa Mungu? Ndiyo maana duniani, Mungu Anakuwa kimya siku zote. Haijalishi mwanadamu ni katili kiasi gani, Mungu wala Hazingatii hayo moyoni Mwake hata kidogo, bali Anaendelea kufanya kazi Anayotaka kufanya ili kutimiza agizo kuu ambalo Baba wa mbinguni Alimpatia. Ni nani miongoni mwenu aliyetambua upendo wa Mungu? Ni nani anayejali sana mzigo Alionao Mungu Baba kuliko Mwana Wake Anavyofanya? Ni nani awezaye kuelewa mapenzi ya Mungu Baba? Roho wa Mungu Baba Aliyeko mbinguni Anasumbuka kila mara, na Mwana Wake duniani Anaomba mara kwa mara juu ya mapenzi ya Mungu Baba, Akihofia moyo Wake kuumia. Kuna mtu yeyote anayejua kuhusu upendo wa Mungu Baba kwa Mwana Wake? Kuna mtu yeyote anayejua jinsi ambavyo Mwana mpendwa Anavyomkumbuka Mungu Baba? Wakipata shida ya kuchagua kati ya mbingu na nchi, utaona wawili Hawa wanatazamana wakati wote kutoka kwa mbali, sambamba na Roho. Ee binadamu! Ni lini mtaufikiria moyo wa Mungu? Ni lini mtaielewa nia ya Mungu? Baba na Mwana siku zote Wamekuwa Wakitegemeana. Kwa nini tena Watengane, mmoja juu mbinguni na mmoja chini duniani? Baba Anampenda Mwana Wake kama vile Mwana Anavyompenda Baba Yake. Kwa nini sasa asubiri kwa muda mrefu huku Akiwa na shauku hiyo? Ingawa Hawajatengana kwa muda mrefu, je, mtu yeyote anajua kwamba Baba tayari Amekuwa Akitaka sana kwa shauku kwa siku nyingi na Amekuwa Akitarajia kwa muda mrefu kurudi haraka kwa Mwana Wake mpendwa? Anatazama, Anakaa kwa utulivu, Anasubiri. Hii yote ni kwa ajili ya kutaka Mwana Wake mpendwa Arudi haraka. Ni lini Atakuwa tena na Mwana ambaye Anazungukazunguka duniani? Ingawa watakapokuwa pamoja tena, Watakuwa pamoja milele, Anawezaje kustahimili maelfu ya siku za utengano, mmoja juu mbinguni na mwingine chini duniani. Makumi ya miaka duniani ni kama maelfu ya miaka mbinguni. Mungu Baba Anawezaje kutokuwa na wasiwasi? Mungu Anapokuja duniani, Anakabiliana na mabadiliko mengi ya ulimwengu wa kibinadamu kama mwanadamu. Mungu Mwenyewe hana hatia, sasa kwa nini Mungu Ateseke kwa maumivu kama mwanadamu? Pengine ndiyo maana Mungu Baba Anatamani sana Mwana Wake Arudi haraka; nani awezaye kuujua moyo wa Mungu? Mungu Anampatia mwanadamu vitu vingi sana; mwanadamu anawezaje kuulipa moyo wa Mungu kikamilifu? Lakini mwanadamu anampatia Mungu kidogo sana; sasa Mungu Atawezaje kutokuwa na wasiwasi?
kutoka "Kazi na Kuingia (4)" katika Neno Laonekana katika Mwili
15. Ni wachache sana miongoni mwa wanadamu wanaouelewa moyo wa Mungu kwa sababu tabia za watu ni duni sana na hisia zao za kiroho zimepoa sana, na kwa sababu hawaoni wala kutilia maanani kile ambacho Mungu anafanya. Hivyo Mungu Anaendelea kuwa na hofu juu ya mwanadamu, kana kwamba asili ya tabia ya wanyama ndani ya mwanadamu inaweza kuonekana muda wowote. Hii inaonyesha zaidi kwamba kuja kwa Mungu duniani kunaambatana na majaribu makubwa. Lakini kwa ajili ya kukamilisha kundi la watu, Mungu, Akiwa na utukufu, Alimwambia mwanadamu juu ya kila kusudi lake, bila kuficha kitu. Ameamua kwa dhati kukamilisha kundi hili la watu. Kwa hiyo, ije shida yoyote au jaribu, Anatazama mbali na kuyapuuzia yote. Anafanya kazi yake kimyakimya tu, Akiamini kwamba siku moja ambapo Mungu Atapata utukufu, mwanadamu atamjua Mungu, na kuamini kwamba mwanadamu atakapokuwa amekamilishwa na Mungu, atakuwa ameuelewa moyo wa Mungu kikamilifu. Sasa hivi kunaweza kuwepo watu wanaomjaribu Mungu au kumwelewa vibaya Mungu au kumlaumu Mungu; Mungu wala hayazingatii haya moyoni. Mungu atakapoingia katika utukufu, watu wote wataelewa kwamba kila kitu ambacho Mungu Anafanya ni kwa ajili ya mema ya binadamu, na watu wote wataelewa kwamba kila kitu ambacho Mungu Anafanya ni kwa sababu binadamu aweze kuishi vizuri. Ujio wa Mungu umeambatana na majaribu, na Mungu pia Anakuja katika adhama na ghadhabu Yangu. Muda ambapo Mungu Anamwacha mwanadamu, Atakuwa tayari Amepata utukufu, na Ataondoka Akiwa Amejawa na utukufu mwingi na furaha ya kurudi. Mungu Anayefanya kazi duniani Hazingatii mambo moyoni Mwake haijalishi watu wamemkataa kiasi gani. Yeye Anafanya tu kazi Yake.
kutoka "Kazi na Kuingia (4)" katika Neno Laonekana katika Mwili
16. Uumbaji wa Mungu wa ulimwengu unaanzia mbali maelfu ya miaka huko nyuma, Amekuja duniani kufanya kazi isiyoweza kupimika, na Amepitia uzoefu mkubwa wa kukataliwa na kashfa. Hakuna anayekaribisha ujio wa Mungu; kila mtu anamwangalia tu kwa jicho kavu. Katika kipindi hiki cha maelfu ya miaka ya taabu, matendo ya mwanadamu yamevunjavunja moyo wa Mungu tangu zamani sana. Wala Hazingatii tena uasi wa watu, lakini badala yake Anatengeneza mpango tofauti ili kumbadilisha na kumsafisha mwanadamu. Dhihaka na kashfa, mateso, dhiki, mateso ya msalaba, kutengwa na wanadamu, na kadhalika ambayo Mungu Alipitia Akiwa katika mwili, Mungu Amepitia ya kutosha. Mungu katika mwili Ameteseka kikamilifu na shida za ulimwengu wa wanadamu. Roho wa Mungu Baba wa mbinguni Aliona mambo hayo hayavumiliki na Akarudisha kichwa Chake nyuma na kufumba macho Yake, Akisubiri Mwana Wake mpendwa kurudi. Yote Anayoyatamani ni kwamba watu wote wasikie na kutii, waweze kuhisi aibu kubwa mbele ya mwili Wake, na wasiasi dhidi Yake. Anachokitamani ni kwamba watu wote waamini kwamba Mungu yupo. Aliacha zamani sana kutaka mambo makubwa kutoka kwa mwanadamu kwa sababu Mungu Amelipa gharama kubwa sana, lakini mwanadamu bado anajistarehesha, haiweki kabisa kazi ya Mungu moyoni mwake.
kutoka "Kazi na Kuingia (4)" katika Neno Laonekana katika Mwili
17. Leo wote mnajua kwamba Mungu Anawaongoza watu katika njia sahihi ya uzima, kwamba Anamwongoza mwanadamu kuingia katika hatua nyingine kuingia katika enzi nyingine, huru kutoka katika enzi hii ya giza, ya kale, kutoka katika mwili, kutoka kwenye ukandamizaji wa nguvu za giza na ushawishi wa Shetani, Akimruhusu kuishi katika ulimwengu wa uhuru. Kwa manufaa ya kesho ya kupendeza, ili kwamba watu wasibanwe katika hatua zao kesho, Roho wa Mungu Anapanga kila kitu kwa ajili ya mwanadamu, na ili kwamba mwanadamu aweze kuwa na furaha kubwa, Mungu Anajitolea jitihada Zake zote katika mwili Akiandaa njia mbele ya mwanadamu, ili kwamba siku ambayo mwanadamu anaitamani sana iweze kuja haraka. Nyote mnaweza kufurahia wakati huu mzuri, maana si rahisi kufanya mkutano na Mungu, na ingawa hamjawahi kumjua, mna muda mrefu tangu mmekutana Naye. Ikiwa tu kila mtu angeweza kukumbuka milele siku zote hizi nzuri lakini fupi, na kuzifanya kuwa mambo yao ya kuwafurahisha duniani.
kutoka "Kazi na Kuingia (5)" katika Neno Laonekana katika Mwili
18. Kwa maelfu ya miaka, Wachina wamekuwa wakiishi maisha ya utumwa na hii imebana mawazo yao, dhana, maisha, lugha, tabia na matendo kiasi kwamba wamebaki bila uhuru wowote. Maelfu kadhaa ya miaka ya historia imewabadilisha watu muhimu kutoka kutawaliwa na roho na kuwa kitu kinachofanana na maiti iliyoondokewa na roho. Wengi ni wale wanaoishi chini ya upanga wa Shetani, wengi wanaishi katika makazi yanayofanana na pango la mnyama, wengi wanakula chakula kama wanachokula ng'ombe au farasi, wengi wapo katika mchafuko huko ahera na hawana maana kabisa. Katika umbo, watu hawana tofauti na watu wa zamani, sehemu yao ya kupumzika ni kama kuzimu, na wote wanaowazunguka wanakuwa na mashetani na mapepo wachafu. Kwa umbo la nje, wanaonekana kuwa ni wanyama wenye mabadiliko ya hali ya juu; kimsingi wanaishi na kukaa na mashetani wachafu. Bila mtu yeyote kuwashughulikia, watu wanaishi katika mtego uliojificha wa Shetani, na wamenaswa kabisa kiasi kwamba hawawezi kutoroka. Hawakusanyiki na wapendwa wao katika makazi yao ya furaha, kuishi kwa furaha na kuyaishi maisha ya kuridhisha, bali wanaishi Kuzimu, wakishughulika na mapepo na kushirikiana na mashetani. Kimsingi, watu bado wamefungwa na Shetani, wanaishi mahali ambapo pepo wachafu wanakusanyika, wanatawaliwa na hawa mapepo wachafu, na ni kama vitanda vyao vipo mahali ambapo maiti zao zimelala, kana kwamba ni sehemu zao za kustarehe.
kutoka "Kazi na Kuingia (5)" katika Neno Laonekana katika Mwili
19. Mwanadamu anaishi bega kwa bega na wanyama, na wanatembea pamoja kwa amani bila ugomvi au vita vya maneno. Mwanadamu ni mgumu kuridhika vile anavyowajali na anavyohusika na wanyama, na wanyama wapo kwa ajili ya mwanadamu kuishi, ni kwa maslahi ya mwanadamu, bila wao kunufaika na chochote na kumtii mwanadamu kikamilifu. Kwa namna zote, uhusiano kati ya mwanadamu na mnyama ni wa karibu na wa amani–na pepo wachafu, inaweza kuonekana ni muungano kamilifu wa mwanadamu na mnyama. Hivyo, mwanadamu na pepo wachafu duniani wanafurahia ukaribu wao mkubwa, na hawawezi kuachana: Mwanadamu anaonekana kufarakana na pepo wachafu, lakini kimsingi ameunganika nao, wakati pepo wachafu hawamnyimi mwanadamu kitu chochote, na "wanajitoa" vyote walivyonavyo kwao. Kila siku, watu wanachacharika katika "kasri la mfalme wa kuzimu," wakichezacheza na "mfalme wa kuzimu" (babu yao), na kutawaliwa naye. Leo, watu wanapakwa masizi, na kuishi muda mrefu sana Kuzimuni, wana muda mrefu toka waache kutamani kurudi katika dunia ya viumbe hai. Hivyo, mara tu wanapoiona nuru, na kutazama matakwa ya Mungu, na tabia ya Mungu, na kazi ya Mungu, wanakuwa na wasiwasi na kuhisi kucheza dansi; bado wanatamani sana kurudi kuzimu na kuishi na mizimu. Wamemsahau Mungu zamani sana, na hivyo wamekuwa wakizungukazunguka katika makaburi.
kutoka "Kazi na Kuingia (5)" katika Neno Laonekana katika Mwili
20. Kazi na kuingia kwa uhalisia ni vya kiutendaji na vinarejelea kazi ya Mungu na kuingia kwa mwanadamu. Mwanadamu kukosa kabisa uelewa juu ya sura halisi ya Mungu na kazi ya Mungu kumesababisha shida kubwa katika kuingia kwake. Leo hii, watu wengi bado hawajui kazi ambayo Mungu anatimiza katika siku za mwisho, au kwa nini Mungu Anastahimili fedheha kubwa kupita kiasi kuja katika mwili na kusimama na mwanadamu katika makovu na majonzi. Mwanadamu hajui chochote kuhusu lengo la kazi ya Mungu, wala kusudi la mpango wa Mungu kwa ajili ya siku za mwisho. Kwa sababu mbalimbali, watu daima wanakuwa vuguvugu katika kuingia ambako Mungu anataka na wanabakia kuutilia mashaka, kitu ambacho kimeleta shida kubwa katika kazi ya Mungu katika mwili. Watu wanaonekana kuwa vizuizi na, leo hii, bado wanakuwa hawana uelewa sahihi. Kwa hiyo Nitazungumza juu ya kazi ambayo Mungu anafanya kwa mwanadamu, na makusudi ya Mungu ya haraka, ili kwamba nyinyi nyote muwe watumishi waaminifu wa Mungu ambao, kama Ayubu, ni bora ufe kuliko kumkataa Mungu na utastahimili kila fedheha, na ambao, kama Petro, mtatoa utu wenu wote kwa Mungu na kuwa wandani ambao Mungu Aliwapata katika siku za mwisho. Ninawasihi kaka na dada kufanya kila kitu kilichopo ndani ya uwezo wao kutoa utu wao wote kwa mapenzi ya kimbingu ya Mungu, kuwa watumishi watakatifu katika nyumba ya Mungu, na kufurahia ahadi zisizokuwa na kikomo zilizotolewa na Mungu, ili kwamba moyo wa Mungu Baba ufurahie pumziko la amani. "Kukamilisha mapenzi ya Mungu Baba" kunapaswa kuwe wito wa wote wanaompenda Mungu. Maneno haya yanapaswa kutumika kama mwongozo wa mwanadamu kwa ajili ya kuingia na dira inayoongoza matendo yake. Hili ndilo suluhisho ambalo mwanadamu anapaswa kuwa nalo. Kukamilisha kabisa kazi ya Mungu duniani na kushirikiana na kazi ya Mungu katika mwili–huu ni wajibu wa mwanadamu. Siku moja, kazi ya Mungu itakapokuwa imekamilika, mwanadamu atamuaga Anaporudi mapema kwa Baba yake mbinguni. Je, huu sio wajibu ambao mwanadamu anapaswa kuutimiza?
kutoka "Kazi na Kuingia (5)" katika Neno Laonekana katika Mwili
21. Kwa mwanadamu, Mungu kusulubiwa kulihitimisha kazi ya Mungu kupata mwili, Aliwakomboa binadamu wote , na Akamruhusu kuteka ufunguo wa Kuzimu. Kila mtu anadhani kwamba kazi ya Mungu imekamilika kikamilifu. Kwa uhalisia, kwa Mungu, ni sehemu ndogo tu ya kazi Yake ndiyo imekamilika. Amemkomboa tu binadamu; Hajamshinda mwanadamu, wala kubadilisha ubaya wa Shetani kwa binadamu. Hiyo ndio maana Mungu Anasema, "Ingawa mwili Wangu ulipitia maumivu ya kifo, hilo sio lengo lote la Mimi kupata mwili. Yesu ni Mwana Wangu mpendwa na Alisulubishwa msalabani kwa ajili Yangu, lakini hakukamilisha kikamilifu kazi Yangu. Alifanya tu sehemu." Hivyo Mungu Akaanza mpango wa mzunguko wa pili ili kuendeleza kazi ya Mungu kupata mwili. Lengo kuu la Mungu ni kumkamilisha na kumpata kila mmoja aokolewe kutoka katika mikono ya Shetani, hiyo ndiyo sababu Mungu Alijiandaa tena kujihatarisha kuja katika mwili.
kutoka "Kazi na Kuingia (6)" katika Neno Laonekana katika Mwili
22. Katika maeneo mengi, Mungu Alitabiri kupata kundi la washindi katika nchi ya Sinim. Ni upande wa Mashariki mwa ulimwengu ambapo washindi wanapatikana, hivyo nchi ambapo Mungu kupata mwili mara ya pili Atatua bila shaka ni nchi ya Sinim, mahali ambapo joka jekundu linaishi. Hapo Mungu Atawapata warithi wa joka kuu jekundu na litashindwa na kuaibishwa. Mungu Anataka kuwaamsha watu hawa walioteseka sana, kuwaamsha kabisa, na kuwafanya waondoke katika ukungu na kulikataa joka kuu jekundu. Mungu Anataka Awaamshe kutoka katika ndoto zao, kuwafanya waelewe tabia ya joka kuu jekundu, kuutoa moyo wao wote kwa Mungu, kuinuka kutoka katika nguvu kandamizi za giza, kusimama Mashariki mwa dunia, na kuwa uthibitisho wa ushindi wa Mungu. Baada ya hapo Mungu Atakuwa Amepata utukufu. Kwa sababu hii tu, kazi ambayo ilisitishwa Israeli Mungu Aliipeleka katika nchi ambapo linakaa joka kuu jekundu na, takribani miaka elfu mbili baada ya kuondoka, Amekuja tena katika mwili ili kuendeleza kazi ya Enzi ya Neema. Mwanadamu anashuhudia kwa macho yake, Mungu Akizindua kazi mpya katika mwili. Lakini kwa Mungu, Anaendeleza kazi ya Enzi ya Neema, kwa mwachano wa miaka elfu kadhaa, na badiliko tu la eneo la kufanyia kazi na mradi wa kazi. Ingawa taswira ya mwili ambayo Mungu Ameichukua katika kazi ya leo ni mtu mwingine tofauti na Yesu, Wanashiriki hulka na mzizi mmoja, na wanatoka katika chanzo kimoja. Pengine wana tofauti za umbo la nje, lakini kweli za ndani za kazi Zao zinafanana kabisa. Hata hivyo, enzi zenyewe, ni tofauti kama ilivyo usiku na mchana. Inawezekanaje kazi ya Mungu isibadilike? Au inawezekanaje kazi ziingiliane?
kutoka "Kazi na Kuingia (6)" katika Neno Laonekana katika Mwili
23. Yesu Alionekana katika umbo la Wayahudi, Alifuata mavazi ya Wayahudi, na Alikua akila chakula cha kiyahudi. Hii ni hali yake ya kawaida ya kibinadamu. Lakini Mungu katika mwili wa leo Anachukua umbo la watu wa Asia na Anakua Akila chakula cha taifa la joka kuu jekundu. Hii haiingiliani na lengo la Mungu kupata mwili. Badala yake, vinakamilishana, na zaidi vinakamilisha maana ya kweli ya Mungu kupata mwili. Kwa sababu Mungu katika mwili Anarejelewa kuwa "Mwana wa Adamu" au "Kristo," umbo la nje la Kristo wa leo haliwezi kulinganishwa na Yesu Kristo. Hata hivyo, mwili huu unaitwa "Mwana wa Adamu" na Yupo katika sura ya mwili. Kila hatua ya kazi ya Mungu inahusisha maana ya kina sana. Sababu ya Yesu kuzaliwa kwa njia ya Roho Mtakatifu ni kwa sababu Alipaswa kuwakomboa wenye dhambi. Alitakiwa Asiwe na dhambi. Isipokuwa tu mwishoni Alipolazimishwa kufanana na mwili wa dhambi na kuchukua dhambi za wenye dhambi ndivyo Aliweza kuwaokoa kutoka katika laana ya msalaba ambao Mungu Alitumia kuwaadibu watu. (Msalaba ni zana ya Mungu kwa ajili ya kuwalaani na kuwarudi watu; mitajo ya kulaani na kurudi mahususi inahusu kuwalaani na kuwarudi wenye dhambi.) Lengo lilikuwa ni kuwafanya wenye dhambi wote kutubu na kutumia msalaba kuwafanya waungame dhambi zao. Yaani, kwa ajili ya kuwakomboa binadamu wote, Mungu Alijiweka Mwenyewe katika mwili uliozaliwa kwa njia ya Roho Mtakatifu na Akachukua dhambi za binadamu wote. Namna ya kawaida ya kuelezea hii ni kutoa mwili mtakatifu kwa kubadilishana na wenye dhambi wote, usawa wa Yesu kuwa sadaka ya dhambi umewekwa mbele ya Shetani ili "kumsihi" Shetani kuwarudisha binadamu wote wasio na hatia kwa Mungu. Hivyo ili kukamilisha hatua hii ya kazi ya wokovu kulihitaji utungaji mimba kwa njia ya Roho Mtakatifu. Hili lilikuwa ni sharti la lazima, "mkataba" wakati wa vita kati ya Mungu Baba na Shetani. Hii ndio maana Yesu Alitolewa kwa Shetani, ni baada ya hapo tu ndipo hatua hii ya kazi ikahitimishwa. Hata hivyo, kazi ya ukombozi ya Mungu leo tayari ni ya umuhimu usio kifani, na Shetani hana sababu ya kufanya madai, hivyo Mungu kufanyika mwili hakuhitaji utungaji mimba kwa njia ya Roho Mtakatifu, maana Mungu kwa asili ni mtakatifu na Asiye na hatia. Hivyo Mungu mwenye mwili wa wakati huu sio tena Yesu wa Enzi ya Neema. Lakini bado Yupo kwa ajili ya mapenzi ya Mungu Baba na kwa ajili ya kutimiza matamanio ya Mungu Baba. Hii inaweza kuchukuliwaje kuwa ni msemo usiokuwa na maana? Je, ni lazima Mungu kupata mwili kufuate kanuni kadhaa?
kutoka "Kazi na Kuingia (6)" katika Neno Laonekana katika Mwili
24. Watu wengi wanatafuta ushahidi katika Biblia, wakitaka kutafuta unabii wa Mungu kupata mwili. Inawezekanaje fikra hafifu za mwanadamu kujua kwamba Mungu Aliacha "kufanya" kazi muda mrefu kwenye Biblia na "Ameachana" nayo na kufurahia kazi ambayo Alipanga kwa muda mrefu lakini Hakuwahi kumwambia mwanadamu? Watu wanakosa sana ufahamu. Baada tu ya kuonja tabia ya Mungu, kwa kawaida wanasimama kwenye jukwaa refu na kukaa kwenye "kiti mwendo" cha hali ya juu wakikagua kazi ya Mungu, na kwenda mbali zaidi kumfundisha Mungu kwa mazungumzo ya misamiati migumu. "Mzee" akiwa amevaa miwani na kupapasa ndevu zake, anafunua Biblia yake kuukuu ambayo amekuwa akiisoma maisha yake yote. Akimumunya maneno na kupepesapepesa macho, sasa anarudi katika Kitabu cha Ufunuo na sasa katika kitabu cha Danieli, na sasa katika Kitabu kinachojulikana sana cha Isaya. Akikodolea macho ukurasa ulioandikwa maneno mengi madogo, anasoma kimya, akili yake ikizunguka bila kupumzika. Ghafula mkono unaopapasa ndevu unasita na kuanza kuzivuta. Kila mara mtu anasikia sauti ya ndevu zikivunjika. Tabia hiyo isiyo ya kawaida inamstaajabisha mtu. "Kwa nini kutumia nguvu zote hizo? Kilichomkasirisha hivyo ni nini? Turudi kwa mtu mzee, nyusi zake sasa zimesimama. Nyusi zenye rangi ya fedha zimeanguka kama manyoya ya bata bukini sentimita mbili kamili kutoka katika kope za mzee huyu, kama tu kwa bahati lakini kwa usahihi kabisa, mzee huyu anaendelea kukaza macho yake katika karatasi. Anarudia mtiririko huo wa matendo mara kadhaa, kisha anashindwa kuvumilia bali anasimama na kuanza kuzungumzazungumza kana kwamba anafanya mazungumzo na mtu, ingawa mwanga katika macho yake bado haujatoka katika shajara yake. Ghafula anafunika ukurasa aliokuwa anausoma na kugeukia "ulimwengu mwingine." Mwendo wake ni wa haraka sana na wa kuogopesha takribani kuwashtua watu. Sasa, panya ambaye ametoka katika shimo lake na ndio tu ameanza "kujisikia yupo huru" wakati wa ukimya wake alishtushwa sana na mizunguko yake isiyoeleweka na kukimbia kurudi kwenye shimo lake, na kutoweka bila kujua alipoelekea. Sasa mkono wa kulia wa mzee uliokuwa umetulia unarudia mwendo wake wa kupapasa ndevu juu chini. Anaondoka kwenye kiti, na kuacha kitabu mezani. Kupitia katika mlango ulio wazi kidogo na dirisha lililo wazi, upepo unaingia ndani, bila kujali unapeperusha kitabu kinajifunika, kisha kinafunguka, kinajifunika, kisha kinafunguka tena. Kuna ukiwa usioweza kuelezeka kuhusu tukio hili, isipokuwa tu kwa sauti ya kurasa za kitabu zinapopeperushwa na upepo, kila kitu kinaonekana kuwa kimya. Yeye, pamoja na mikono aliyojikumbatia kwa nyuma, anatembeatembea chumbani, sasa anasimama, sasa anaanza, anatikisa kichwa chake mara kwa mara, anaonekana kurudia kusema "Ee! Mungu! Unaweza kweli kufanya hivyo?" Muda hadi muda pia anatikisa kichwa, "Ee Mungu! Nani anaweza kuijua kazi Yako? Ni vigumu kiasi gani kuchunguza hatua Zako? Ninaamini Hufanyi vitu visivyokuwa na maana." Sasa mzee huyu anakunja uso, macho yake anayafumba kwa nguvu, akionyesha sura iliyokasirika, pia anaonyesha maumivu makali kupita kiasi, kana kwamba anataka kutafakari taratibu. Hii kweli inampatia changamoto "mzee huyu." Katika hatua hii ya maisha yake, "kwa bahati mbaya" amekutana na suala hili. Nini kinaweza kufanyika juu yake? Nami pia sina nguvu ya kufanya kitu chochote. Nani alifanya shajara yake kuwa "ya njano"? Nani alifanya ndevu na nyusi zake kukua bila huruma kama theluji nyeupe katika maeneo mbalimbali ya uso wake? Ni kana kwamba ndevu zake zinawakilisha usuli wake. Lakini nani angejua mwanadamu angekuwa mpumbavu kwa kiasi hiki, akitafuta uwepo wa Mungu katika shajara kuukuu? Shajara hii ya zamani inaweza kuwa na karatasi ngapi? Je, inaweza kweli kurekodi matendo yote ya Mungu? Nani anathubutu kuhakikisha hilo? Mwanadamu kimsingi anatafuta umbo la Mungu na anajaribu kutimiza mapenzi ya Mungu kwa kuchanganua zaidi maneno? Je, kujaribu kuingia katika uzima kwa namna hii, ni rahisi kama inavyosikika? Je, huku sio kufikiri bila mantiki na kimakosa? Huoni hii inachekesha?
kutoka "Kazi na Kuingia (6)" katika Neno Laonekana katika Mwili
25. Mungu Anakuja miongoni mwa wanadamu siku ya leo kwa kusudi la kubadilisha mawazo na roho zao, na taswira ya Mungu katika mioyo yao ambayo wamekuwa nayo kwa maelfu ya miaka. Kupitia fursa hii, Atamfanya mwanadamu kuwa mkamilifu. Yaani, kupitia maarifa ya mwanadamu, Atabadilisha namna wanavyomfahamu na mitazamo yao Kwake, ili kwamba maarifa yao juu ya Mungu, yaweze kuanza katika rekodi safi, na mioyo yao itakuwa imesafishwa upya na kubadilishwa. Kushughulika na nidhamu ni njia, na ushindi na kufanya upya ni malengo. Kuondoa mawazo ya kishirikina aliyonayo mwanadamu kuhusu Mungu asiye dhahiri ndilo limekuwa kusudi la Mungu milele, na hivi karibuni limekuwa suala la haraka kwake. Ni matumaini Yangu kwamba watu wote watalifikiria hili zaidi. Wabadilishe jinsi kila mtu anavyopitia uzoefu ili kwamba kusudi hili la haraka la Mungu liweze kufanyika hivi karibuni na hatua ya mwisho ya kazi ya Mungu duniani iweze kuhitimishwa kwa matokeo mazuri. Onyesheni uaminifu wenu kama mnavyopaswa, na ufariji moyo wa Mungu kwa mara ya mwisho. Ni matumaini Yangu kwamba hakuna mtu yeyote miongoni mwa kaka na dada atakayekwepa jukumu hili au kuzungukazunguka tu.
kutoka "Kazi na Kuingia (6)" katika Neno Laonekana katika Mwili
26. Mungu Anakuja katika mwili wakati huu kwa mwaliko, na kutokana na hali ya mwanadamu. Yaani, Anakuja kumpatia mwanadamu kile alichokuwa anahitaji. Atakuja kumwezesha kila mwanadamu, wa tabia yoyote au jamii, kuona neno la Mungu na, kutoka katika neno Lake, kuona uwepo na udhihirishaji wa Mungu na kukubali ukamilishaji wa Mungu. Neno lake litabadilisha mawazo na mitazamo ya mwanadamu ili kwamba sura ya kweli ya Mungu ikite mizizi kabisa katika moyo wa mwanadamu. Hili ndilo tamanio pekee la Mungu duniani. Haijalishi jinsi gani asili ya mwanadamu ilivyo, jinsi gani asili yake ilivyo duni, au matendo yake yalivyokuwa huko nyuma, Mungu Hajali haya. Anatumainia tu mwanadamu kuisafisha kabisa taswira ya Mungu aliyonayo moyoni mwake na kuijua asili ya binadamu, na hapo Atakuwa Amebadilisha mtazamo wa kiitikadi wa mwanadamu. Anatarajia mwanadamu kuwa na shauku ya kina kwa Mungu na kuwa na mahusiano ya milele na Yeye. Hiki ndicho Mungu Anachomwomba mwanadamu.
kutoka "Kazi na Kuingia (7)" katika Neno Laonekana katika Mwili
27. Maarifa ya maelfu kadhaa ya miaka ya utamaduni wa kale na historia vimefunga fikra na dhana na akili ya mwanadamu kwa nguvu sana kiasi cha kutoweza kupenyeka na kutoweza kubadilishwa. Mwanadamu anaishi katika ngazi ya kumi na nane ya kuzimu, kana kwamba wamefukuziwa chini na Mungu, wasiweze kuona mwanga tena. Fikra za kishirikina zimemkandamiza mwanadamu kiasi kwamba mwanadamu anaweza kupumua kwa shida sana na hivyo kufa kwa kukosa hewa. Hawana nguvu hata kidogo ya kupinga, kimya kimya wanaendelea kuvumilia na kuvumilia... Hakuna hata mmoja aliyewahi kujaribu kupigana au kusimama kwa ajili ya uadilifu na haki; wanaishi maisha ambayo hayana tofauti na maisha ya mnyama, huku wakinyanyaswa na kushambuliwa na mabwana wa ushirikina, mwaka baada ya mwaka, siku baada ya siku. Mwanadamu hajawahi kufikiria kumtafuta Mungu ili kufurahia furaha duniani. Ni kana kwamba mwanadamu amepigwa, kama majani ya majira ya kupukutika, yaliyonyauka na kukauka kabisa. Mwanadamu amepoteza kumbukumbu na anaishi bila matumaini kuzimu kwa jina la ulimwengu wa kibinadamu, akisubiri ujio wa siku ya mwisho ili kwamba waweze kupotea pamoja na kuzimu, kana kwamba siku ya mwisho wanayoitamani sana ni siku watakayofurahia pumziko la amani. Maadili ya kishirikina yamempeleka mwanadamu "Kuzimu," kiasi kwamba mwanadamu anakuwa na uwezo mdogo wa kupinga. Ukandamizaji wa aina mbalimbali umemlazimisha mwanadamu taratibu kuzama chini kabisa Kuzimu na kutanga mbali kabisa na Mungu. Sasa, Mungu Amekuwa mgeni kabisa kwa mwanadamu, na mwanadamu bado anafanya haraka kumwepuka wanapokutana. Mwanadamu hamtambui na anamtenga kana kwamba mwanadamu hajawahi kumwona hapo kabla.... Maarifa ya utamaduni wa kale kwa taratibu yamemwondoa mwanadamu kutoka katika uwepo wa Mungu na kumweka mwanadamu kwa mfalme wa mashetani na wana wake. Vitabu Vinne na Maandiko ya Kale ya Kiyunani Matano vimepeleka fikra na mawazo ya mwanadamu katika enzi nyingine ya uasi, na kumfanya mwanadamu kuendelea kuwaabudu wale walioandika Vitabu hivyo na Maandiko ya Kiyunani, wakikuza zaidi mitazamo yao juu ya Mungu. Mfalme wa mashetani bila huruma alimtupa Mungu nje kutoka katika moyo wa mwanadamu bila wao kujua, huku akifurahia kuuchukua moyo wa mwanadamu. Baada ya hapo na kuendelea mwanadamu akawa na roho mbaya na ya uovu akiwa na sura ya mfalme wa mashetani. Chuki juu ya Mungu ilijaza kifua chao na sumu ya mfalme wa mashetani ikasambaa ndani ya mwanadamu hadi alipomalizwa kabisa. Mwanadamu hakuwa na uhuru tena na hakuweza kuvunja vifungo vya mfalme wa mashetani. Kwa hiyo, mwanadamu angeweza kuendelea kukaa pale tu na kufungwa, kujisalimisha kwake na kujitiisha kwake. Amepanda zamani sana mbegu ya kutoamini kuwa kuna Mungu ndani ya moyo mchanga wa mwanadamu, akimfundisha mwanadamu dhana za uongo kama vile, "kujifunza sayansi na teknolojia, kutambua Vipengele Vinne vya Usasa, hakuna Mungu duniani." Si hivyo tu, ametangaza kwa kurudiarudia, "Hebu tujenge makazi mazuri sana kwa kufanya kazi kwa bidii," akiwaomba wote kujiandaa toka wakiwa watoto kutumikia nchi yao." Mwanadamu amepelekwa mbele yake bila kujitambua, na bila kusita akajichukulia sifa (akimrejelea Mungu akiwa Ameshikilia binadamu mzima katika mikono Yake). Hajawahi kuhisi aibu au kuwa na hisia yoyote ya aibu. Aidha, bila aibu amewanyakua watu wa Mungu na kuwaweka katika nyumba yake, wakati akirukaruka kama panya mezani na kumfanya mwanadamu amwabudu kama Mungu. Ni ujahili kabisa huu! Anaropoka tuhuma hizo za kushtua, "Hakuna Mungu duniani. Upepo upo kwa ajili ya sheria za asili; mvua ni unyevunyevu unaoganda na kudondoka chini kama matone; tetemeko la ardhi ni mtikisiko wa uso wa ardhi kwa sababu ya mabadiliko ya jiolojia; ukame ni kwa sababu ya ukavu hewani kwa mwingiliano wa kinyuklia katika uso wa jua. Haya ni matukio ya asili. Ni sehemu gani ambayo ni tendo la Mungu?" Hata anaropoka[a] kauli kama hizi: "Mwanadamu alitokana na sokwe wa zamani, na dunia leo imeendelea kutoka katika jamii ya kale ya takribani miaka bilioni moja iliyopita. Ama nchi inaendelea au inaanguka inaamuliwa na mikono ya watu wake." Mwanadamu amemning'iniza ukutani miguu juu kichwa chini na kumweka mezani ili kutunzwa vizuri na kuabudiwa. Anapokuwa anapiga kelele kwamba "Hakuna Mungu," anajichukulia mwenyewe kuwa ni Mungu, na kumsukumia mbali Mungu nje ya mipaka ya dunia bila huruma. Anasimama katika sehemu ya Mungu na kutenda kama mfalme wa mashetani. Ni upuuzi mkubwa kiasi gani! Anamsababisha mtu kuteketezwa na chuki yenye sumu. Inaonekana kwamba Mungu ni adui wake mkubwa na Mungu Hapatani naye kabisa. Anafanya hila zake za kumfukuza Mungu wakati anabakia bila kuadhibiwa kwa kiasi kikubwa. Huyo kweli ni mfalme wa mashetani! Tunawezaje kuvumilia uwepo wake? Hatapumzika hadi awe ameisumbua kazi ya Mungu na kuiacha katika matambara na kuwa katika hali ya shaghalabaghala, kana kwamba anataka kumpinga Mungu hadi mwisho, hadi mmoja kati yao awe ameangamia. Anampinga Mungu kwa makusudi na kusogea karibu zaidi. Sura yake ya kuchukiza imefunuliwa toka zamani na sasa imevilia damu na kugongwagongwa, ipo katika hali mbaya sana, lakini bado hapunguzi hasira zake kwa Mungu, kana kwamba anatamani kummeza Mungu kabisa kwa mara moja ili kutuliza hasira moyoni mwake. Tunawezaje kumvumilia, huyu adui wa Mungu anayechukiwa! Ni kumalizwa kwake na kuondolewa kabisa ndiko kutaleta mwisho wa matamanio yetu ya maisha. Anawezaje kuruhusiwa kuendelea kukimbia ovyoovyo? Amemharibu mwanadamu kwa kiwango ambacho mwanadamu hajui ’mahali pa raha zote, na anakuwa mfu na hajitambui. Mwanadamu amepoteza uwezo wa kawaida wa kufikiri wa kibinadamu. Kwa nini tusijitoe sadaka uhai wetu wote kumwangamiza na kumchoma na kuondoa kabisa hofu ya hatari inayobakia na kuruhusu kazi ya Mungu kuufikia uzuri usiotarajiwa hivi karibuni? Genge hili la waovu limekuja miongoni mwa wanadamu na kusababisha hofu na shida kubwa. Wamewaleta wanadamu wote katika ukingo wa jabali, wakipanga kwa siri kuwasukumia chini wavunjike vipande vipande na kumeza maiti zao. Wana matumaini ya kuharibu mpango wa Mungu na kushindana na Mungu katika pambano ambalo ana nafasi ndogo sana ya kushinda. Hiyo kwa vyovyote vile ni rahisi! Msalaba umeandaliwa, mahususi kwa ajili ya mfalme wa mashetani ambaye ni mwenye hatia ya makosa maovu sana. Mungu si wa msalaba tena na Amekwishamwachia Shetani. Mungu Aliibuka mshindi muda mrefu uliopita, Hahisi tena huzuni juu ya dhambi za binadamu. Ataleta wokovu kwa binadamu wote.
kutoka "Kazi na Kuingia(7)" katika Neno Laonekana katika Mwili
28. Kutoka juu hadi chini na kuanzia mwanzo hadi mwisho, amekuwa akisumbua kazi ya Mungu na kutenda kinyume Chake. Mazungumzo yote ya "urithi wa utamaduni wa kale," "maarifa ya thamani ya utamaduni wa kale," "mafundisho ya imani ya Tao na imani ya Confucius,” na "maandiko ya kale ya Confucius na ibada ya kishirikina" vimempeleka mwanadamu kuzimu. Sayansi na teknolojia ya kisasa, vilevile maendeleo ya viwanda, kilimo, na biashara havionekeni popote. Badala yake, anasisitiza ibada za kishirikina zilizoenezwa na "masokwe" wa kale kwa makusudi kabisa kuingilia, kupinga na kuharibu kazi ya Mungu. Sio tu amemtesa mwanadamu hadi leo hii, bali anataka kummaliza mwanadamu kabisa. Mafundisho ya maadili ya kishirikina na kurithisha maarifa ya utamaduni wa kale vimemwambukiza mwanadamu kwa muda mrefu na kumbadilisha mwanadamu kuwa mashetani wakubwa na wadogo. Kuna wachache sana ambao wapo tayari kumpokea Mungu na kukaribisha kwa furaha ujio wa Mungu. Uso wa mwanadamu umejawa na mauaji, na katika sehemu zote, kifo kipo hewani. Wanatafuta kumwondoa Mungu katika nchi hii; wakiwa na visu na mapanga mikononi, wanajipanga katika pambano kumwangamiza Mungu. Sanamu zimetapakaa nchi nzima ya shetani ambapo mwanadamu anafundishwa kuwa hakuna Mungu. Juu ya nchi hii kunatoka harufu mbaya sana ya karatasi linaloungua na ubani, ni harufu nzito sana inayomaliza hewa. Inaonekana kuwa ni harufu ya uchafu unaopeperuka wakati joka anapojisogeza na kujizungusha, na ni harufu ambayo mwanadamu hawezi kuvumilia bali kutapika tu. Licha ya hiyo, kunaweza kusikika pepo waovu wakikariri maandiko. Sauti inaonekana kutoka mbali kuzimu, na mwanadamu hawezi kujizua kusikia baridi ikiteremka chini ya uti wake. Katika nchi hii sanamu zimetapakaa, zikiwa na rangi zote za upinde wa mvua, ambazo zinaibadilisha nchi kuwa ulimwengu unaometameta, na mfalme wa mashetani amekenua, kana kwamba njama zake ovu zimefanikiwa. Wakati huo mwanadamu hana habari naye, wala mwanadamu hajui kwamba shetani amekwishamharibu kwa kiwango ambacho amekuwa hawezi kuhisi na ameshindwa. Anatamani kumfutilia mbali Mungu mara moja, na kumtukana na kumwangamiza, na kujaribu kuchana na kuvuruga kazi Yake. Anawezaje kumruhusu Mungu kuwa wa "hadhi sawa"? Anawezaje kumvumilia Mungu "akiingilia" kazi yake miongoni mwa wanadamu wa duniani? Anawezaje kumruhusu Mungu kufichua uso wake wa chuki? Anawezaje kumruhusu Mungu kuingilia kazi yake? Inawezekanaje Shetani huyu anayevimba kwa ghadhabu, amruhusu Mungu kutawala nguvu yake duniani? Anawezaje kukubali kushindwa kwa urahisi? Sura yake ya chuki imefunuliwa wazi, hivyo mtu anajikuta hajui kama acheke au alie, na ni vigumu sana kuzungumzia hili. Hii si asili yake? Akiwa na roho mbaya, bado anaamini kwamba yeye ni mzuri kupita kiasi. Genge hili la washiriki jinai! Wanakuja miongoni mwa walio na mwili wa kufa na kuendeleza starehe na kuvuruga mpangilio. Usumbufu wao unaleta kigeugeu duniani na kusababisha hofu katika moyo wa mwanadamu, na wamemharibu mwanadamu kiasi kwamba mwanadamu anafanana na wanyama wabaya wasioweza kuvumilika, wala hana tena hata chembe ya mwanadamu asilia mtakatifu. Hata wanatamani kutawala kama madikteta duniani. Wanakwamisha kazi ya Mungu ili kwamba isiweze kusonga mbele na kumfunga mwanadamu kana kwamba wapo nyuma ya kuta za shaba na chuma cha pua. Baada ya kufanya dhambi nyingi sana na kusababisha shida nyingi sana, wanawezaje kutarajia kitu chochote tofauti na kusubiri kuadibu? Mapepo na roho wa Shetani wamekuwa wakicharuka duniani na wamefunga mapenzi na jitihada za maumivu za Mungu, na kuwafanya wasiweze kupenyeka. Ni dhambi ya mauti kiasi gani! Inawezekanaje Mungu Asiwe na wasiwasi? Inawezekanaje Mungu Asiwe na ghadhabu? Wanasababisha vikwazo vya kusikitisha na upinzani kwa kazi ya Mungu. Uasi wa kutisha! Hata mapepo hao wadogo kwa wakubwa wanajivunia nguvu za Shetani mwenye nguvu zaidi na kuanza kufanya fujo. Kwa makusudi wanapinga ukweli licha ya kuuelewa vizuri. Wana wa uasi! Ni kana kwamba, sasa mfalme wao amepanda kwenda katika kiti cha enzi cha kifalme, wamekuwa wa kuridhika nafsi na kuwatendea wengine wote kwa dharau. Ni wangapi wanautafuta ukweli na kufuata haki? Wote ni wanyama kama tu nguruwe na mbwa, wakuongoza genge la nzi wanaonuka katika rundo la kinyesi na kuchomeka vichwa vyao na kuharibu mpangilio. Wanaamini kwamba mfalme wao wa kuzimu ni mkuu wa wafalme wote, bila kutambua kwamba si chochote zaidi ya nzi katika kitu kilichooza. Si hivyo tu, wanatoa maoni ya kashfa dhidi ya uwepo wa Mungu kwa kutegemea nguruwe na mbwa wa wazazi wao. Nzi wadogo wanadhani wazazi wao ni wakubwa kama nyangumi mwenye meno. Hawatambui kwamba wao ni wadogo sana, wazazi wao ni nguruwe na mbwa wachafu mara bilioni kuliko wao wenyewe? Hawatambui uduni wao, wanacharuka kwa misingi ya harufu iliyooza ya nguruwe na mbwa hao na wana mawazo ya udanganyifu ya kuzaa vizazi vijavyo. Huko ni kukosa aibu kabisa! Wakiwa na mbawa za kijani mgongoni mwao (hii inarejelea wao kudai kuwa wanamwamini Mungu), wanaanza kuwa na majivuno na kiburi juu ya uzuri wao na mvuto wao, kwa siri kabisa wanamtupia mwanadamu uchafu wao. Na hata ni wa kuridhika nafsi, kana kwamba jozi ya mbawa zenye rangi ya upinde wa mvua zingeweza kuficha uchafu wao, na hivyo wanautesa uwepo wa Mungu wa kweli (hii inarejelea kisa cha ndani cha ulimwengu wa kidini). Mwanadamu anajua kidogo kwamba, ingawa mbawa za nzi ni nzuri za kupendeza, hata hivyo ni nzi mdogo tu aliyejaa uchafu na kujazwa na vijidudu. Kwa kutegemea uwezo wa nguruwe na mbwa wa wazazi wao, wanacharuka nchi nzima (hii inarejelea viongozi wa dini wanaomtesa Mungu kwa misingi ya uungwaji mkono mkubwa kutoka katika nchi inayomsaliti Mungu wa kweli na ukweli) kwa ukatili uliopitiliza. Ni kana kwamba mizimu ya Mafarisayo wa Kiyahudi wamerudi pamoja na Mungu katika nchi ya joka kuu jekundu, wamerudi katika kiota chao cha zamani. Wameanza kazi yao tena ya utesaji, wakiendeleza kazi yao yenye umri wa maelfu kadhaa ya miaka. Kikundi hiki cha waliopotoka ni hakika kitaangamia duniani hatimaye! Inaonekana kwamba, baada ya milenia kadhaa, roho wachafu wamekuwa wenye hila na wadanganyifu sana. Muda wote wanafikiri juu ya njia za kuidhoofisha kazi ya Mungu kwa siri. Ni werevu sana na wajanja na wanatamani kurudia katika nchi yao kufanya majanga yaliyotokea maelfu kadhaa ya miaka iliyopita. Hii takribani imfanye Mungu kulia kwa sauti kuu, na Anajizuia sana kurudi katika mbingu ya tatu ili Awaangamize. Kwa mwanadamu kumpenda Mungu ni lazima aelewe mapenzi Yake na furaha Yake na huzuni, vilevile na kile Anachokichukia zaidi. Hii itakuza zaidi kuingia kwa mwanadamu. Kadri mwanadamu anavyoingia kwa haraka, ndivyo moyo wa Mungu unavyoridhika; kadri mwanadamu anavyomtambua kwa uwazi mfalme wa mashetani, ndivyo mwanadamu anavyosogea karibu zaidi kwa Mungu, ili kwamba matamanio yake yaweze kutimizwa.
kutoka "Kazi na Kuingia (7)" katika Neno Laonekana katika Mwili
29. Nimezungumza mara nyingi sana kwamba kazi ya Mungu ya siku za mwisho ni kwa ajili ya kubadilisha roho ya kila mtu, kubadilisha nafsi ya kila mtu, ili kwamba moyo wake, ambao umeteseka sana na kiwewe, uwe umebadilishwa, hivyo kuokoa roho zao, ambazo zimeumizwa kwa kina zaidi na Shetani; ni kwa sababu ya kuamsha roho za watu, kuyeyusha mioyo yao baridi, na kuwaruhusu kurudisha nguvu za ujana. Haya ndiyo mapenzi makubwa ya Mungu. Weka pembeni mazungumzo ya ni namna gani maisha na uzoefu wa mwanadamu ni ya kiburi au ya kina k; mioyo ya watu itakapokuwa imeamshwa, wanapokuwa wameamshwa kutoka katika ndoto zao na kujua kikamilifu madhara yaliyoletwa na joka kuu jekundu, kazi ya huduma ya Mungu itakuwa imekamilika. Siku ambayo kazi ya Mungu itakuwa imekamilika ni wakati ambapo mwanadamu ataanza rasmi njia ya imani sahihi kwa Mungu. Wakati huu, huduma ya Mungu itakuwa imekamilika: Kazi ya Mungu katika mwili itakuwa imekamilika kabisa, na mwanadamu atakuwa ameanza rasmi kufanya kazi ambayo anapaswa kufanya—atafanya huduma yake. Hizi ni hatua za kazi ya Mungu. Hivyo mnapaswa kutafuta kwa kupapasa kuingia kwenu katika misingi ya kujua mambo haya. Haya yote ndiyo mnayopaswa kuyajua.
kutoka "Kazi na Kuingia(8)" katika Neno Laonekana katika Mwili
30. Kuingia kwa mwanadamu kutaboreka tu pale ambapo mabadiliko yatatokea ndani kabisa ya moyo wake, maana kazi ya Mungu ni wokovu kamili wa mwanadamu—mwanadamu aliyekombolewa, ambaye bado anaishi chini ya nguvu za giza, na ambaye hajawahi kuzinduka kutoka katika eneo hili la kusanyiko la mapepo; ili kwamba mwanadamu aweze kuwekwa huru dhidi ya milenia ya dhambi, na kuwa wapendwa wa Mungu, kumkanyaga kabisa joka kuu jekundu, kuanzisha ufalme wa Mungu, na kuupumzisha moyo wa Mungu mapema, ni kutoa mawazo bila woga, bila kubania, kwa chuki inayovimbisha kifua chenu, kuondoa kabisa vijidudu hivyo, kuwafanya muache maisha haya ambayo hayana tofauti na maisha ya ng'ombe au farasi, ili msiwe watumwa tena, ili msiweze kukanyagwa tena au kuamrishwa na joka kuu jekundu; hamtakuwa tena wa taifa hili lililoanguka, hamtakuwa tena wa joka kuu jekundu lenye chuki, hamtafungwa nalo tena. Kiota cha mapepo hakika kitachanwachanwa na Mungu, na mtasimama kando ya Mungu—nyinyi ni wa Mungu, na sio wa dola hii ya watumwa. Mungu Ameichukia sana jamii hii ya giza toka zamani. Anasaga meno Yake, Akitamani kumkanyaga mwovu huyu, joka wa zamani mwenye chuki, ili kwamba asiinuke tena, na hatamnyanyasa tena mwanadamu; Hatasamehe matendo yake ya zamani, Hatavumilia udanganyifu wake kwa mwanadamu, atalipiza kisasi kwa kila kosa alilofanya katika enzi zote; Mungu Hatamhurumia hata kidogo huyu kiongozi wa uovu wote, Atamharibu kabisa.
kutoka "Kazi na Kuingia(8)" katika Neno Laonekana katika Mwili
31. Kwa maelfu ya miaka hii imekuwa ni nchi ya uchafu, ni chafu sana, shida zimejaa, mizimu wanazunguka kila kona, wakihadaa na kudanganya, wakitoa tuhuma zisizokuwa na msingi, wasiokuwa na huruma na waovu, wakikandamiza mji huu ulio mahame na kuuacha ukiwa umetapakaa maiti; harufu ya uozo inajaza nchi na kuenea hewani, na unalindwa kwa nguvu sana. Nani awezaye kuuona ulimwengu zaidi ya anga? Shetani anaufunga mwili wote wa mwanadamu, anafumba macho yake yote, na kufunga kinywa chake kwa nguvu. Mfalme wa mashetani amefanya ghasia kwa maelfu kadhaa ya miaka, hadi leo hii, wakati bado anaangalia kwa karibu mji ulio mahame kana kwamba ulikuwa "kasiri la mapepo" lisilopenyeka; kundi hili la walinzi, wakati uo huo, wakiangalia kwa macho yanayong'aa, wakiogopa sana kwamba Mungu Atawakamata bila wao kujua na kuwafutilia wote mbali, Akiwaacha wakiwa hawana sehemu ya "amani na furaha." Inawezekanaje watu wa mji wa mahame kama huu wawe wamewahi kumwona Mungu? Je, wamekwishawahi kufurahia uzuri na upendo wa Mungu? Wanathamini vipi masuala ya ulimwengu wa kibinadamu? Ni nani miongoni mwao anayeweza kuelewa matakwa ya kina ya Mungu? Ni ajabu dogo, basi, kwamba Mungu mwenye mwili abaki kuendelea kuwa Amefichwa: Katika jamii ya giza kama hii, ambapo mashetani hawana huruma na ni makatili, inawezekanaje mfalme wa mashetani anayeua watu kwa kufumba na kufumbua, avumilie uwepo wa Mungu Ambaye ni mwenye upendo, mpole, na mtakatifu? Anawezaje kushangilia na kufurahia ujio wa Mungu? Vikaragosi hawa! Wanalipa upole kwa chuki, wanamtweza Mungu kwa muda mrefu, wanamtukana Mungu, ni washenzi kupita kiasi, hawamjali Mungu hata kidogo, wanapora na kuteka nyara, wamepoteza dhamiri yote, na hawana hata chembe ya wema, na wanawajaribu watu wasiokuwa na hatia na kuwa watu wasiokuwa na uwezo wa kuhisi. Wazazi wa kale? Viongozi Wapendwa? Wote wanampinga Mungu! Udukuzi wao umeacha wote walio chini ya mbingu katika hali ya giza na machafuko! Uhuru wa dini? Haki halali na matakwa ya wananchi? Zote hizo ni njama za kufunika dhambi! Nani ambaye ameikumbatia kazi ya Mungu? Nani ametoa maisha yake au kumwaga damu kwa ajili ya kazi ya Mungu? Kwa kizazi baada ya kizazi, kutoka kwa wazazi hadi watoto, mwanadamu aliyepo katika utumwa bila heshima amemfanya Mungu mtumwa - hii inawezaje kuacha kuamsha hasira? Maelfu ya miaka ya chuki ikiwa imejaa kifuani, milenia ya madhambi imeandikwa katika moyo–inawezekanaje hii isichochee ghadhabu? Kumlipiza Mungu, kuuondoa kabisa uadui wake, usimwache kutangatanga tena, na usimruhusu kufanya fujo zaidi kama anavyotaka! Sasa ni wakati: Mwanadamu ana muda mrefu tangu akusanye nguvu zake zote, amejitolea nguvu zake zote, amelipa kila gharama, kwa hili, kuchana uso uliojificha wa pepo hili na kuwafanya watu, ambao wamepofushwa na kuvumilia kila aina ya mateso na taabu, kuinuka kutoka katika maumivu na kurudi kwa Shetani huyu wa zamani. Kwa nini kuweka kikwazo hicho kisichopenyeka katika kazi ya Mungu? Kwa nini utumie hila mbalimbali kuwadanganya watu wa Mungu? Uhuru wa kweli na haki na matakwa halali vipo wapi? Usawa uko wapi? Faraja iko wapi? Wema upo wapi? Kwa nini kutumia mbinu za hila kuwadanganya watu wa Mungu? Kwa nini kutumia nguvu kukandamiza ujio wa Mungu? Kwa nini asimruhusu Mungu kuzunguka katika dunia ambayo Ameiumba? Kwa nini kumbana Mungu hadi Anakosa sehemu ya kupumzisha kichwa Chake? Wema upo wapi miongoni mwa wanadamu? Ukarimu upo wapi miongoni mwa wanadamu? Kwa nini kusababisha matamanio makubwa kiasi hicho kwa Mungu? Kwa nini kumfanya Mungu kuita tena na tena? Kwa nini kumlazimisha Mungu kumhofia Mwana Wake mpendwa? Kwa nini jamii hii ya giza na mbwa wao walinzi wasimruhusu Mungu kuja bila kizuizi na kuzunguka dunia ambayo Aliiumba? Kwa nini mwanadamu haelewi, mwanadamu anayeishi katika maumivu na mateso? Mungu Amevumilia mateso makubwa kwa ajili yenu, kwa maumivu makubwa Amemtoa Mwanawe wa pekee, mwili wake na damu, kwa ajili yenu, sasa kwa nini bado mnakuwa vipofu? Katika mtazamo mzima wa kila mtu, mnakataa ujio wa Mungu, na mnakataa urafiki wa Mungu. Kwa nini mnakosa busara kiasi hicho? Mko tayari kuvumilia uonevu katika jamii ya giza kama hii? Kwa nini, badala ya kujaza tumbo lenu kwa milenia ya uadui, mnajidanganya wenyewe kwa "kinyesi" cha mfalme wa mashetani?
kutoka "Kazi na Kuingia (8)" katika Neno Laonekana katika Mwili
32. Hatua za kazi ya Mungu duniani zinahusisha shida kubwa: Udhaifu wa mwanadamu, upungufu, utoto, ujinga na kila kitu cha mwanadamu—kila kimoja kimepangwa kwa uangalifu sana na kuangaliwa kwa hadhari sana na Mungu. Mwanadamu ni kama duma wa kutisha ambaye mtu hathubutu kumtega au kumchokoza; anapoguswa tu anauma, au vinginevyo anaanguka chini na kupoteza mwelekeo wake, na ni kana kwamba, akipoteza umakini kidogo tu, anarudia uovu tena, au anampuuza Mungu, au anakimbia kwa baba yake nguruwe au mama yake mbwa kuendeleza mambo machafu ya mwili wao. Ni kizuizi kikubwa kiasi gani! Katika kila hatua ya kazi Yake haswa, Mungu anawekwa katika majaribu, na takribani kila hatua inaleta hatari kubwa. Maneno yake ni ya kweli na ya uaminifu, na bila uovu, lakini nani yupo tayari kuyakubali? Nani yupo tayari kutii kikamilifu? Inavunja moyo wa Mungu. Anafanya kazi usiku na mchana kwa ajili ya mwanadamu, Anasongwa na wasiwasi kuhusu maisha ya mwanadamu na Anauonea huruma udhaifu wa mwanadamu. Amevumilia shida nyingi katika kila hatua ya kazi Yake, kwa kila neno Analozungumza; Yupo katikati ya mwamba na sehemu ngumu, na kufikiria juu ya udhaifu wa mwanadamu, ukaidi, utoto, na vile alivyo hatarini wakati wote....tena na tena. Nani aliyekwishawahi kujua hili? Nani anaweza kuwa na imani? Nani anaweza kufahamu? Anachukia dhambi za wanadamu daima, na ukosefu wa uti wa mgongo, mwanadamu kutokuwa na uti wa mgongo, ndiko kunamfanya kuwa na hofu juu ya hatari aliyonayo mwanadamu, na kutafakari njia zilizopo mbele ya mwanadamu; siku zote, anapoangalia maneno na matendo ya mwanadamu, je, yanamjaza huruma, hasira, na siku zote vitu hivi vinamletea maumivu moyoni Mwake. Hata hivyo, wasio na hatia wamekuwa sugu; kwa nini ni lazima Mungu siku zote afanye vitu kuwa vigumu kwao? Mwanadamu dhaifu, ameondolewa kabisa uvumilivu; kwa nini Mungu Awe na hasira isiyopungua kwa mwanadamu? Mwanadamu dhaifu na asiye na nguvu hana tena uzima hata kidogo; kwa nini Mungu Anamkaripia siku zote kwa ukaidi wake? Nani anayeweza kuhimili matishio ya Mungu mbinguni? Hata hivyo, mwanadamu ni dhaifu, na yupo katika dhiki sana, Mungu Ameisukuma hasira Yake ndani kabisa moyoni Mwake, ili kwamba mwanadamu ajiakisi mwenyewe taratibu. Ilhali mwanadamu, aliyepo katika matatizo makubwa, hazingatii hata kidogo mapenzi ya Mungu; amedondoshwa miguuni na mfalme mzee wa mashetani, na bado haelewi kabisa, siku zote anajiweka dhidi ya Mungu, au si moto wala baridi kwa Mungu. Mungu Amezungumza maneno mengi sana, lakini nani ambaye ameyazingatia? Mwanadamu haelewi maneno ya Mungu, lakini bado hashtuki, bila kuwa na shauku, na hajawahi kuelewa kabisa hulka ya Shetani wa kale. Watu wanaishi Kuzimu, lakini wanaamini wanaishi katika "kasri la chini ya bahari"; wanateswa na joka kuu jekundu, lakini bado wanadhani wanatendewa vyema na nchi ya joka; wanadhihakiwa na Shetani lakini wanadhani wanafurahia ustadi wa hali ya juu wa mwili. Ni chafu kiasi gani, ni mafidhuli kiasi gani! Mwanadamu amekutana na bahati mbaya, lakini haijui, na katika jamii hii ya giza anateseka na ajali baada ya ajali, lakini bado hajazinduka katika hili. Ni lini atakapoachana na wema wake wa kibinafsi na tabia ya mawazo ya kiutumwa? Kwa nini hajali moyo wa Mungu kiasi hicho? Je, anajifanya haoni ukandamizaji na shida hii? Je, hatamani kuwe na siku ambayo atabadilisha giza kuwa nuru? Je, hatamani zaidi kuponya uonevu dhidi ya haki na ukweli? Je, yupo tayari kutazama tu bila kufanya chochote watu wakitupilia mbali ukweli na kupindua ukweli? Je, anafurahia kuendelea kuvumilia matendo haya mabaya? Je, yupo radhi kuwa mtumwa? Je, yupo tayari kuangamia mkononi mwa Mungu pamoja na mali za taifa hili lililoanguka? Azma yako ipo wapi? Malengo yako yapo wapi? Heshima yako ipo wapi? Maadili yako yapo wapi? Uhuru wako upo wapi? Je, upo radhi kutoa maisha yako yote kwa ajili ya joka kuu jekundu, mfalme wa mashetani? Je, unafurahi kumwacha akutese hadi kufa? Kina chake ni vurugu na giza, mtu wa kawaida, anayeteseka na mateso kama hayo, analalamika bila kupumzika. Ni lini mwanadamu ataweza kunyanyua kichwa chake juu? Mwanadamu amekuwa kimbaumbau na amekonda, anawezaje kuridhika na Shetani huyu katili na dikteta? Kwa nini asiyatoe maisha yake kwa Mungu mapema awezavyo? Kwa nini bado anayumbayumba, ni lini atamaliza kazi ya Mungu? Hivyo anaonewa na kunyanyaswa bila sababu yoyote, maisha yake yote hatimaye yatakuwa bure; kwa nini ana haraka hivyo ya kufika, na haraka hiyo ya kuondoka? Kwa nini hahifadhi kitu kizuri cha kumpa Mungu? Je, amesahau milenia ya chuki?
kutoka "Kazi na Kuingia(8)" katika Neno Laonekana katika Mwili
33. Mungu Amefanyika kuwa mwili wakati huu kufanya kazi hii, kukamilisha kazi ambayo bado Hajaikamilisha, kuifunga enzi hii, kuihukumu enzi hii, kuwaokoa waliozama kabisa dhambini kutoka katika ulimwengu wa bahari ya mateso na kuwabadilisha kabisa. Wayahudi walimsulubisha Mungu msalabani, hivyo kuhitimisha "safari za Mungu kwenda Uyahudi." Sio baada ya muda mrefu, Mungu mwenyewe Alikuja kwa wanadamu kwa mara nyingine tena, na kuwasili kimyakimya katika nchi ya joka kuu jekundu. Kimsingi, jumuiya ya kidini ya serikali ya Kiyahudi kwa muda mrefu ilikuwa imetundika picha ya Yesu katika kuta zao, na kwa vinywa vyao watu wakalia "Bwana Yesu Kristo." Hawakujua kwamba Yesu Alikubali zamani sana amri ya Baba Yake kurudi miongoni mwa wanadamu kukamilisha hatua ya pili ya kazi Yake ambayo haijakamilika. Na matokeo yake, watu walipigwa na butwaa walipomwangalia: Alikuwa Amezaliwa katika ulimwengu ambamo enzi nyingi zilikuwa zimepita, na Alionekana miongoni mwa wanadamu kwa umbo la yule ambaye ni wa kawaida kabisa. Kimsingi, kadiri enzi zilivyopita, mavazi Yake na umbo lote vimembadilika, kana kwamba Amezaliwa upya. Watu wangewezaje kujua kuwa ni Bwana Yesu Kristo Yule Aliyeshuka msalabani na Aliyefufuliwa? Hana hata chembe ya jeraha, kama ambavyo Yesu Hakuwa Anafanana na Yehova. Yesu wa leo Ana muda mrefu bila kuvumilia nyakati zilizopita. Watu wangewezaje kumjua? Watu wenye mashaka kama "Tomaso" siku zote wanakuwa na mashaka kuwa ni Yesu Aliyefufuka, siku zote anataka kuona makovu ya misumari katika mikono ya Yesu kabla hajatuliza akili yake; bila kuyaona, siku zote anaweza kusimama katika wingu la mashaka, na anakuwa hana uwezo wa kusimamisha miguu yake katika "nchi ya kweli" na kumfuata Yesu. Maskini "Tomaso"—angewezaje kujua kuwa Yesu Amekuja kufanya kazi Aliyoamriwa na Mungu Baba? Kwa nini Yesu Anataka kuchukua makovu ya msalaba? Je, makovu ya kusulubiwa ni alama za Yesu? Amekuja kufanya kazi kwa ajili ya mapenzi ya Baba Yake; kwa nini Aje Akiwa Amevaa na kupambika kama Myahudi wa miaka elfu kadhaa iliyopita? Je, umbo ambalo Mungu Analichukua katika mwili linaweza kuzuia kazi ya Mungu? Je, hii ni nadharia ya nani? Kwa nini, Mungu Anapofanya kazi, ni lazima iwe kulingana na mitazamo ya mwanadamu? Kitu pekee ambacho Mungu Anapambana kwa ajili yake katika kazi Yake ni ili kazi hiyo iwe na matokeo. Hafuati sheria, na hakuna kanuni katika kazi Yake–mwanadamu angewezaje kuielewa? Ingewezekanaje mitazamo ya binadamu ione kazi yote ya Mungu? Hivyo ni vizuri zaidi kutulia chini vizuri: Msihangaike na mambo madogomadogo, na usichukulie kwa ukubwa mambo ambayo ni mapya kwenu—hii itakuzuia kujitania na watu kukucheka. Umemwamini Mungu kwa miaka yote hii lakini bado humjui Mungu; hatimaye unajitumbukiza katika kuadibu, wewe, ambaye umewekwa katika "kiwango cha juu kabisa," mmejiweka katika madaraja ya walioadibiwa. Ni bora zaidi usitumie mbinu zako za kijanja kuonyesha hila zako; je, mtazamo wako huo finyu unaweza kumwelewa Mungu, Anayetazama kutoka milele hadi milele? Je, uzoefu wako huo wa juujuu unaweza kuelewa kabisa mapenzi ya Mungu? Usiwe na majivuno. Hata hivyo, Mungu sio wa duniani—sasa inawezekanaje kazi Yake iwe kama ulivyotarajia?
kutoka "Kazi na Kuingia(8)" katika Neno Laonekana katika Mwili
34. "Tamaduni za asili "na "mitazamo ya kiakili" madhubuti vimeweka kivuli katika roho safi na ya kitoto ya mwanadamu, vimeshambulia roho ya mwanadamu bila "ubinadamu" hata kidogo kana kwamba anaondolewa hisia na hali yoyote ya nafsi. Mbinu za mashetani hawa ni za kikatili kupita kiasi, na ni kana kwamba "elimu" na "malezi" vimekuwa ni njia za kitamaduni ambazo kwazo mfalme wa mashetani anamchinja mwanadamu; kwa kutumia "mafundisho yake ya kina" anafunika kabisa roho yake mbaya, akivaa mavazi ya kondoo ili kupata imani ya mwanadamu na halafu kusubiri mwanadamu akiwa amelala na kummeza kabisa. Masikini binadamu—wangewezaje kujua kwamba nchi ambayo kwayo wamelelewa ni nchi ya Shetani, kwamba aliyewalea kimsingi ni adui ambaye anawaumiza. Lakini bado mwanadamu hazinduki kabisa; baada ya kushibisha hasira na kiu chake, anajiandaa kulipa "wema" wa wazazi wake kwa kumlea. Hivyo ndivyo mwanadamu alivyo. Leo, bado hajui kwamba "mfalme" ambaye alimlea ni adui yake. Nchi imechafuliwa na mifupa ya wafu, Shetani anafanya wazimu bila kutulia, na anaendelea kumeza mwili wa mwanadamu huko "kuzimu," akishiriki kaburi pamoja na mifupa ya wanadamu na akijaribu waziwazi kuwamaliza masalia wa mwisho wa mwili wa mwanadamu uliobakia matambara. Lakini mwanadamu bado ni mjinga, na hajawahi kumchukuliwa Shetani kama adui yake, lakini badala yake anamtumikia kwa moyo wake wote. Watu kama hao waliokengeuka hawawezi kumjua Mungu. Ni rahisi kwa Mungu kuwa mwili na kuja miongoni mwa wanadamu, Akitekeleza kazi Zake zote za wokovu? Mwanadamu, ambaye tayari amekwishajiingiza Kuzimu, anawezaje kukidhi matakwa ya Mungu?
kutoka "Kazi na Kuingia(9)" katika Neno Laonekana katika Mwili
35. Mungu Amevumilia sana kulala bila kupata usingizi kwa ajili ya kazi ya binadamu. Kutoka vina vya juu hadi vya chini, Amepanda kwenda katika kuzimu ambapo mwanadamu anaishi kupitisha siku Zake na mwanadamu, hajawahi kulalamikia uchakavu walionao wanadamu, hajawahi kumlaumu kwa ukaidi wake, lakini Anavumilia mateso makuu kadri Anavyofanya kazi Yake. Inawezekanaje Mungu Awe wa kuzimu? Inawezekanaje Aishi maisha yake kuzimu? Lakini kwa ajili ya binadamu wote, ili binadamu wote waweze kupata pumziko mapema zaidi, Amestahimili fedheha na kupitia udhalimu kuja duniani, na Aliingia mwenyewe “jahanamu” na “kuzimu,” katika tundu la duma, kumwokoa mwanadamu. Mwanadamu amefuzu vipi kumpinga Mungu? Ana sababu gani tena ya kumlaumu Mungu? Anawezaje kuwa na ujasiri wa kumwangalia Mungu tena? Mungu wa mbinguni Amekuja katika nchi hii chafu zaidi ya uovu, na Hajawahi kutangaza manung'uniko au kulalamika kuhusu mwanadamu, lakini badala yake Anakubali kimyakimya unyang'anyi na ukandamizaji wa mwanadamu. Kamwe Hajawahi kujibu matakwa ya mwanadamu yasiyokuwa na msingi, hajawahi kutaka mambo mengi yanayomuelemea mwanadamu, na hajawahi kumwekea mwanadamu matakwa yasiyokuwa na msingi; Anafanya tu kazi ambazo mwanadamu alitakiwa kufanya bila malalamiko: kufundisha, kutia mwanga, kukaripia, usafishaji wa maneno, kukumbusha, kusihi, kufariji, kuhukumu na kufunua. Ni hatua gani Alizozichukua ambazo sio kwa ajili ya maisha ya mwanadamu? Ingawa Ameondoa matarajio na majaliwa ya mwanadamu, ni hatua zipi zilizochukuliwa na Mungu ambazo hazikuwa kwa ajili ya majaliwa ya mwanadamu? Ni ipi kati ya hatua hizo ambayo haijawahi kuwa kwa ajili ya mwanadamu kuendelea kuishi? Ni ipi kati ya hatua hizo haikuwepo kwa ajili ya kumweka mwanadamu huru dhidi ya mateso na minyanyaso ya nguvu za giza ambazo ni nyeusi kama usiku? Ni ipi kati ya hatua hizo si kwa ajili ya mwanadamu? Ni nani awezaye kuujua moyo wa Mungu, ambao ni sawa na mama mwenye mapenzi? Ni nani awezaye kuujua moyo wa Mungu wenye shauku? Moyo wa upendo na matarajio ya shauku ya Mungu vimelipwa kwa mioyo ya baridi, na usugu, na macho yanayoonyesha kutojali, kwa makaripio ya kujirudia na matusi ya mwanadamu, kwa maneno ya mkato na dhihaka na udhalilishaji, vimelipwa kwa dhihaka ya mwanadamu, kwa kukanyagwa na kukataliwa, kwa kutokuwa na ufahamu, na kupiga kite, na farakano, na uepukaji, kwa uongo, mashambulizi na ukali. Maneno ya wema ya Mungu yamekutana na nyusi kali na ufidhuli wa vidole elfu moja vinavyotikisika. Mungu Anaweza kustahimili, Akiwa Ameinamisha kichwa, Akiwahudumia watu kama dume la ng'ombe lililo hiari kufungwa. Ni idadi gani ya miezi na jua, ni mara ngapi Amekabiliana na nyota, ni mara ngapi Ameondoka alfajiri na kurudi jioni, na kurushwarushwa na kugeuzwa, Akivumilia maumivu makubwa mara elfu moja kuliko maumivu Aliyoyapata Alipokuwa Anaondoka kutoka kwa Baba Yake, Akivumilia mashambulizi na "kuvunja" kwa mwanadamu, na "kumshughulikia" na "kumpogoa" mwanadamu. Unyenyekevu wa Mungu na kujishusha vimelipwa kwa kiburi cha mwanadamu, kwa mitazamo na vitendo vya mwanadamu visivyokuwa vya haki, na kutojulikana Kwake, ustahimilivu, na uvumilivu vimelipizwa kwa jicho la tamaa la mwanadamu, mwanadamu hujaribu kumkanyaga Mungu hadi afe, bila majuto, na anajaribu kumkanyagia Mungu ardhini. Mtazamo wa mwanadamu katika vile anavyomtendea Mungu ni wa "ujanja adimu," na Mungu ambaye Anachokozwa na kutwezwa na mwanadamu, Anakanyagwa na kuwa bapa kwa miguu ya makumi elfu ya watu wakati mwanadamu mwenyewe anasimama juu kabisa, kana kwamba angeweza kuwa "mfalme wa kasri," kana kwamba anataka kuchukua "mamlaka kamili," "kuendesha mahakama akiwa nyuma ya skrini," kumfanya Mungu kuwa makini na mwenye kanuni "mwongozaji nyuma ya matukio," ambaye haruhusiwi kupigana au kusababisha shida; Mungu ni lazima afanye sehemu ya "Mtawala wa Mwisho," ni lazima Awe "kibaraka," bila uhuru wote. Matendo ya mwanadamu hayaongeleki, sasa ana sifa gani ya kutaka hili au kile kuhusu Mungu? Ana sifa gani ya kutoa mapendekezo kwa Mungu? Anafaa kwa kiasi gani kumtaka Mungu amhurumie juu ya udhaifu wake? Anafaa kwa kiasi gani kupokea huruma ya Mungu? Anafaa kwa kiasi gani kupokea ukarimu wa Mungu kila mara? Anafaa kwa kiasi gani kupokea msamaha wa Mungu kila mara? Dhamiri yake ipo wapi? Alivunja moyo wa Mungu muda mrefu uliopita, ni muda mrefu toka ameuacha moyo wa Mungu katika vipande. Mungu Alikuja miongoni mwa wanadamu Akiwa na nguvu nyingi na mwenye shauku kubwa, Akitegemea kwamba mwanadamu atakuwa mkarimu Kwake, hata kama ni kwa wema mdogo tu. Bado moyo wa Mungu haujafarijiwa na mwanadamu, yote Aliyopokea ni mashambulizi ya kuongezeka haraka na mateso; moyo wa mwanadamu ni wenye tamaa sana, tamaa yake ni kubwa sana, hawezi akatosheka, siku zote ni mwenye fitina na jasiri pasi busara, hawezi kamwe kumpatia Mungu uhuru au haki ya kuzungumza, na anamwacha Mungu bila cha kufanya bali kukubali unyanyasaji, na kumruhusu mwanadamu kumtawala vyovyote anavyotaka.
kutoka "Kazi na Kuingia(9)" katika Neno Laonekana katika Mwili
36. Tangu uumbaji hadi leo, Mungu Amestahimili maumivu mengi sana, na kupata mashambulizi mengi sana. Ilhali hata leo, bado mwanadamu hayalegezi matakwa yake kwa Mungu kwa urahisi, bado anamchunguza Mungu, bado hana uvumilivu Naye, na anachofanya ni kumpatia "ushauri," na "kumkosoa," na “kumfundisha nidhamu" kana kwamba Mungu Atapotoka njia, kwamba Mungu duniani ni hayawani na Hana busara, au Atafanya fujo, au kwamba Hatafanya kitu chochote cha maana. Mwanadamu siku zote huwa na mtazamo wa aina hii kwa Mungu. Inawezekanaje isimhuzunishe Mungu? Kwa kuwa mwili, Mungu Amevumilia maumivu na mateso mengi; ni vibaya kiasi gani, kumfanya Mungu Akubali mafundisho ya mwanadamu? Kuwasili kwake miongoni mwa wanadamu kumemvua uhuru wote, kama vile Amefungwa Kuzimu, na Amekubali "uchunguzi" wa mwanadamu bila upinzani hata kidogo. Hii sio aibu? Katika kuja miongoni mwa familia ya wanadamu wa kawaida, Yesu Amepitia uonevu mkubwa. Na kinachoumiza zaidi ni kwamba Amekuja katika ulimwengu huu wa vumbi na kujinyenyekeza Mwenyewe katika hadhi ya chini kabisa, na Amechukua mwili wa kawaida kabisa. Kwa binadamu kuwa mwembamba, je, Mungu Mwenyezi Hapati shida? Je, na hii yote si kwa ajili ya binadamu? Kuna wakati wowote ambapo alikuwa Anajifikiria Mwenyewe? Baada ya kukataliwa na kuuawa na Wayahudi, na kukejeliwa na kudhihakiwa na watu, Hajawahi kulalamika mbinguni au kupinga duniani. Leo, janga hili lenye umri wa milenia limetokea tena miongoni mwa watu hawa wanaofanana na Wayahudi. Je, hawafanyi dhambi ile ile? Nini kinamfanya mwanadamu kuwa na sifa ya kupokea ahadi za Mungu? Je, hampingi Mungu na kisha kukubali baraka Zake? Kwa nini haifikii haki, au kutafuta ukweli? Kwa nini havutiwi na kile ambacho Mungu Anafanya? Haki yake ipo wapi? Usawa wake upo wapi? Je, ana ujasiri wa kumwakilisha Mungu? Zipo wapi fahamu zake za haki? Ni kiasi gani ambacho kile kinachopendwa na mwanadamu ndicho kile kinachopendwa na Mungu? Mwanadamu hawezi kutofautisha kati ya chaki na jibini, siku zote anachanganya kati ya nyeusi na nyeupe, anakandamiza haki na ukweli, na anashikilia kutokuwa na haki wala usawa kwa kiwango kikubwa. Anafukuzia mbali mwanga na anarukaruka gizani. Wale wanaotafuta ukweli na haki badala yake wanafukuzia mbali mwanga, wale wanaomtafuta Mungu wanamkanyaga kwa miguu yao, na wanajipandisha angani. Mwanadamu hana tofauti na gaidi. Sababu yake ipo wapi? Nani anayeweza kutofautisha kati ya jema na baya? Nani anayeweza kushikilia haki? Nani ambaye yupo tayari kuteseka kwa ajili ya kweli? Watu ni waovu na wana tabia za kishetani kabisa! Baada ya kumwangika Mungu msalabani wanapiga makofi na kufurahi, vilio vyao havikomi. Wapo kama kuku na mbwa, wanashirikiana na kula njama, wameanzisha ufalme wao, udukuzi wao haujaachwa bila kusumbuliwa, wanafumba macho yao na kulia kwa maumivu makali zaidi na zaidi, wote wameungana pamoja, na hali ya kututumka imeenea kote, ni harakaharaka na hai, na wale ambao wanajishikamanisha kwa wengine kiupofu wanazidi kuibuka, wote wakiwa wameshikilia majina "mashuhuri" ya mababu zao. Hawa mbwa na kuku wamemweka Mungu mbali na akili zao, na hawajawahi kuzingatia kabisa hali ya moyo wa Mungu. Ni ajabu kidogo kwamba Mungu Anasema mwanadamu ni kama mbwa au kuku, mbwa anayebweka anayewafanya mia wengine kutoa mlio mkali; kwa nia hii, kwa makelele mengi ameileta kazi ya Mungu katika siku ya leo, bila kujali kazi ya Mungu ni ya namna gani, bila kujali kuna haki, bila kujali Mungu Ana nafasi Yake ya kuweka miguu Yake, bila kujali kesho itakuwaje, uduni wake, na hali yake ya kuwa mchafu. Mwanadamu hajawahi kufikiria juu ya mambo kiasi hicho, hajawahi kuhofia kesho, na amekusanya yale yote ambayo ni ya manufaa na ya thamani na kuyakumbatia, na bila kumwachia Mungu chochote isipokuwa mabaki. Binadamu ni katili kiasi gani! Hawi na hisia hata kidogo juu ya Mungu, na baada ya kuteketeza kila kitu cha Mungu, anamrusha Mungu nyuma yake na kuacha kujali kabisa kuhusu uwepo wake. Anamfurahia Mungu, halafu anampinga Mungu, na anamkanyagia chini ya miguu yake, wakati mdomoni mwake anamshukuru na kumsifu Mungu; anamwomba Mungu, na anamtegemea Mungu, wakati huo pia anamdanganya Mungu; "analiinua" jina Mungu, na kuutazama uso wa Mungu, halafu pia bila haya na bila kuwa na aibu anakaa katika kiti cha enzi cha Mungu na "kuhukumu" "udhalimu" wa Mungu; kutoka katika kinywa chake yanatoka maneno haya "anapaswa kumshukuru Mungu," na anatazama katika maneno ya Mungu, halafu katika moyo wake anavurumisha shutuma kwa Mungu; ni "mvumilivu" kwa Mungu halafu anamkandamiza Mungu, na kinywa chake kinasema ni "kwa ajili ya Mungu"; mikononi mwake ameshikilia vitu vya Mungu, na kinywani mwake anatafuna chakula ambacho Mungu Amempatia, bado macho yake yanamtazama Mungu yakiwa hayana hisia kabisa, kana kwamba anatamani kummeza; anautazama ukweli lakini anasisitiza kuwa ni hila za Shetani; anatazama haki lakini analazimisha iwe kujikana nafsi; anatazama matendo ya mwanadamu lakini anasisitiza kuwa ni kile Mungu Alicho ; anatazama karama za asili za mwanadamu lakini anasisitiza kuwa ni ukweli; anatazama matendo ya Mungu lakini anasisitiza kuwa ni kiburi na majivuno, majigambo na haki binafsi; mwanadamu anapomwangalia Mungu anasisitiza kumpachika uanadamu, na anajitahidi sana kumweka katika kiti cha kiumbe aliyeumbwa akishirikiana na Shetani; anajua kweli kabisa ni matamshi ya Mungu, bado atasema si kitu chochote zaidi ya maandiko ya mwanadamu; anajua kabisa kwamba Roho anatambulika katika mwili, Mungu anakuwa mwili, lakini anasema mwili huu ni uzao wa Shetani; anajua kikamilifu kuwa Mungu ni mnyenyekevu na hajionyeshi, lakini anasema kwamba Shetani ameaibishwa na Mungu Ameshinda. Uzuri wa bure ulioje! Mwanadamu hata hafai kuwa mbwa mlinzi! Hawezi kutofautisha kati ya nyeusi na nyeupe, na hata anachanganya kwa makusudi nyeusi ndani ya nyeupe. Je, nguvu za mwanadamu na husuru ya mwanadamu vinaweza kustahimili siku ya ukombozi wa Mungu? Baada ya kumpinga Mungu kwa kukusudia, mwanadamu hakuweza kujali sana, au hata kwenda mbali sana na kumuua, asimpatie Mungu nafasi ya kujionyesha Mwenyewe. Haki iko wapi? Upendo uko wapi? Anakaa kando ya Mungu na kumsukuma Mungu Apige magoti ili Aombe msamaha, kutii mipango yake yote, kuridhia hila zake zote, na anamfanya Mungu kuchukua ishara Zake zote kutoka kwake, la sivyo anaghadhabishwa na kuwakwa na hasira. Inawezekanaje Mungu Asiwe na maumivu katika ushawishi huo wa giza, ambao unachanganya nyeusi kuwa nyeupe? Angewezaje kukosa kuwa na wasiwasi? Kwa nini inasemwa kwamba Mungu Alipoanza kazi yake ya hivi karibuni kabisa, ilikuwa kama alfajiri ya mwanzo mpya? Matendo ya mwanadamu "yana utajiri," ni "chemchemi isiyokoma ya maji ya uzima" bila kukoma "yanajaza tena" shamba la moyo wa mwanadamu, wakati "chemchemi isiyokoma ya maji ya uzima" ya mwanadamu "inashindana" na Mungu bila haya; wawili hawa hawapatani, na anawapa watu vitu kwa niaba ya Mungu bila kuacha chochote, wakati mwanadamu anashirikiana naye bila kujali hatari iliyopo. Na kwa athari gani? Anamtupilia mbali Mungu katika upande mmoja, na kumweka mbali sana, ambapo watu hawatamzingatia, wakiogopa sana kwamba Atavuta usikivu wao, na anaogopa sana kwamba chemchemi isiyokoma ya maji ya uzima ya Mungu itamteka mwanadamu, na kumpata mwanadamu. Hivyo, baada ya kupitia uzoefu wa miaka mingi wa masuala ya kidunia, anakula njama dhidi ya Mungu, na hata anamfanya Mungu kuwa mlengwa wa "adhabu." Ni kana kwamba Mungu Amekuwa gogo machoni mwake, na anatamani kumnyakua Mungu na kumweka motoni ili Atakaswe na kusafishwa. Mwanadamu anapoona mahangaiko ya Mungu, anapiga kifua chake na kucheka, anacheza kwa furaha, na kusema kwamba Mungu pia Amewekwa motoni, na anasema kwamba atausafisha uchafu wa Mungu, kana kwamba hii ni ya kiurazini na ina maana, kana kwamba hizi tu ndio njia za haki na zenye mantiki za Mbinguni. Tabia hii ya fujo ya mwanadamu inaonekana kuwa ni ya makusudi na ya kutofahamu. Mwanadamu anafichua uso wake mbaya na roho yake mbaya, vilevile sura ya kusikitisha ya ombaomba; baada ya kufanya ghasia sana, anavaa sura ya kuhurumiwa na kuomba msamaha wa Mbingu, akifanana na udongo wa kufinyangwa. Mwanadamu siku zote hutenda kwa namna asivyotarajiwa, siku zote "anamwendesha duma kuwatisha wengine," anajiunga katika michezo vyovyote anavyoweza, hajali hata kidogo moyo wa Mungu, wala halinganishi hadhi yake mwenyewe. Kimyakimya anampinga Mungu, kana kwamba Mungu Amemkosea, na Hapaswi kumtendea hivyo, na kana kwamba Mbingu haina macho na inafanya kwa makusudi vitu kuwa vigumu kwake. Hivyo mwanadamu anapanga njama za siri, na hajali matakwa ya Mungu hata kidogo, anatazama kwa macho ya mnyama mkali, anatazama kwa hasira kila kitu Anachokifanya Mungu, hafikirii kwamba yeye ni adui ya Mungu, na ana matumaini kwamba siku itakuja ambapo Mungu Atatawanya umande na kuviweka vitu wazi, na kumwokoa kutoka katika "kinywa cha duma" na kulipiza kisasa kwa niaba yake. Hata leo, watu bado hawafikiri kwamba wanatekeleza jukumu la kumpinga Mungu, jukumu ambalo limefanywa kwa enzi nyingi sana, wangewezaje kujua kwamba, katika yote wanayofanya, wamepotoka toka muda mrefu sana, kwamba yote waliyoyaelewa yamemezwa na bahari zamani sana.
Ni nani ambaye amekubali ukweli? Ni nani ambaye amemkaribisha Mungu kwa mikono yote? Nani ambaye amewahi kutamani uwepo wa Mungu? Tabia ya mwanadamu imeoza toka muda mrefu sana, na unajisi wake umefanya hekalu la Mungu lisitambulike toka zamani sana. Mwanadamu, wakati akiendelea kufanya kazi yake, amekuwa akimdharau Mungu. Ni kana kwamba upinzani wake kwa Mungu umeandikwa kwenye jiwe, na haubadiliki, na matokeo yake ni bora alaaniwe kuliko kuendelea kuteseka "kwa kufanyiwa vibaya" na maneno na matendo yake. Inakuwaje watu kama hawa wamjue Mungu? Wanawezaje kupata pumziko kwa Mungu? Na wanawezaje kufaa kuja mbele za Mungu?
kutoka "Kazi na Kuingia(9)" katika Neno Laonekana katika Mwili
37. Nimetumia siku nyingi nikiwa na mwanadamu, Nimeishi duniani pamoja na mwanadamu, na Sijawahi kutaka vitu zaidi kutoka kwa mwanadamu, Ninamwongoza tu mwanadamu kusonga mbele, Sifanyi chochote bali kumwongoza mwanadamu, na kwa ajili ya hatima ya binadamu, bila kuchoka Nafanya kazi ya kupangilia. Nani ambaye amewahi kuelewa mapenzi ya Baba wa mbinguni? Nani amekwishasafiri kati ya mbingu na dunia? Sitamani kuishi tena na mwanadamu katika "uzee" wake , kwani mwanadamu ni "wa mtindo wa zamani sana," hajui chochote, kitu pekee anachojua ni kula na kuvimbiwa kwenye sherehe Niliyoiandaa, amejitenga na yote—hafikirii suala jingine lolote lile. Binadamu anateseka sana, makelele, huzuni, na hatari miongoni mwa wanadamu ni kubwa sana, na hivyo Natamani nisiwashirikishe matunda ya thamani ya kupata ushindi wakati wa siku za mwisho. Acha mwanadamu afurahie baraka tele ambazo ametengeneza yeye mwenyewe, maana mwanadamu hanikaribishi–kwa nini Nimlazimishe binadamu kulazimisha tabasamu? Kila kona ya dunia haina joto, hakuna hata chembe ya chemchemi katika ardhi yote ya nchi, maana, kama vile mnyama aishiye majini hana joto hata kidogo, ni kama maiti, na hata damu inayopita katika mishipa yake ni kama barafu iliyoganda inayofanya moyo kuwa baridi. Wema upo wapi? Mwanadamu alimsulubisha Mungu msalabani bila sababu yoyote, na baadaye hakuhisi wasiwasi wowote. Hakuna hata mmoja aliyekuwa na majuto, na madikteta hawa makatili bado wanapanga "kumkamata Akiwa hai" Mwana wa Adamu kwa mara nyingine tena na kumleta mbele ya kikosi cha kufyatua risasi, kukomesha chuki ndani ya mioyo yao. Kuna faida gani Kwangu, kubaki katika nchi hii ya hatari? Ikiwa Nitabaki, kitu pekee Nitakachomletea mwanadamu ni mgogoro na fujo, na hakutakuwa na mwisho wa shida, maana Sijawahi kumpatia mwanadamu amani, ni vita tu. Siku za mwisho za binadamu lazima zijae vita, na hatima ya mwanadamu lazima ipinduliwe katikati ya vurugu na migogoro. Na Sipo tayari kushiriki katika "furaha" ya vita, sitaunga mkono umwagaji wa damu na mwanadamu kujitoa mhanga, maana kukataliwa na mwanadamu kumenipeleka katika hali ya kukata tamaa, na Sina moyo wa kuangalia vita vya mwanadamu—hebu mwanadamu apigane kuuridhisha moyo wake, Natamani kupumzika, Nataka kulala, acha mapepo wawe washirika wa binadamu wakati wa siku zao za mwisho! Nani ajuaye mapenzi Yangu? Kwa sababu sijakaribishwa na mwanadamu, na hajawahi kunisubiri, Ninaweza tu kumuaga, na kumkabidhi hatima yake, na kumwachia mwanadamu utajiri Wangu wote, na kupanda maisha Yangu ndani yake, kupanda mbegu ya maisha Yangu ndani ya shamba la moyo wa mwanadamu, na kumwachia kumbukumbu za milele, Ninaweza kuacha tu upendo Wangu wote kwa binadamu, kumwachia yote ambayo mwanadamu anafurahia Kwangu, kama zawadi ya upendo ambayo kwayo tunaitamani kwa kila mmoja. Ningependa tupendane milele, kwamba jana yetu iwe kitu kizuri sana tunachopeana, maana Nimejitoa kikamilifu kwa binadamu–ni malalamiko gani ambayo mwanadamu anaweza kuwa nayo? Tayari Nimeyaacha maisha Yangu yote kwa mwanadamu, na bila neno lolote, Nimetokwa jasho kulima "ardhi nzuri ya upendo" kwa ajili ya binadamu; Sijafanya matakwa yoyote linganifu kwa mwanadamu, na Sijafanya chochote isipokuwa kujitiisha katika mipangilio ya mwanadamu na kutengeneza kesho nzuri zaidi ya binadamu.
kutoka "Kazi na Kuingia(10)" katika Neno Laonekana katika Mwili
38. Hali ya Mungu kupata mwili imetuma mawimbi mazito katika vikundi na madhehebu yote, "imeparaganya" mpangilio wao wa awali, na imetikisa mioyo ya wale wanaotamani sana kujitokeza kwa Mungu. Ni nani asiyeabudu? Nani hatamani kumwona Mungu? Mungu Amekuwa miongoni mwa wanadamu kwa miaka mingi sana, lakini mwanadamu kamwe hajawahi kutambua. Leo, Mungu mwenyewe Amejitokeza, na Ameonyesha utambulisho Wake kwa watu—inawezekanaje hii isiupatie moyo wa mwanadamu furaha? Mungu Aliwahi kushiriki furaha na huzuni pamoja na mwanadamu, na leo Ameunganika tena na mwanadamu, na kushiriki visa vya muda uliopita pamoja naye. Baada ya kutoka Uyahudi, watu hawakuweza kupata alama Yake yoyote. Wanatamani kukutana tena na Mungu, bila kujua kwamba leo wamekutana Naye tena, na kuungana Naye tena. Inawezekanaje hii isiamshe mawazo ya jana? Siku kama ya leo miaka elfu mbili iliyopita, Simon wa Yona, uzao wa Wayahudi, alimtazama Yesu Mwokozi, alikula meza moja pamoja Naye, na baada ya kumfuata kwa miaka mingi alihisi kumpenda sana: Alimpenda sana kutoka moyoni mwake, alimpenda sana Bwana Yesu. Watu wa Uyahudi hawakujua chochote juu ya jinsi mtoto huyu mwenye nywele za dhahabu, Aliyezaliwa katika hori la ng'ombe, Alikuwa ni sura ya kwanza ya Mungu kupata mwili. Wote walidhani kwamba Alikuwa ni mmoja wao, hakuna aliyedhani kwamba Yupo tofauti nao—watu wangewezaje kumtambua Yesu wa kawaida kabisa? Watu wa Uyahudi walidhani kwamba alikuwa ni mtoto wa Kiyahudi wa wakati huo. Hakuna aliyemtazama kama Mungu mwenye upendo, na watu hawakufanya chochote isipokuwa kufanya maombi bila kutambua, wakiomba Awape neema nyingi na maradufu, na amani, na furaha. Walijua tu kwamba, kama milionea, Alikuwa na kila kitu ambacho mtu angetamani kuwa nacho. Lakini watu hawakumchukulia kama mtu ambaye Alikuwa mpendwa; watu wa wakati huo hawakumpenda, na walimpinga tu, na walifanya maombi kwake yasiyokuwa na mantiki, na Hakuwahi kupinga, Aliendelea kutoa neema kwa mwanadamu, ingawa mwanadamu hakumjua. Hakufanya chochote isipokuwa kwa kimya kumpatia mwanadamu wema, upendo, na huruma, na zaidi, Alimpatia mwanadamu njia mpya ya kutenda, kumwongoza mwanadamu kutoka katika vifungo vya sheria. Mwanadamu hakumpenda, alimhusudu tu na kutambua "talanta Zake za kipekee." Inawezekanaje mwanadamu kipofu kujua jinsi ambavyo Yesu Mwokozi Alipitia mateso makubwa Alipokuja miongoni mwa wanadamu? Hakuna aliyejali shida Zake, hakuna mtu aliyejua upendo Wake kwa Mungu Baba, na hakuna ambaye angejua upweke Wake; ingawa Maria alikuwa mama Yake wa kumzaa, angewezaje kujua mawazo yaliyopo moyoni mwa Bwana Yesu mwenye huruma? Nani alijua mateso yasiyoweza kuzungumzika Aliyoyapitia Mwana wa Adamu? Baada ya kumwomba watu wa kipindi hicho walimweka nyuma ya akili zao, na kumtupa nje Akizungukazunguka mitaani, siku baada ya siku, mwaka baada ya mwaka, na kwenda bila mwelekeo kwa miaka mingi hadi Alipofikisha miaka thelathini na mitatu, miaka ambayo ilikuwa mirefu pia mifupi. Watu walipomhitaji, walimwalika nyumbani mwao wakiwa na nyuso za tabasamu, wakijaribu kumwomba kitu—na baada ya kuwa Ametoa mchango wake kwao, walimsukuma mara moja nje ya mlango. Watu walikula kile Alichokitoa mdomoni Mwake, walikunywa damu Yake, walifurahia neema Alizowapatia, lakini bado walimpinga, maana hawakujua nani aliwapa uhai walionao. Hatimaye, walimsulubisha msalabani, lakini bado Hakutoa hata sauti. Hata leo, bado Anabakia kimya. Watu wanakula mwili wake, wanakula chakula Anachowatengenezea, wanapita njia ambayo Ameifungua kwa ajili yao, na wanakunywa damu Yake, lakini bado wanakusudia kumkataa, kimsingi wanamchukulia Mungu ambaye Amewapatia maisha yao kama adui, na badala yake wanawachukulia wale ambao ni watumwa kama wao kama Anavyofanya Baba wa mbinguni. Katika hili, je, hawampingi kwa makusudi? Yesu Aliwezaje kufa msalabani? Je, mnajua? Je, Hakusalitiwa na Yuda, ambaye alikuwa karibu kabisa Naye, na akamla, akamnywa, na akamfurahia? Je, sababu ya usaliti wa Yuda haikuwa ni kwa sababu Yesu hakuwa kitu chochote isipokuwa mwalimu mdogo wa kawaida? Ikiwa watu walikuwa wameona kwamba Yesu Alikuwa si wa kawaida kabisa, na Ambaye Alitoka mbinguni, wangewezaje kumsulubisha msalabani Akiwa hai kwa masaa ishirini na nne, hadi Alipoishiwa na pumzi yote katika mwili wake? Nani awezaye kumjua Mungu? Watu hawafanyi chochote isipokuwa kumfurahia Mungu kwa tamaa isiyotosheka, lakini hawajawahi kumjua. Walipewa inchi na wamechukua maili, na wanamfanya Yesu kutii kabisa amri zao, na maelekezo yao. Ni nani ambaye ameonyesha huruma kwa Mwana wa Adamu huyu, Ambaye hana mahali pa kuweka kichwa Chake? Ni nani ambaye amewahi kufikiria kuunganisha nguvu pamoja Naye kukamilisha agizo la Mungu Baba? Ni nani ambaye amewahi kumwaza? Ni nani mbaye amewahi kuyajali matatizo Yake? Bila upendo hata kidogo, mwanadamu anamvuta nyuma na mbele; mwanadamu hajui nuru na uhai wake unatoka wapi, na hafanyi chochote isipokuwa kupanga kwa siri jinsi ya kumsulubisha tena Yesu wa miaka elfu mbili iliyopita, nani ambaye amepitia uzoefu wa maumivu miongoni mwa wanadamu. Je, Yesu Anawatia watu moyo kuwa na chuki ya namna hiyo? Je, yote Aliyoyafanya yamesahaulika zamani? Chuki ambayo ilichanganyika kwa maelfu ya miaka itaibuka tena juu. Nyinyi vifaranga wa Wayahudi! Ni lini Yesu Amekuwa adui kwenu, hadi mmchukie kiasi hicho? Amefanya mengi na kuzungumza mengi—je hakuna chochote chenye manufaa kwenu? Ameyatoa maisha Yake kwenu bila kuomba kurudishiwa kitu chochote, Amejitoa mzima kwenu—kweli bado mnataka kumla Akiwa mzima? Amejitoa kwenu kikamilifu bila kuacha kitu chochote, bila kufurahia utukufu wa kidunia, wema miongoni mwa wanadamu, na upendo miongoni mwa wanadamu, au baraka zote miongoni mwa wanadamu. Watu ni wabinafsi sana Kwake, hajawahi kufurahia utajiri wote wa duniani, Amejitoa kikamilifu, moyo wa upendo wa dhati kwa mwanadamu, Amejirithisha Yeye mzima kwa mwanadamu—ni nani ambaye amemfanyia wema? Ni nani aliyewahi kumpatia faraja? Mwanadamu amemjazia mashinikizo yote, balaa yote amempatia Yeye, shida zote mbaya Alizozipitia ni mwanadamu amempatia Yeye, anamtupia lawama kwa uonevu wote, na Amezikubali kimyakimya. Je, Amewahi kumpinga mtu yeyote? Je, Amewahi kuomba fidia hata ndogo kutoka kwa mtu yeyote yule? Ni nani amewahi kuonyesha huruma yoyote Kwake? Kama watu wa kawaida, ni nani miongoni mwenu ambaye hajawahi kuwa na kipindi cha utotoni chenye mapenzi ya dhati? Ni nani ambaye hajawahi kuwa na ujana wa kupendeza? Ni nani ambaye hana joto la wapendwa? Ni nani ambaye hana upendo wa rafiki wa karibu? Ni nani ambaye haheshimiwi na wengine? Ni nani ambaye hana familia yenye upendo? Ni nani ambaye hana faraja ya wandani wao? Je, Amekwishawahi kufurahia moja ya haya? Ni nani ambaye amewahi kumtendea wema hata kidogo? Ni nani ambaye amekwishawahi kumpatia faraja hata kidogo? Ni nani ambaye amekwishawahi kumwonyesha angalau hata maadili kidogo ya kibinadamu? Ni nani ambaye amewahi kuwa mvumilivu Kwake? Ni nani ambaye amewahi kuwa pamoja naye katika nyakati za shida? Ni nani ambaye amewahi kupitia maisha ya shida pamoja Naye? Mwanadamu bado hajaacha kumwomba Yeye; anapeleka tu maombi kwake bila hata haya, kana kwamba kuja katika ulimwengu wa mwanadamu, Alipaswa kuwa ng'ombe au farasi wake, na alipaswa kumpatia mwanadamu kila kitu chake; Asipofanya hivyo, mwanadamu hatamsamehe, hatamtendea vizuri, hatamwita Mungu, na hatamheshimu kwa kiwango cha juu. Mwanadamu ni katili sana katika mtazamo wake kwa Mungu, kana kwamba amewekwa ili kutesa Mungu hadi kifo, ni baada ya hapo tu ndipo anapunguza maombi yake kwa Mungu; kama sivyo, mwanadamu hatapunguza kiwango cha matakwa yake kwa Mungu. Inawezekanaje mwanadamu kama huyu asidharauliwe na Mungu? Je, hili si janga la siku hizi? Dhamiri ya mwanadamu haionekani popote. Anasema tu atalipa upendo wa Mungu, lakini anamchanachana Mungu na kumtesa hadi kifo. Je, hii sio "mbinu ya siri" kwa imani yake kwa Mungu, iliyorithishwa kutoka kwa mababu zake? Hakuna mahali ambapo huwezi kuwakuta "Wayahudi," na leo bado wanafanya kazi ile ile, bado wanafanya kazi ile ile ya kumpinga Mungu, na bado wanaamini kwamba wanamwinua Mungu juu? Inawezekanaje macho ya mwanadamu yamjue Mungu? Inawezekanaje mwanadamu, anayeishi katika mwili, kumchukulia Mungu kama Mungu mwenye mwili ambaye Amekuja kutoka katika Roho? Ni nani miongoni mwa wanadamu anaweza kumjua? Ukweli upo wapi miongoni mwa wanadamu? Haki ya kweli ipo wapi? Ni nani anayeweza kuijua tabia ya Mungu? Ni nani anayeweza kushindana na Mungu mbinguni? Haishangazi kwamba, Alipokuwa miongoni mwa wanadamu, hakuna aliyemjua Mungu, na amekataliwa. Inawezekanaje mwanadamu kuvumilia uwepo wa Mungu? Anawezaje kuvumilia kuruhusu mwanga kuondosha giza la ulimwengu? Je, hii yote si kujitoa kwa heshima kwa mwanadamu? Je, huku sio kuingia adilifu kwa mwanadamu? Je, kazi ya Mungu haijajikita katika kuingia kwa mwanadamu? Ningependa muunganishe kazi ya Mungu na kuingia kwa mwanadamu, na kurekebisha uhusiano kati ya mwanadamu na Mungu, na kufanya majukumu ambayo yanapaswa kufanywa na mwanadamu kwa uwezo wake wote. Kwa njia hii, kazi ya Mungu hatimaye itafikia mwisho, ikiwa ni pamoja na utukufu Wake!
kutoka "Kazi na Kuingia (10)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Tanbihi:
a. Matini asilia inasomeka "Baadhi hata wanapiga makelele."
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili
Chanzo: Kanisa la Mwenyezi Mungu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni