4.19.2018

Umeme wa Mashariki | "Mji Utaangushwa" (1) - Ulimwengu wa Dini Umepotoka na kuwa Mji wa Babeli

Umeme wa Mashariki | "Mji Utaangushwa" (2) - Mbona Dhiki Imewafika Mafarisayo Wanafiki?


    Viongozi wa ulimwengu wa dini wanapotea toka kwenye njia ya Bwana na kufuata mitindo ya kidunia, pia wao hushirikiana na uasi mkali wa mamlaka ya utawala na shutuma ya Umeme wa Mashariki, na tayari wameanza kutembea kwenye njia ya upinzani kwa Mungu. Ulimwengu wa dini umepotoka na kuwa mji wa Babeli.  Biblia inasema, "Na Yesu akaingia katika hekalu la Mungu, na akawafukuza wote waliokuwa wakiuza na kununua katika hekalu, na akazipindua meza za wabadilishaji wa fedha, na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa, Na akawaambia, imeandikwa, nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala; lakini mmeifanya pango la wezi" (Mathayo 21:12-13). "Babeli kuu imeanguka, imeanguka, na imekuwa makazi ya pepo, ngome ya kila pepo mwovu, na tundu la kila ndege mchafu na wa kuchukiza. Kwani mataifa yote yamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa ulimwengu wamefanya naye uasherati, na wafanya biashara wa ulimwengu wametajirika kupitia kwa utele wa uzuri wake" (Ufunuo 18:2-3).


    Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni