10.29.2018

Kutembea Katika Njia ya Kumpenda Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Nyimbo, Injili

 Kutembea Katika Njia ya Kumpenda Mungu

Sijali kuhusu njia iliyo mbele;
nafanya tu mapenzi ya Mungu kama wito wangu.
Wala sijali kuhusu maisha yangu ya usoni.
Kwa kuwa nimechagua kumpenda Mungu, nitakuwa mwaminifu hadi mwisho. 
Bila kujali jinsi hatari na ugumu ulivyo mkubwa,
ama jinsi njia ilivyo na mabonde na isiyo laini mbele,
Kwa kuwa nalenga siku ambayo Mungu atapata utukufu,
Nitatupa kila kitu na kutia bidii kusonga mbele.
Je, umewahi kufikiria jinsi Mungu alivyo na wasiwasi?
Jinsi ya kushirikiana na Mungu ili kugawa mashaka Yake?
Nitafikiria zaidi jinsi ya kumfariji Mungu.
Kwani nataka kumpenda Mungu, nitajitoa mwenyewe.
Ni wakati wetu wa kuwa waminifu kwa Mungu; tutateseka kwa kumshuhudia Yeye.
Mungu ameteseka sana kwa ajili yetu; ni wakati wa kulipa upendo Wake.
Ndugu, hebu tusimame.
Hakuna yeyote ama chochote kinachoweza kutuzuia kumpenda Mungu.
Wacha kila kitu na uwe muaminifu kwa Mungu, ili aweze kupumzika mapema.
Tukaribishe siku ambayo Mungu anapata utukufu, siku ambayo Mungu anapata utukufu.

kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

     Sikiliza zaidi: Kanisa la Mwenyezi Mungu nyimbo za injil

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni