7.18.2018

Mungu Ameonekana Mashariki mwa Dunia na Utukufu

 Mungu Ameonekana Mashariki mwa Dunia na Utukufu

Mungu anafanya kazi ulimwenguni kote.
Kelele za radi ya Mashariki hazipungui,
Zikitikisa madhehebu na makundi yote.
Ni sauti ya Mungu iliyoleta vyote wakati wa sasa.
Ni sauti Yake ndiyo itashinda kila kitu.
Wanaanguka katika mtiririko huu, na kumtii Yeye.
Mungu ameshachukua utukufu kutoka duniani kitambo,
na kutoka Mashariki Ameutoa tena.
Ni nani asiyetamani sana kuuona utukufu wa Mungu?
Ni nani asiyengoja kurudi Kwake kwa hamu?
Ni nani asiyekuwa na kiu ya kuonekana Kwake tena?
Ni nani asiyekosa uzuri Wake?
Ni nani ambaye hangeweza kuja katika mwangaza?
Ni nani hangeweza kuona utajiri wa Kanaani?
Ni nani asiyetamani sana kurudi kwa Mkombozi?
Ni nani asiyetamani Yule mwenye kudura?
Sauti ya Mungu lazima isambae katika nchi nzima.
Kwa watu Wake wateule, Ana maneno zaidi ya kuzungumza.
Kama radi kubwa inayotikisa milima na mito,
Anaunenea ulimwengu mzima na binadamu wote.
Hivyo maneno ya Mungu yanakuwa hazina ya mwanadamu.
Maneno Yake yanapendwa kwa dhati na wote.
Radi inaangaza moja kwa moja kutoka Mashariki mpaka Magharibi.
Maneno ya Mungu yanawafanya watu wachukie kuyaacha.
Maneno ya Mungu ni yasiyoeleweka lakini yanaleta furaha.
Wanadamu wote wanafurahia na kusherehekea Mungu kuja, kama tu vile mtoto mchanga.
Sauti ya Mungu inawavutia watu kuelekea Kwake.
Mungu anaingia kirasmi miongoni mwa wanadamu tangu sasa na kuendelea.
Wanadamu wote wanakuja kumwabudu kwa ajili ya hili.
Kwa sababu ya utukufu na maneno ambayo Mungu anatoa,
wote wanakuja mbele ya Mungu na kuuona umeme kutoka Mashariki.
Mungu ameshuka katika “Mlima wa Mizeituni” katika Mashariki.
Amekuwa hapa duniani kwa muda mrefu, si tena Mwana wa Wayahudi.
Yeye ni Umeme wa Mashariki, kwa kuwa Mungu amefufuka.
Aliwaacha wanadamu na sasa Ameonekana tena, Aliyejaa utukufu.
Mungu ni Yule aliyeabudiwa kabla ya enzi,
mtoto aliyetelekezwa na Waisraeli kutoka katika awamu hiyo.
Yeye ndiye Mwenyezi Mungu mwenye utukufu wote na wa enzi mpya!
Yote Anayotaka kufakinisha si mengine ila haya:
Watu wote wanakuja mbele ya kiti cha enzi cha Mungu,
kuona uso Wake na matendo, kusikia sauti Yake.
Ni mwisho na kilele cha mpango Wake,
na kusudi la mpango wa usimamizi wa Mungu.
Hivyo mataifa yote yanamwabudu na kumtambua Yeye.
Watu wote wanamwamini na wako chini Yake!
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Tazama video Nyimbo za Neno la Mungu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni